Kwa Tito 3:1-15

  • Ujitiisho wa kweli (1-3)

  • Ukuwe tayari kwa ajili ya matendo ya muzuri (4-8)

  • Epuka mabishano ya upumbavu na mazehebu (9-11)

  • Maagizo ya Paulo kwa Tito na salamu (12-15)

3  Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kutii serikali na mamlaka,+ wakuwe tayari kwa ajili ya kila kazi ya muzuri,  wasiseme mubaya juu ya mutu yeyote, wasikuwe wagomvi, lakini wakuwe na usawaziko,+ na wakuwe wapole kuelekea watu wote.+  Kwa sababu hata sisi wakati fulani tulikuwa wapumbavu, watu wenye hawatii, wenye kupotoshwa, watumwa wa tamaa na raha mbalimbali, na tuliendelea katika ubaya na wivu, tulikuwa wenye kuchukiza, na wenye kuchukiana.  Lakini, wakati Mwokozi wetu, Mungu,+ alionyesha fazili na upendo wake kwa wanadamu  (haikukuwa kwa sababu ya matendo yoyote yenye haki yenye tulikuwa tumefanya,+ lakini kwa sababu ya rehema yake),+ alituokoa kupitia kutuosha kwenye kulituleta katika uzima,+ na kwa kutufanya wapya kupitia roho takatifu.+  Alimwanga roho hii kwa wingi* juu yetu kupitia Yesu Kristo Mwokozi wetu,+  ili kisha kutangazwa kuwa wenye haki kupitia fazili zake zenye hazistahiliwe,+ tukuwe wariti+ kulingana na tumaini la uzima wa milele.+  Maneno haya ni yenye kutegemeka, na ninataka uendelee kutilia mukazo mambo hayo, ili wale wenye wamemuamini Mungu waendelee kukaza akili zao juu ya kufanya matendo ya muzuri. Mambo haya ni ya muzuri na yenye faida kwa watu.  Lakini epuka mabishano ya upumbavu na ukoo mbalimbali na magomvi na mapigano juu ya Sheria, kwa sababu mambo hayo hayana faida na ni ya bure.*+ 10  Mutu mwenye anaendeleza zehebu,*+ umuepuke+ kisha kumuonya* mara ya kwanza na mara ya pili,+ 11  ukijua kwamba mutu wa namna hiyo ameacha njia yenye inafaa na anafanya zambi, na amejihukumu yeye mwenyewe. 12  Wakati nitamutuma Artema ao Tikiko+ kwako, fanya nguvu yako yote ukuje kwangu katika Nikopoli, kwa maana nimeamua kupitisha kule kipindi cha baridi. 13  Ujikaze kabisa kumusaidia Zena, mwenye kujua sana Sheria, na Apolo pia ili wasikose kitu chochote kwa ajili ya safari yao.+ 14  Lakini acha watu wetu pia wajifunze kuendelea kufanya matendo ya muzuri ili wasaidie wakati kunatokea uhitaji wa haraka,+ na hivyo wasikuwe watu wenye hawazae matunda.+ 15  Wale wote wenye kuwa na mimi wanakutumia salamu zao. Upatie salamu zangu wale wenye kutupenda, wenye kuwa katika imani. Fazili zenye hazistahiliwe zikuwe pamoja na ninyi wote.

Maelezo ya Chini

Ao “kwa ukarimu.”
Ao “ubatili.”
Ao “kumushauri.”