Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 7:1-40

  • Ushauri kwa waseja na waliofunga ndoa (1-16)

  • Baki katika hali uliyokuwa nayo ulipoitwa (17-24)

  • Waseja na wajane (25-40)

    • Faida za kuwa mseja (32-35)

    • Funga ndoa “katika Bwana tu” (39)

7  Basi kuhusu mambo ambayo mliandika, ni bora mwanamume asimguse* mwanamke;  lakini kwa sababu ya kuenea kwa uasherati,* kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe+ na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.+  Mume na ampe mke wake haki yake, na mke pia na amfanyie vivyo hivyo mume wake.+  Mke hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mume wake anayo; vivyo hivyo, mume hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mke wake anayo.  Msiwe mkinyimana ila kwa makubaliano kwa wakati uliowekwa, ili mtenge wakati kwa ajili ya sala na mje pamoja tena, ili Shetani asiendelee kuwajaribu kwa sababu mnakosa kujizuia.*  Hata hivyo, ninasema hilo ili kuwapa ruhusa, bali si amri.  Lakini ningependa watu wote wawe kama mimi nilivyo. Hata hivyo, kila mmoja ana zawadi yake+ mwenyewe kutoka kwa Mungu, mmoja kwa njia hii, mwingine kwa njia ile.  Sasa ninawaambia waseja na wajane, ni bora wabaki kama mimi nilivyo.+  Lakini ikiwa hawawezi kujizuia,* acheni wafunge ndoa, kwa maana ni bora kufunga ndoa kuliko kuwaka tamaa.+ 10  Kwa watu waliofunga ndoa ninatoa maagizo, si mimi bali ni Bwana, kwamba mke hapaswi kutengana na mume wake.+ 11  Lakini wakitengana, abaki bila kuolewa la sivyo apatane tena na mume wake; na mume hapaswi kumwacha mke wake.+ 12  Lakini kwa wale wengine ninawaambia, ndiyo, mimi, si Bwana:+ Ikiwa ndugu yeyote ana mke asiyeamini na mke huyo anakubali kuishi pamoja naye, basi asimwache; 13  na ikiwa mwanamke ana mume asiyeamini na mume huyo anakubali kuishi pamoja naye, basi asimwache mume wake. 14  Kwa maana mume asiyeamini hutakaswa kuhusiana na mke wake, na mke asiyeamini hutakaswa kuhusiana na huyo ndugu; la sivyo, watoto wenu hawangekuwa safi, lakini sasa wao ni watakatifu. 15  Lakini yule asiyeamini akiamua kuondoka,* acha aondoke; ndugu au dada hajafungwa chini ya hali kama hizo, lakini Mungu amewaita ninyi kwenye amani.+ 16  Wewe mke, unajuaje kama utamwokoa mume wako?+ Au wewe mume, unajuaje kama utamwokoa mke wako? 17  Hata hivyo, kama Yehova* alivyompa kila mmoja fungu, kila mmoja na ajiendeshe kama Mungu alivyomwita.+ Ninatoa agizo hilo katika makutaniko yote. 18  Je, mtu yeyote aliitwa akiwa tayari ametahiriwa?+ Basi asibadili kutahiriwa kwake. Je, mtu yeyote ameitwa akiwa hajatahiriwa? Basi asitahiriwe.+ 19  Kutahiriwa hakuna maana, wala kutotahiriwa hakuna maana;+ lakini kushika amri za Mungu kuna maana.+ 20  Basi katika hali yoyote ambayo kila mmoja aliitwa, acheni abaki hivyo.+ 21  Je, uliitwa ukiwa mtumwa? Usiache hilo likuhangaishe;+ lakini ikiwa unaweza kuwa huru, basi tumia nafasi hiyo. 22  Kwa maana yeyote aliyeitwa katika Bwana akiwa mtumwa ni mtu aliyewekwa huru wa Bwana;+ vivyo hivyo yeyote aliyeitwa akiwa mtu aliye huru ni mtumwa wa Kristo. 23  Mlinunuliwa kwa bei;+ acheni kuwa watumwa wa wanadamu. 24  Akina ndugu, katika hali yoyote ambayo kila mmoja aliitwa, acheni abaki hivyo mbele za Mungu. 25  Sasa kuhusu mabikira,* sina amri kutoka kwa Bwana, lakini ninatoa maoni yangu+ nikiwa mtu aliyeonyeshwa rehema na Bwana kuwa mwaminifu. 26  Kwa hiyo, ninaona ni bora kwa mtu kuendelea kama alivyo kwa sababu ya ugumu uliopo. 27  Je, umefungwa kwa mke? Acha kutafuta kufunguliwa.+ Je, umewekwa huru kutoka kwa mke? Acha kutafuta mke. 28  Lakini hata kama ukifunga ndoa, hutakuwa ukifanya dhambi. Na kama bikira akifunga ndoa, mtu huyo hatakuwa akifanya dhambi. Hata hivyo, wale wanaofanya hivyo watakuwa na dhiki katika mwili wao. Lakini ninajaribu kuwaepusha ninyi. 29  Isitoshe, ninasema hivi akina ndugu, wakati uliobaki umepungua.+ Tangu sasa wale walio na wake na wawe kana kwamba hawana, 30  na wale wanaolia wawe kama wale wasiolia, na wale wanaoshangilia wawe kama wale wasioshangilia, na wale wanaonunua wawe kama wale wasio na kitu, 31  na wale wanaoutumia ulimwengu wawe kama wale wasioutumia kwa ukamili; kwa maana tamasha ya ulimwengu huu inabadilika. 32  Kwa kweli, ninataka msihangaike. Mwanamume ambaye hajaoa huhangaikia mambo ya Bwana, jinsi anavyoweza kupata kibali cha* Bwana. 33  Lakini mwanamume aliyeoa huhangaikia mambo ya ulimwengu,+ jinsi anavyoweza kupata kibali cha* mke wake, 34  naye amegawanyika. Zaidi ya hayo, mwanamke ambaye hajaolewa, na vilevile bikira, huhangaikia mambo ya Bwana,+ ili awe mtakatifu katika mwili wake na pia katika roho yake. Hata hivyo, mwanamke aliyeolewa huhangaikia mambo ya ulimwengu, jinsi anavyoweza kupata kibali cha* mume wake. 35  Lakini ninasema hivyo kwa faida yenu wenyewe, si ili niwazuie,* bali niwachochee kufanya jambo linalofaa na kumtumikia Bwana daima bila kukengeushwa fikira. 36  Lakini kama yeyote akiona kwamba anajiendesha isivyofaa kwa kubaki mseja,* na ikiwa amepita upeo wa ujana, basi inapaswa kuwa hivi: Acheni afanye anavyotaka; hafanyi dhambi. Acheni afunge ndoa.+ 37  Hata hivyo ikiwa yeyote ametulia moyoni mwake, na hana uhitaji wowote, lakini ana mamlaka juu ya nia yake mwenyewe naye amefanya uamuzi moyoni mwake kubaki mseja,* atafanya vema.+ 38  Vivyo hivyo yeyote anayefunga ndoa* anafanya vema, lakini yeyote asiyefunga ndoa atafanya vema zaidi.+ 39  Mke amefungwa kwa muda wote ambao mume wake yuko hai.+ Lakini mume wake akilala usingizi katika kifo, yuko huru kuolewa na yeyote anayemtaka, katika Bwana tu.+ 40  Lakini kwa maoni yangu, mwanamke huyo atakuwa na furaha zaidi akibaki kama alivyo; na ninafikiri mimi pia nina roho ya Mungu.

Maelezo ya Chini

Yaani, asifanye ngono na.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “kujidhibiti; kujiweza.”
Au “kujidhibiti; kujiweza.”
Au “kutengana.”
Au “wale ambao hawajawahi kufunga ndoa.”
Au “kumpendeza.”
Au “kumpendeza.”
Au “kumpendeza.”
Tnn., “nisiwawekee mtego.”
Au “kuelekea ubikira wake.”
Au “kuendelea kuwa bikira.”
Au “anayetoa ubikira wake katika ndoa.”