Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unamruhusu Mungu Azungumze Nawe Kila Siku?

Je, Unamruhusu Mungu Azungumze Nawe Kila Siku?

UNAJIANGALIA mara ngapi katika kioo? Wengi wetu tumezoea kufanya hivyo kila siku, labda hata tunajiangalia mara nyingi kwa siku. Kwa nini? Kwa sababu tunahangaikia jinsi tunavyoonekana kwa nje.

Kusoma Biblia kunaweza kulinganishwa na kujiangalia katika kioo. (Yakobo 1:23-25) Ujumbe ambao umeandikwa katika Neno la Mungu una nguvu za kutuwezesha kuona jinsi tulivyo kikweli. ‘Unachoma hata kufikia kugawanya nafsi na roho.’ (Waebrania 4:12) Yaani, unagawanya au kutofautisha jinsi tunavyoonekana kwa nje na jinsi tulivyo kikweli kwa ndani. Ujumbe huo unatuonyesha marekebisho ambayo tunahitaji kufanya, kama vile tu kioo kinavyotuonyesha.

Biblia inafunua marekebisho tunayohitaji kufanya na pia inatusaidia kufanya marekebisho hayo. Mtume Paulo aliandika hivi: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu.” (2 Timotheo 3:16, 17) Ona kwamba kati ya hizo faida nne zinazotajwa, faida tatu, yaani, kukaripia, kunyoosha mambo, na kutia nidhamu, zinahusisha kurekebisha mtazamo na matendo yetu. Ikiwa tunahitaji kujiangalia kwa ukawaida katika kioo ili kuhakikisha kwamba sura yetu inakubalika, je, si jambo la maana hata zaidi kusoma Neno la Mungu, Biblia, kwa ukawaida?

Baada ya kumtia mafuta Yoshua ili aliongoze taifa la Israeli, Yehova Mungu alimwambia hivi: “Kitabu hiki cha sheria kisiondoke katika kinywa chako, nawe ukisome kwa sauti ya chini mchana na usiku, upate kuangalia kufanya kulingana na yote ambayo yameandikwa ndani yake; kwa maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha utatenda kwa hekima.” (Yoshua 1:8) Ndiyo, Yoshua alihitaji kusoma Neno la Mungu kwa ukawaida, “mchana na usiku,” ili aifanikishe njia yake.

Vivyo hivyo, zaburi ya kwanza inakazia faida za kusoma Biblia kwa ukawaida inaposema hivi: “Mwenye furaha ni mtu ambaye hakutembea katika shauri la waovu, na katika njia ya watenda-dhambi hakusimama, na katika kiti cha wenye dhihaka hakuketi. Bali mapendezi yake ni katika sheria ya Yehova, naye huisoma sheria yake kwa sauti ya chini mchana na usiku. Naye hakika atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao hutoa matunda yake katika majira yake na ambao majani yake hayanyauki, na kila jambo analofanya litafanikiwa.” (Zaburi 1:1-3) Bila shaka, tunataka kuwa kama mtu huyo.

Watu wengi wana zoea la kusoma Biblia kila siku. Mkristo mmoja alipoulizwa kwa nini anasoma Biblia kila siku, alijibu hivi: “Ikiwa ninasali kwa Mungu tena na tena kila siku na ninatazamia anisikilize, kwa nini mimi pia nisimsikilize Mungu kwa kusoma Neno lake kila siku? Ikiwa tunataka kuwa marafiki wazuri, basi hatupaswi kuongea tu bila kusikiliza.” Na hilo ni kweli. Kusoma Biblia ni kama tu kumsikiliza Mungu kwa sababu tunaposoma tunapata maoni yake kuhusu mambo mbalimbali.

Jinsi ya Kufaulu Kusoma Biblia Kila Siku

Labda tayari umejaribu kuanza programu ya kusoma Biblia. Je, umesoma Biblia nzima kuanzia mwanzo mpaka mwisho? Hiyo ndiyo njia bora kabisa ya kufahamu vizuri zaidi mambo yaliyomo. Hata hivyo, mara nyingi watu fulani wanaanza kusoma Biblia nzima, kisha wanaacha kusoma baada ya muda. Je, umekabili tatizo hilo? Unaweza kufanya nini ili ufikie mradi wa kusoma Biblia nzima? Kwa nini usijaribu kufuata mapendekezo mawili yafuatayo?

Panga kusoma Biblia kila siku. Chagua wakati unaofaa ambao unaweza kusoma Biblia kila siku. Pia, panga ratiba nyingine ya badala. Ikiwa kwa sababu fulani huwezi kusoma Biblia wakati ambao unapendelea, chagua wakati mwingine ili usikose kamwe kusoma Neno la Mungu hata siku moja. Kwa njia hiyo, utaiga mfano wa Waberoya wa zamani. Tunaambiwa hivi kuwahusu: “Walilipokea neno kwa hamu kubwa zaidi ya akili, wakiyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku ili kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo.”—Matendo 17:11.

Uwe na mradi hususa akilini. Kwa mfano, ukisoma sura tatu mpaka tano za Biblia kila siku, unaweza kuisoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja tu. Ratiba iliyo kwenye kurasa zinazofuata inaonyesha jinsi unavyoweza kufanya hivyo. Kwa nini usiazimie kujaribu kufuata ratiba hiyo? Chini ya kichwa “Tarehe,” panga wakati utakaposoma sura fulani. Kisha, katika kisanduku kilicho kando, tia alama sehemu ambazo umesoma. Kufanya hivyo kutakusaidia kuona maendeleo unayofanya.

Baada ya kusoma Biblia nzima, kwa nini uachie hapo? Unaweza kutumia ratiba hiyohiyo kusoma Biblia nzima kila mwaka, labda kila mara ukianza na sehemu tofauti. Au ikiwa ungependa kumaliza kusoma Biblia polepole zaidi, unaweza kusoma kila sehemu kwa siku mbili au tatu.

Kila mara unaposoma Biblia, utapata mambo mapya ambayo yanahusu maisha yako, mambo ambayo hujawahi kamwe kuona. Kwa nini? “Tamasha ya ulimwengu huu inabadilika,” na pia maisha na hali zetu zinabadilika-badilika. (1 Wakorintho 7:31) Basi, azimia kabisa kuangalia kila siku katika kioo cha Neno la Mungu, Biblia. Ukifanya hivyo, unaweza kuwa na hakika kwamba unamruhusu Mungu azungumze nawe kila siku.—Zaburi 16:8.

[Chati/Picha katika ukurasa wa 15-18]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

1

Ratiba ya Kusoma Biblia

MAAGIZO. Andika kwenye orodha tarehe ambazo unapanga kusoma kila sehemu. Tia alama kila sehemu unayomaliza kusoma. Unaweza kusoma vitabu vya Biblia kulingana na jinsi vinavyofuatana au unaweza kuchagua vichwa fulani ikitegemea sehemu zilizoonyeshwa. Ukisoma sehemu moja yenye sura kadhaa kila siku, utamaliza kusoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.

◆ Soma siku zilizotiwa alama NYEKUNDU yenye umbo la almasi ili uelewe maelezo ya kihistoria kuhusu shughuli za Mungu pamoja na Waisraeli.

● Soma siku zilizotiwa alama ya nukta kubwa ya BULUU ili uelewe mpangilio wa matukio katika ukuzi wa kutaniko la Kikristo.

2

VITABU VYA MUSA

TAREHE SURA □✔

/ MWANZO 1-3

/ 4-7

/ 8-11

/ ◆ 12-15

/ ◆ 16-18

/ ◆ 19-22

/ ◆ 23-24

/ ◆ 25-27

/ ◆ 28-30

/ ◆ 31-32

/ ◆ 33-34

/ ◆ 35-37

/ ◆ 38-40

/ ◆ 41-42

/ ◆ 43-45

/ ◆ 46-48

/ ◆ 49-50

/ KUTOKA ◆ 1-4

/ ◆ 5-7

/ ◆ 8-10

/ ◆ 11-13

/ ◆ 14-15

/ ◆ 16-18

/ ◆ 19-21

/ 22-25

/ 26-28

/ 29-30

/ ◆ 31-33

/ ◆ 34-35

/ 36-38

/ 39-40

/ MAMBO YA WALAWI 1-4

/ 5-7

/ 8-10

/ 11-13

/ 14-15

/ 16-18

/ 19-21

/ 22-23

/ 24-25

/ 26-27

/ HESABU 1-3

/ 4-6

/ 7-9

/ ◆ 10-12

/ ◆ 13-15

/ ◆ 16-18

/ ◆ 19-21

/ ◆ 22-24

/ ◆ 25-27

/ 28-30

/ ◆ 31-32

/ ◆ 33-36

/ KUMBUKUMBU 1-2

/ ◆ 3-4

/ 5-7

/ 8-10

/ 11-13

3

/ 14-16

/ ◆ 17-19

/ 20-22

/ 23-26

/ 27-28

/ ◆ 29-31

/ ◆ 32

/ ◆ 33-34

WAISRAELI WANAINGIA KATIKA NCHI YA AHADI

TAREHE SURA □✔

/ YOSHUA ◆ 1-4

/ ◆ 5-7

/ ◆ 8-9

/ ◆ 10-12

/ ◆ 13-15

/ ◆ 16-18

/ ◆ 19-21

/ ◆ 22-24

/ WAAMUZI ◆ 1-2

/ ◆ 3-5

/ ◆ 6-7

/ ◆ 8-9

/ ◆ 10-11

/ ◆ 12-13

/ ◆ 14-16

/ ◆ 17-19

/ ◆ 20-21

/ RUTHU ◆ 1-4

WAFALME WALIPOTAWALA ISRAELI

TAREHE SURA □✔

/ 1 SAMWELI ◆ 1-2

/ ◆ 3-6

/ ◆ 7-9

/ ◆ 10-12

/ ◆ 13-14

/ ◆ 15-16

/ ◆ 17-18

/ ◆ 19-21

/ ◆ 22-24

/ ◆ 25-27

/ ◆ 28-31

/ 2 SAMWELI ◆ 1-2

/ ◆ 3-5

/ ◆ 6-8

/ ◆ 9-12

/ ◆ 13-14

/ ◆ 15-16

/ ◆ 17-18

/ ◆ 19-20

/ ◆ 21-22

/ ◆ 23-24

/ 1 WAFALME ◆ 1-2

/ ◆ 3-5

/ ◆ 6-7

/ ◆ 8

/ ◆ 9-10

/ ◆ 11-12

4

/ 1 WAFALME (end.) ◆ 13-14

/ ◆ 15-17

/ ◆ 18-19

/ ◆ 20-21

/ ◆ 22

/ 2 WAFALME ◆ 1-3

/ ◆ 4-5

/ ◆ 6-8

/ ◆ 9-10

/ ◆ 11-13

/ ◆ 14-15

/ ◆ 16-17

/ ◆ 18-19

/ ◆ 20-22

/ ◆ 23-25

/ 1 M. YA NYAKATI 1-2

/ 3-5

/ 6-7

/ 8-10

/ 11-12

/ 13-15

/ 16-17

/ 18-20

/ 21-23

/ 24-26

/ 27-29

/ 2 M. YA NYAKATI 1-3

/ 4-6

/ 7-9

/ 10-14

/ 15-18

/ 19-22

/ 23-25

/ 26-28

/ 29-30

/ 31-33

/ 34-36

WAYAHUDI WANARUDI KUTOKA UHAMISHONI

TAREHE SURA □✔

/ EZRA ◆ 1-3

/ ◆ 4-7

/ ◆ 8-10

/ NEHEMIA ◆ 1-3

/ ◆ 4-6

/ ◆ 7-8

/ ◆ 9-10

/ ◆ 11-13

/ ESTA ◆ 1-4

/ ◆ 5-10

VITABU VYA MUSA

TAREHE SURA □✔

/ JOB 1-5

/ 6-9

/ 10-14

/ 15-18

/ 19-20

5

/ 21-24

/ 25-29

/ 30-31

/ 32-34

/ 35-38

/ 39-42

VITABU VYA NYIMBO NA MASHAURI YENYE HEKIMA

TAREHE SURA □✔

/ ZABURI 1-8

/ 9-16

/ 17-19

/ 20-25

/ 26-31

/ 32-35

/ 36-38

/ 39-42

/ 43-47

/ 48-52

/ 53-58

/ 59-64

/ 65-68

/ 69-72

/ 73-77

/ 78-79

/ 80-86

/ 87-90

/ 91-96

/ 97-103

/ 104-105

/ 106-108

/ 109-115

/ 116-119:63

/ 119:64-176

/ 120-129

/ 130-138

/ 139-144

/ 145-150

/ METHALI 1-4

/ 5-8

/ 9-12

/ 13-16

/ 17-19

/ 20-22

/ 23-27

/ 28-31

/ MHUBIRI 1-4

/ 5-8

/ 9-12

/ WIMBO WA SULEMANI 1-8

MANABII

TAREHE SURA □✔

/ ISAYA 1-4

/ 5-7

/ 8-10

6

/ ISAYA (endelea) 11-14

/ 15-19

/ 20-24

/ 25-28

/ 29-31

/ 32-35

/ 36-37

/ 38-40

/ 41-43

/ 44-47

/ 48-50

/ 51-55

/ 56-58

/ 59-62

/ 63-66

/ YEREMIA 1-3

/ 4-5

/ 6-7

/ 8-10

/ 11-13

/ 14-16

/ 17-20

/ 21-23

/ 24-26

/ 27-29

/ 30-31

/ 32-33

/ 34-36

/ 37-39

/ 40-42

/ 43-44

/ 45-48

/ 49-50

/ 51-52

/ MAOMBOLEZO 1-2

/ 3-5

/ EZEKIELI 1-3

/ 4-6

/ 7-9

/ 10-12

/ 13-15

/ 16

/ 17-18

/ 19-21

/ 22-23

/ 24-26

/ 27-28

/ 29-31

/ 32-33

/ 34-36

/ 37-38

/ 39-40

/ 41-43

/ 44-45

/ 46-48

/ DANIELI 1-2

/ 3-4

/ 5-7

/ 8-10

/ 11-12

7

/ HOSEA 1-7

/ 8-14

/ YOELI 1-3

/ AMOSI 1-5

/ 6-9

/ OBADIA/YONA

/ MIKA 1-7

/ NAHUM/HABAKKUK

/ SEFANIA/HAGAI

/ ZEKARIA 1-7

/ 8-11

/ 12-14

/ MALAKI 1-4

MASIMULIZI YA MAISHA NA HUDUMA YA YESU

TAREHE SURA □✔

/ MATHAYO 1-4

/ 5-7

/ 8-10

/ 11-13

/ 14-17

/ 18-20

/ 21-23

/ 24-25

/ 26

/ 27-28

/ MARKO ● 1-3

/ ● 4-5

/ ● 6-8

/ ● 9-10

/ ● 11-13

/ ● 14-16

/ LUKA 1-2

/ 3-5

/ 6-7

/ 8-9

/ 10-11

/ 12-13

/ 14-17

/ 18-19

/ 20-22

/ 23-24

/ YOHANA 1-3

/ 4-5

/ 6-7

/ 8-9

/ 10-12

/ 13-15

/ 16-18

/ 19-21

UKUZI WA KUTANIKO LA KIKRISTO

TAREHE SURA □✔

/ MATENDO ● 1-3

/ ● 4-6

/ ● 7-8

/ ● 9-11

8

/ MATENDO (end.) ● 12-14

/ ● 15-16

/ ● 917-19

/ ● 20-21

/ ● 22-23

/ ● 24-26

/ ● 27-28

BARUA ZA PAULO

TAREHE SURA □✔

/ WAROMA 1-3

/ 4-7

/ 8-11

/ 12-16

/ 1 WAKORINTHO 1-6

/ 7-10

/ 11-14

/ 15-16

/ 2 WAKORINTHO 1-6

/ 7-10

/ 11-13

/ WAGALATIA 1-6

/ WAEFESO 1-6

/ WAFILIPI 1-4

/ WAKOLOSAI 1-4

/ 1 WATHESALONIKE 1-5

/ 2 WATHESALONIKE 1-3

/ 1 TIMOTHEO 1-6

/ 2 TIMOTHEO 1-4

/ TITO/FILEMONI

/ WAEBRANIA 1-6

/ 7-10

/ 11-13

VITABU VYA MITUME NA WANAFUNZI WENGINE

TAREHE SURA □✔

/ YAKOBO 1-5

/ 1 PETRO 1-5

/ 2 PETRO 1-3

/ 1 YOHANA 1-5

/ 2 YOHANA/3 YOHANA/YUDA

/ UFUNUO 1-4

/ 5-9

/ 10-14

/ 15-18

/ 19-22

Kwanza, kata ukifuata mstari wa nukta

Pili, unganisha kurasa hizo mbili na uzikunje

[Picha katika ukurasa wa 14]

Je, unaweza kutenga wakati wa kusoma Biblia kila siku?