Kwa Wafilipi 2:1-30

  • Unyenyekevu wa Kikristo (1-4)

  • Unyenyekevu wa Kristo na kuinuliwa kwake (5-11)

  • Mufanyie kazi wokovu wenu wenyewe (12-18)

    • Kuangaza kama vitu vya kutoa mwangaza (15)

  • Kutuma Timoteo na Epafrodito (19-30)

2  Basi, kama kuko kitia-moyo chochote katika Kristo, kama kuko faraja yoyote ya upendo, kama kuko ushirika wowote wa kiroho,* kama kuko upendo wenye upole* wowote na huruma yoyote,  mufanye furaha yangu ijae kwa kuwa na akili ileile na kuwa na upendo uleule, mukiwa mumeunganishwa kabisa,* mukiwa na wazo moja katika akili.+  Musifanye jambo lolote kwa ugomvi+ ao kwa kutafuta sifa,+ lakini kwa unyenyekevu* muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi,+  mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu,+ lakini pia faida za we­ngine.+  Mukuwe na mutazamo huu wa akili ndani yenu wenye ulikuwa pia ndani ya Kristo Yesu,+  mwenye, hata kama alikuwa katika umbo ya Mungu,+ hakufikiria kuchukua nafasi ya Mungu, ni kusema, kwamba yeye akuwe sawa na Mungu.+  Hapana, lakini alijiondolea hali yake na akachukua umbo ya mutumwa+ na kuwa mwanadamu.*+  Zaidi ya hayo, wakati alikuja akiwa mwanadamu,* alijinyenyekeza mwenyewe na kuwa mutiifu mupaka kifo,+ ndiyo, kifo kwenye muti wa mateso.*+  Kwa sababu hiyo, Mungu alimuinua kwenye cheo cha juu zaidi+ na kumupatia kwa fazili jina lenye kuwa juu zaidi ya kila jina lingine,+ 10  ili katika jina la Yesu kila goti lipigwe​—la wale wenye kuwa mbinguni na la wale wenye kuwa duniani na la wale wenye kuwa chini ya udongo+​— 11  na kila ulimi ukubali waziwazi kama Yesu Kristo ni Bwana+ kwa utukufu wa Mungu Baba. 12  Kwa hiyo, wapendwa wangu, kama vile mumekuwa mukitii sikuzote, haiko tu wakati niko pamoja na ninyi, lakini kwa utayari zaidi sasa wakati siko pamoja na ninyi, muendelee kufanyia kazi wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. 13  Kwa maana Mungu ndiye kwa ajili ya mapenzi yake mema anawachochea ninyi, na kuwapatia hamu na pia nguvu za kutenda. 14  Muendelee kufanya mambo yote bila kunungunika+ na kubishana,+ 15  ili mufikie kuwa bila lawama na bila kosa, watoto wa Mungu+ wenye hawana kasoro katikati ya kizazi chenye kuharibika na chenye kupotoka,+ wenye kati yao munaangaza kama vitu vya kutoa mwangaza katika ulimwengu,+ 16  mukiendelea kushika sana neno la uzima.+ Kisha nitakuwa na sababu ya kushangilia katika siku ya Kristo, nikijua kwamba sikukimbia bure ao sikufanya kazi kwa bidii bure. 17  Hata hivyo, hata kama ninamwangwa kama toleo la kinywaji+ juu ya zabihu+ na utumishi mutakatifu* kwenye imani yenu imewaongoza, ninafurahi na kushangilia pamoja na ninyi wote. 18  Kwa njia ileile, ninyi pia munapaswa kufurahi na kushangilia pamoja na mimi. 19  Sasa ninatumaini katika Bwana Yesu kumutuma Timoteo+ kwenu haraka, ili nitiwe moyo wakati nitapata habari juu yenu. 20  Kwa maana sina mutu mwingine mwenye kuwa na muelekeo kama wake mwenye atajali kabisa mahangaiko yenu. 21  Kwa maana wengine wote wanatafuta faida zao wenyewe, hapana faida za Yesu Kristo. 22  Lakini ninyi munajua uhakikisho wenye alitoa juu yake mwenyewe, kwamba kama mutoto+ na baba yake alitumika pamoja na mimi ili kuendeleza habari njema. 23  Kwa hiyo, yeye ndiye ninatumaini kutuma wakati tu nitaona namna mambo yatakuwa kunihusu mimi. 24  Kwa kweli, niko na uhakika katika Bwana kwamba mimi mwenyewe pia nitakuja hivi karibuni.+ 25  Lakini sasa ninaona ni lazima nimutume kwenu Epafrodito, ndugu yangu na mufanyakazi mwenzangu na askari mwenzangu, na mujumbe wenu na mutumishi wa wangu mwenyewe kwa ajili ya mahitaji yangu,+ 26  kwa kuwa anatamani kuwaona ninyi wote na ameshuka moyo kwa sababu mulisikia alikuwa mugonjwa. 27  Kwa hakika, alikuwa mugonjwa karibu kufa; lakini Mungu alimusikilia huruma, kwa kweli, hakumusikilia huruma yeye tu lakini mimi pia, ili nisipatwe na huzuni juu ya huzuni. 28  Kwa hiyo, ninamutuma mbio sana, ili wakati mutamuona mufurahi tena na mimi nipunguziwe wasiwasi. 29  Basi mumukaribishe kulingana na desturi katika Bwana kwa furaha yote, na muendelee kuheshimia watu wa namna hiyo,+ 30  kwa kuwa alikaribia kufa kwa sababu ya kazi ya Kristo,* akitia uzima wake katika hatari* ili anitolee utumishi wa kipekee pa nafasi yenu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ushirika wowote wa roho.”
Ao “upendo mwororo.”
Ao “mukiwa mumeunganishwa pamoja katika nafsi.”
Ao “unyenyekevu wa akili.”
Tnn., “na akakuwa kama wanadamu.”
Tnn., “wakati alipatikana katika umbo ya mwanadamu.”
Ao “utumishi wa watu wote.”
Ao pengine, “kazi ya Bwana.”
Ao “akitia nafsi yake katika hatari.”