Ya Kwanza kwa Wakorinto 11:1-34

  • “Mukuwe waigaji wangu” (1)

  • Ukichwa na kufunika kichwa (2-16)

  • Kukumbuka Chakula cha Mangaribi cha Bwana (17-34)

11  Mukuwe waigaji wangu, kama vile mimi niko muigaji wa Kristo.+  Ninawapongeza ninyi kwa sababu katika mambo yote munanikumbuka na munashika sana desturi kama vile niliwapatia ninyi.  Lakini ninataka mujue kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo;+ na kichwa cha mwanamuke ni mwanaume;+ na kichwa cha Kristo ni Mungu.+  Kila mwanaume mwenye anasali ao kutoa unabii akiwa na kitu juu ya kichwa chake anapatisha haya kichwa chake;  lakini kila mwanamuke mwenye anasali ao kutoa unabii+ bila kufunika kichwa chake anapatisha haya kichwa chake, kwa maana ni kama vile yeye ni mwanamuke mwenye kichwa chenye kunyolewa.  Kwa maana kama mwanamuke hajifunike, anapaswa kukatwa nywele zake; lakini kama ni haya kwa mwanamuke kukatwa nywele ao kunyolewa, anapaswa kujifunika.  Kwa maana mwanaume hapaswe kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mufano na utukufu wa Mungu,+ lakini mwanamuke ni utukufu wa mwanaume.  Kwa maana mwanaume hakutoka katika mwanamuke, lakini mwanamuke alitoka katika mwanaume.+  Na zaidi ya hayo, mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamuke, lakini mwanamuke aliumbwa kwa ajili ya mwanaume.+ 10  Ndiyo sababu mwanamuke anapaswa kuwa na alama ya mamlaka juu ya kichwa chake, kwa sababu ya malaika.+ 11  Tena, kuhusiana na Bwana, mwanamuke hatenganishwe na mwanaume na mwanaume hatenganishwe na mwanamuke. 12  Kwa maana kama vile mwanamuke alitoka katika mwanaume,+ vilevile pia mwanaume iko* kupitia mwanamuke; lakini vitu vyote vimetoka kwa Mungu.+ 13  Muhukumu ninyi wenyewe: Je, inafaa mwanamuke kusali kwa Mungu bila kufunika kichwa chake? 14  Je, maumbile yenyewe hayawafundishe ninyi kwamba nywele za murefu ni haya kwa mwanaume, 15  lakini kama mwanamuke iko* na nywele za murefu, ni utukufu kwake? Kwa maana amepewa nywele zake zikuwe kitu cha kujifunika. 16  Hata hivyo, kama mutu yeyote anataka kubishana ili kutetea desturi ingine, sisi hatuna desturi ingine, na hata makutaniko ya Mungu. 17  Lakini wakati ninatoa maagizo haya, siwapongeze ninyi, kwa sababu munakutana pamoja, haiko kwa ajili ya wema, lakini kwa ajili ya ubaya. 18  Kwa maana, kwanza kabisa, ninasikia kwamba wakati munakutana pamoja katika kutaniko, kuko migawanyiko katikati yenu; na kwa kadiri fulani ninaamini jambo hilo. 19  Kwa maana lazima kutakuwa pia mazehebu* katikati yenu,+ ili wale wenye wanakubaliwa wafunuliwe pia. 20  Wakati munakutana mahali pamoja, kwa kweli haiko kwa sababu ya kula Chakula cha Mangaribi cha Bwana.+ 21  Kwa maana wakati munakikula, kila mutu anatangulia kula chakula chake mwenyewe cha mangaribi, hivi kwamba mumoja iko* na njaa lakini mwingine amelewa. 22  Je, hamuna nyumba za kukulia chakula na kukunywea ndani? Ao je, munazarau kutaniko la Mungu na kupatisha haya wale wenye hawana kitu? Niwaambie nini? Niwapongeze? Juu ya jambo hilo, siwapongeze ninyi. 23  Kwa maana nilipokea kutoka kwa Bwana kile chenye niliwapatia ninyi pia, kwamba Bwana Yesu katika usiku+ wenye angesalitiwa, alichukua mukate, 24  na kisha kutoa shukrani, akauvunja na kusema: “Huu unamaanisha mwili wangu,+ wenye uko kwa ajili yenu. Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”+ 25  Akafanya vilevile na kikombe+ pia, kisha wao kula chakula cha mangaribi, akisema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano jipya+ kwa musingi wa damu yangu.+ Muendelee kufanya hivi, kila wakati wenye munakikunywa, kwa kunikumbuka mimi.”+ 26  Kwa maana kila wakati wenye munakula mukate huu na kunywa kikombe hiki, munaendelea kutangaza kifo cha Bwana, mupaka wakati atakuja. 27  Kwa hiyo, mutu yeyote mwenye anakula mukate ao kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili atakuwa na hatia kuhusiana na mwili na damu ya Bwana. 28  Kwanza, mutu ajichunguze mwenyewe na kuona kama anastahili,+ na kisha akule mukate na akunywe kikombe. 29  Kwa maana ule mwenye anakula na kunywa bila kutambua mwili, anakula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe. 30  Ndiyo sababu wengi kati yenu ni wazaifu na wagonjwa, na wengi wamelala usingizi katika kifo.*+ 31  Lakini kama tungetambua sisi wenyewe ni nani, hatungehukumiwa. 32  Hata hivyo, wakati tunahukumiwa, tunatiwa nizamu na Yehova,*+ ili tusihukumiwe pamoja na ulimwengu.+ 33  Kwa hiyo, ndugu zangu, wakati munakutana pamoja ili kula chakula hicho, kila mumoja amungojee mwenzake. 34  Kama mutu yeyote iko* na njaa, akule kwenye nyumba yake, ili wakati munakutana pamoja isikuwe kwa ajili ya hukumu.+ Lakini kuhusu mambo yenye yanabakia, nitayatengeneza wakati nitafika kule.

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “eko.”
Uwingi wa zehebu. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Inaonekana ni kifo cha kiroho.
Ao “eko.”