Ya Kwanza ya Petro 3:1-22

  • Bibi na bwana (1-7)

  • Musikie maumivu ya wengine; mutafute amani (8-12)

  • Kuteseka kwa sababu ya haki (13-22)

    • Mukuwe tayari kutetea tumaini lenu (15)

    • Ubatizo na zamiri ya muzuri (21)

3  Kwa njia ileile, ninyi bibi, mujitiishe kwa bwana zenu,+ ili kama kuko wale wenye hawatii lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa bibi zao,+  kwa sababu wameshuhudia kwa macho yao mwenendo wenu wenye kuwa safi+ pamoja na heshima kubwa.  Kujipamba kwenu kusikuwe kwa inje​—kusuka nywele na kuvaa mapambo ya zahabu+ ao nguo za muzuri—  lakini kukuwe ule mutu wa siri wa ndani ya moyo katika mapambo yenye hayawezi kuharibika ya roho ya utulivu na ya upole,+ yenye samani kubwa mbele ya macho ya Mungu.  Kwa maana ni vile wanamuke watakatifu wa zamani wenye kutumaini Mungu walikuwa wanajipamba, walikuwa wanajitiisha kwa bwana zao,  kama vile Sara alimutii Abrahamu, akimuita bwana.+ Na ninyi mumekuwa watoto wake, kama tu munaendelea kutenda mema na hamuogope.+  Ninyi bwana, katika njia ileile, muendelee kukaa nao kulingana na ujuzi.* Muwapatie heshima+ kama chombo kizaifu zaidi, ni kusema, mwanamuke, kwa kuwa wao pia ni wariti pamoja na ninyi+ wa pendeleo la uzima lenye mulipewa bure, ili sala zenu zisizuiwe.  Mwishowe, ninyi wote mukuwe na umoja wa akili,*+ mujitie pa nafasi ya wengine, mukuwe na upendo wa kindugu, huruma yenye upole,*+ na unyenyekevu.+  Musilipe ubaya kwa ubaya+ ao matukano kwa matukano.+ Tofauti na hilo, mulipe kwa kubariki,+ kwa maana muliitwa kwenye njia hii, ili muriti baraka. 10  Kwa maana “mutu yeyote mwenye anapenda uzima na kuona siku njema, anapaswa kulinda ulimi wake kutokana na ubaya+ na midomo yake isiseme udanganyifu. 11  Ageuke na kuacha mambo ya mubaya+ na afanye mambo ya muzuri;+ atafute amani na kuifuatilia.+ 12  Kwa maana macho ya Yehova* yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza sala yao ya kumulilia Mungu,*+ lakini uso wa Yehova* unapinga wale wenye kutenda mambo ya mubaya.”+ 13  Kwa kweli, ni nani mwenye atawatendea mubaya kama munakuwa na bidii kwa ajili mambo ya muzuri?+ 14  Lakini hata kama munateseka kwa sababu ya haki, ninyi ni wenye furaha.+ Hata hivyo, musiogope kile wanaogopa,* na musivurugike.+ 15  Lakini mumutakase Kristo kuwa Bwana katika mioyo yenu, na sikuzote mukuwe tayari kujitetea mbele ya kila mutu mwenye anawauliza ninyi sababu ya tumaini lenye muko nalo, lakini mufanye vile kwa upole+ na heshima kubwa.+ 16  Muendelee kuwa na zamiri ya muzuri,+ ili katika kila njia yenye wanasema mubaya juu yenu, wale wenye wanasema mubaya juu yenu wapate haya+ kwa sababu ya mwenendo wenu muzuri mukiwa wafuasi wa Kristo.+ 17  Kwa maana ni muzuri zaidi kuteseka kwa sababu munatenda mema,+ kama ni mapenzi ya Mungu kuruhusu jambo hilo, kuliko kuteseka kwa sababu munatenda maovu.+ 18  Kwa maana Kristo alikufa mara moja kwa wakati wote kwa ajili ya zambi,+ mutu mwenye haki kwa ajili ya watu wenye hawako wenye haki,+ ili awaongoze ninyi kwa Mungu.+ Aliuawa katika mwili+ lakini akafanywa kuwa muzima katika roho.+ 19  Na katika hali hiyo alienda na kuhubiria roho wenye kuwa katika gereza,+ 20  wenye zamani hawakukuwa watiifu wakati Mungu alikuwa anangojea kwa uvumilivu* katika siku za Noa,+ wakati safina ilikuwa inajengwa,+ yenye ndani yake watu kidogo, ni kusema, nafsi* munane (8), walichukuliwa salama kupitia maji.+ 21  Ubatizo wenye unalingana na jambo hilo, unawaokoa ninyi sasa pia (haiko kuondoa uchafu wa mwili, lakini ombi lenye linatolewa kwa Mungu ili kupata zamiri ya muzuri),+ kupitia ufufuo wa Yesu Kristo. 22  Iko* kwenye mukono wa kuume wa Mungu,+ kwa maana alienda mbinguni, na malaika na mamlaka na nguvu vilitiishwa kwake.+

Maelezo ya Chini

Ao “na muwaonyeshe ufikirio; muwaelewe.”
Ao “huruma nyororo.”
Ao “mufikiri kwa upatano.”
Ao “dua yao.”
Ao pengine, “musiogope namna wanawaogopesha.”
Tnn., “uvumilivu wa Mungu ulikuwa unangojea.”
Ao “watu.”
Ao “Eko.”