Methali 20:1-30

  • Divai ni mdhihaki (1)

  • Mvivu halimi katika majira ya baridi kali (4)

  • Mawazo ya mtu ni kama maji yenye kina (5)

  • Onyo dhidi ya kuapa haraka-haraka (25)

  • Utukufu wa vijana ni nguvu zao (29)

20  Divai ni mdhihaki,+ kileo ni vurugu;+Yeyote anayepotoshwa navyo hana hekima.+   Kutisha* kwa mfalme ni kama mngurumo wa simba;*+Yeyote anayemkasirisha anauhatarisha uhai wake mwenyewe.+   Ni heshima kwa mtu kujiepusha na ugomvi,+Lakini kila mjinga atajitumbukiza humo.+   Mvivu halimi katika majira ya baridi kali,Kwa hiyo atakuwa akiombaomba wakati wa mavuno, wakati hana chochote.*+   Mawazo* yaliyo moyoni mwa mtu ni kama maji yenye kina,Lakini mtu mwenye utambuzi huyateka.   Watu wengi hutangaza upendo wao mshikamanifu,Lakini ni nani anayeweza kumpata mtu mwaminifu?   Mwadilifu anatembea kwa utimilifu wake.+ Watoto* wake wanaokuja baada yake watakuwa na furaha.+   Mfalme anapoketi kwenye kiti cha ufalme ili kuhukumu,+Hupepeta uovu wote kwa macho yake.+   Ni nani anayeweza kusema: “Nimeusafisha moyo wangu;+Mimi ni safi kutokana na dhambi yangu”?+ 10  Vipimo vya udanganyifu na mizani za uwongo*—Vyote viwili humchukiza Yehova.+ 11  Hata mtoto* hujulikana kwa matendo yake,Kama tabia yake ni safi na ya unyoofu.+ 12  Sikio linalosikia na jicho linaloona—Yehova ameviumba vyote viwili.+ 13  Usipende usingizi, la sivyo utakuwa maskini.+ Fungua macho yako, nawe utashiba mkate.+ 14  “Si kizuri, si kizuri!” asema mnunuzi;Kisha anaenda zake na kujigamba.+ 15  Kuna dhahabu, pia kuna marijani* kwa wingi,Lakini midomo ya ujuzi ni kitu chenye thamani.+ 16  Chukua vazi la mtu ikiwa amemwekea dhamana mtu asiyemjua;+Chukua dhamana kutoka kwake ikiwa alimfanyia hivyo mwanamke mgeni.*+ 17  Mkate uliopatikana kwa udanganyifu ni mtamu kwa mtu,Lakini baadaye kinywa chake kitajaa changarawe.+ 18  Kwa mashauriano,* mipango itafanikiwa,*+Na kwa mwelekezo stadi* pigana vita vyako.+ 19  Mchongezi huzurura-zurura akifunua mazungumzo ya siri;+Usishirikiane na mtu anayependa kupiga porojo.* 20  Yeyote anayemtukana baba yake na mama yake,Taa yake itazimwa giza litakapoingia.+ 21  Urithi unaopatikana kwa pupa mwanzoniHautakuwa baraka mwishoni.+ 22  Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+ Mtumaini Yehova,+ naye atakuokoa.+ 23  Vipimo vya udanganyifu vinamchukiza* Yehova,Na mizani za uwongo si nzuri. 24  Hatua za mtu huongozwa na Yehova;+Mwanadamu anawezaje kuelewa njia yake mwenyewe?* 25  Ni mtego kwa mtu kutangaza haraka-haraka, “Ni kitakatifu!”+ Kisha anachunguza baadaye alichoweka nadhiri.+ 26  Mfalme mwenye hekima huwapepeta waovu+Na kuwakanyaga kwa gurudumu la kupuria.+ 27  Pumzi ya mtu ni taa ya Yehova,Inayochunguza kikamili utu wake wa ndani kabisa. 28  Upendo mshikamanifu na uaminifu humlinda mfalme;+Kwa upendo mshikamanifu anadumisha kiti chake cha ufalme.+ 29  Utukufu wa vijana ni nguvu zao,+Na fahari ya wazee ni mvi zao.+ 30  Michubuko na majeraha huondolea mbali* uovu,+Na mapigo husafisha utu wa ndani kabisa wa mtu.

Maelezo ya Chini

Au “Kuogopesha.”
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Au labda, “Atatazama wakati wa mavuno lakini hatapata chochote.”
Au “Makusudio.” Tnn., “Mashauri.”
Tnn., “Wana.”
Au “Mawe mawili ya kupimia yaliyo tofauti na vyombo viwili vya kupimia vilivyo tofauti.”
Au “mvulana.”
Angalia Kamusi.
Au “mgeni.”
Au “mashauri.”
Au “itaimarishwa.”
Au “mwongozo wenye hekima.”
Au “anayeshawishi kwa midomo yake.”
Au “Mawe mawili ya kupimia yaliyo tofauti yanamchukiza.”
Au “njia ya kufuata.”
Au “husugua na kuondoa.”