Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kitabu cha Yobu

Sura

Habari Zenye Kuwa Ndani

  • 1

    • Uaminifu-mushikamanifu na utajiri wa Yobu (1-5)

    • Shetani anatilia mashaka nia ya Yobu (6-12)

    • Yobu anapoteza mali na watoto wake (13-19)

    • Yobu hamulaumu Mungu (20-22)

  • 2

    • Shetani anatilia tena mashaka nia ya Yobu (1-5)

    • Shetani anaruhusiwa kupiga mwili wa Yobu (6-8)

    • Bibi ya Yobu: “Laani Mungu na ukufe!” (9, 10)

    • Marafiki watatu wa Yobu wanafika (11-13)

  • 3

    • Yobu analaani siku yenye alizaliwa (1-26)

      • Anauliza sababu gani anateseka (20, 21)

  • 4

    • Hotuba ya kwanza ya Elifazi (1-21)

      • Anachekelea uaminifu-mushikamanifu wa Yobu (7, 8)

      • Anaeleza ujumbe wa kiumbe fulani wa roho (12-17)

      • ‘Mungu hana imani katika watumishi wake’ (18)

  • 5

    • Hotuba ya kwanza ya Elifazi inaendelea (1-27)

      • ‘Mungu ananasa wenye hekima katika ujanja wao’ (13)

      • ‘Yobu hapaswe kukataa nizamu ya Mungu’ (17)

  • 6

    • Jibu la Yobu (1-30)

      • Anasema kuwa iko na sababu ya kulia (2-6)

      • Wafariji wake ni wajanja (15-18)

      • “Maneno ya kweli hayaumize!” (25)

  • 7

    • Yobu anaendelea kujibu (1-21)

      • Maisha ni kama kazi ya kulazimishwa (1, 2)

      • “Sababu gani umenifanya kuwa shabaha yako?” (20)

  • 8

    • Hotuba ya kwanza ya Bildadi (1-22)

      • Anaonyesha kwamba wana wa Yobu wamefanya zambi (4)

      • ‘Kama ungekuwa safi, Mungu angekulinda’ (6)

      • Anaonyesha kwamba Yobu hamuogope Mungu (13)

  • 9

    • Jibu la Yobu (1-35)

      • Mwanadamu mwenye anaweza kufa hawezi kushindana na Mungu (2-4)

      • ‘Mungu anafanya mambo yenye hayawezi kuchunguzwa’ (10)

      • Mutu hawezi kubishana na Mungu (32)

  • 10

    • Yobu anaendelea kujibu (1-22)

      • ‘Sababu gani Mungu anashindana na mimi?’ (2)

      • Mungu iko tofauti na mwanadamu Yobu mwenye anaweza kufa (4-12)

      • ‘Ninaweza kupata kitulizo kidogo’ (20)

  • 11

    • Hotuba ya kwanza ya Sofari (1-20)

      • Anamushitaki Yobu kwa sababu ya maneno yake yenye hayana maana (2, 3)

      • Anamuambia Yobu aache uovu (14)

  • 12

    • Jibu la Yobu (1-25)

      • “Mimi siko mudogo kuliko ninyi” (3)

      • “Nimekuwa kitu cha kuchekwa” (4)

      • ‘Mungu iko na hekima’ (13)

      • Mungu iko juu kuliko waamuzi na wafalme (17, 18)

  • 13

    • Yobu anaendelea kujibu (1-28)

      • ‘Afazali ningezungumuza na Mungu’ (3)

      • ‘Ninyi ni waganga wenye hawana faida yoyote’ (4)

      • “Ninajua kwamba niko na haki” (18)

      • Anauliza sababu gani Mungu anamuona kuwa adui (24)

  • 14

    • Yobu anaendelea kujibu (1-22)

      • Maisha ya mwanadamu ni mafupi na yamejaa taabu (1)

      • “Kuko tumaini hata kwa ajili ya muti” (7)

      • “Ingekuwa muzuri kama ungenificha katika Kaburi!” (13)

      • “Mutu akikufa, je, anaweza kuishi tena?” (14)

      • Mungu atatamani sana kazi ya mikono yake (15)

  • 15

    • Hotuba ya pili ya Elifazi (1-35)

      • Anasema kwamba Yobu hamuogope Mungu (4)

      • Anasema kwamba Yobu iko na kimbelembele (7-9)

      • ‘Mungu hana imani katika watakatifu wake’ (15)

      • ‘Mutu mwenye kuteseka ni muovu’ (20-24)

  • 16

    • Jibu la Yobu (1-22)

      • ‘Ninyi ni wafariji wenye kusumbua!’ (2)

      • Anasema kwamba Mungu anamufanya kuwa shabaha yake (12)

  • 17

    • Yobu anaendelea kujibu (1-16)

      • “Watu wenye kufanya zihaka wananizunguka” (2)

      • “Amenifanya kuwa kitu cha kuzarauliwa” (6)

      • “Kaburi litakuwa nyumba yangu” (13)

  • 18

    • Hotuba ya pili ya Bildadi (1-21)

      • Anaeleza mambo yenye yatapata waovu (5-20)

      • Anasema kwamba Yobu hamujue Mungu (21)

  • 19

    • Jibu la Yobu (1-29)

      • Anakataa makaripio ya “marafiki” wake (1-6)

      • Anasema kwamba ameachwa (13-19)

      • “Mukombozi wangu iko muzima” (25)

  • 20

    • Hotuba ya pili ya Sofari (1-29)

      • Anajisikia kuwa Yobu amemutukana (2, 3)

      • Anaonyesha kwamba Yobu ni muovu (5)

      • Anasema kwamba Yobu anafurahia zambi (12, 13)

  • 21

    • Jibu la Yobu (1-34)

      • ‘Sababu gani waovu wako na maisha ya muzuri?’ (7-13)

      • Anaonyesha waziwazi ujanja wa “wafariji” wake (27-34)

  • 22

    • Hotuba ya tatu ya Elifazi (1-30)

      • ‘Mwanadamu anaweza kuwa na faida gani kwa Mungu?’ (2, 3)

      • Anamushitaki Yobu kwamba ni mutu wa pupa na hatende kwa haki (9)

      • ‘Umurudilie Mungu ili urudishwe katika hali ya muzuri’ (23)

  • 23

    • Jibu la Yobu (1-17)

      • Anataka kupeleka kesi yake ya hukumu mbele ya Mungu (1-7)

      • Anasema kwamba hawezi kumupata Mungu (8, 9)

      • “Nimefuata njia yake bila kugeukia upande mwingine” (11)

  • 24

    • Yobu anaendelea kujibu (1-25)

      • ‘Sababu gani Mungu haweke wakati?’ (1)

      • Anasema kwamba Mungu ameruhusu uovu (12)

      • Watenda-zambi wanapenda giza (13-17)

  • 25

    • Hotuba ya tatu ya Bildadi (1-6)

      • ‘Namna gani mutu anaweza kuwa bila kosa mbele ya Mungu?’ (4)

      • Anasema kwamba uaminifu-mushikamanifu wa mwanadamu ni wa bure (5, 6)

  • 26

    • Jibu la Yobu (1-14)

      • “Mumemusaidia mutu mwenye hana nguvu kabisa!” (1-4)

      • ‘Mungu ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu’ (7)

      • ‘Sehemu za pembeni-pembeni tu za njia za Mungu’ (14)

  • 27

    • Yobu anaazimia kuendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu (1-23)

      • “Sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu” (5)

      • Mutu mwenye hamuogope Mungu hana tumaini (8)

      • “Sababu gani munasema mambo yenye hayana maana kabisa?” (12)

      • Muovu hatabakia na kitu (13-23)

  • 28

    • Yobu anaonyesha tofauti kati ya hazina za dunia na hekima (1-28)

      • Bidii za wanadamu za kuchimba majiwe yenye samani (1-11)

      • Hekima iko na samani kubwa kuliko lulu (18)

      • Kumuogopa Yehova ndiyo hekima ya kweli (28)

  • 29

    • Yobu anakumbuka namna alikuwa na maisha ya muzuri mbele ateseke (1-25)

      • Aliheshimiwa kwenye mulango mukubwa wa muji (7-10)

      • Namna alitembea kwa haki zamani (11-17)

      • Kila mutu alisikiliza mashauri yake (21-23)

  • 30

    • Yobu anaeleza namna maisha yake yalibadilika (1-31)

      • Anachekwa na watu wenye hawana mafaa yoyote (1-15)

      • Inaonekana kama Mungu hamusaidie (20, 21)

      • “Ngozi yangu imekuwa nyeusi” (30)

  • 31

    • Yobu anatetea uaminifu-mushikamanifu wake (1-40)

      • “Agano na macho yangu” (1)

      • Anamuomba Mungu amupime kwenye mizani (6)

      • Yeye haiko muzinifu (9-12)

      • Yeye haiko mupenda-feza (24, 25)

      • Yeye haiko muabudu-sanamu (26-28)

  • 32

    • Kijana Elihu anaanza kuzungumuza (1-22)

      • Anakasirikia Yobu na marafiki wake (2, 3)

      • Alingojea kwa heshima mbele ya kuzungumuza (6, 7)

      • Haiko kuishi miaka mingi tu ndiyo inafanya mutu kuwa na hekima (9)

      • Elihu anatamani sana kuongea (18-20)

  • 33

    • Elihu anamukaripia Yobu kwa sababu yeye anajiona kuwa mwenye haki (1-33)

      • Bei ya ukombozi inapatikana (24)

      • Kuwa tena na nguvu za wakati wa ujana (25)

  • 34

    • Elihu anatetea haki na njia za Mungu (1-37)

      • Yobu anasema kwamba Mungu alimuima haki (5)

      • Mungu wa kweli hawezi hata kidogo kutenda uovu (10)

      • Yobu anakosa ujuzi (35)

  • 35

    • Elihu anaonyesha mawazo yenye makosa ya Yobu (1-16)

      • Yobu anasema yeye iko mwenye haki kuliko Mungu (2)

      • Mungu iko juu sana, zambi haiwezi kumufanya kitu (5, 6)

      • Yobu anapaswa kumungojea Mungu (14)

  • 36

    • Elihu anatukuza ukubwa wa Mungu wenye hauwezi kuchunguzwa (1-33)

      • Wenye kutiii wanakuwa na maisha ya muzuri; wenye hawamuogope Mungu wanakataliwa (11-13)

      • ‘Ni mwalimu gani anaweza kufundisha kama Mungu?’ (22)

      • Yobu anapaswa kumutukuza Mungu (24)

      • “Mungu ni mukubwa kuliko namna tunaweza kujua” (26)

      • Mungu anaongoza mvua na umeme wa radi (27-33)

  • 37

    • Nguvu za asili zinafunua ukubwa wa Mungu (1-24)

      • Mungu anaweza kusimamisha kazi za wanadamu (7)

      • ‘Ufikiri sana juu ya kazi za ajabu za Mungu’ (14)

      • Wanadamu hawawezi kumuelewa kabisa Mungu (23)

      • Hakuna mwanadamu mwenye anapaswa kufikiri kwamba iko na hekima (24)

  • 38

    • Yehova anafundisha juu ya udogo wa mwanadamu (1-41)

      • ‘Ulikuwa wapi wakati dunia iliumbwa?’ (4-6)

      • Wana wa Mungu walipandisha sauti za shangwe (7)

      • Maulizo juu ya maajabu ya asili (8-32)

      • “Sheria zenye zinaongoza mbingu” (33)

  • 39

    • Namna wanyama wameumbwa inaonyesha ujinga wa mwanadamu (1-30)

      • Mbuzi wa milima na paa (1-4)

      • Punda wa pori (5-8)

      • Ngombe-dume wa pori (9-12)

      • Mbuni (13-18)

      • Farasi (19-25)

      • Kipanga na tai (26-30)

  • 40

    • Maulizo mengine yenye Yehova anauliza (1-24)

      • Yobu anakubali kama hana neno la kusema (3-5)

      • “Je, utatilia mashaka haki yangu?” (8)

      • Mungu anaeleza juu ya nguvu za Behemoti (15-24)

  • 41

    • Mungu anaeleza juu ya munyama wa ajabu mwenye kuitwa Leviatani (1-34)

  • 42

    • Yobu anamujibu Yehova (1-6)

    • Marafiki watatu wa Yobu wanalaumiwa (7-9)

    • Yehova anamurudisha Yobu katika hali ya muzuri (10-17)

      • Watoto wanaume na watoto wanamuke wa Yobu (13-15)