Matendo ya Mitume 7:1-60

  • Hotuba ya Stefano mbele ya Sanhedrini (1-53)

    • Nyakati za wazee wa ukoo (2-16)

    • Uongozi wa Musa; Waisraeli waabudu sanamu (17-43)

    • Mungu haishi kwenye mahekalu yaliyojengwa na wanadamu (44-50)

  • Stefano apigwa mawe (54-60)

7  Lakini kuhani mkuu akasema: “Je, mambo hayo ni ya kweli?”  Stefano akajibu: “Wanaume, akina ndugu na akina baba, sikilizeni. Mungu wa utukufu alimtokea babu yetu Abrahamu alipokuwa Mesopotamia, kabla hajaanza kuishi Harani,+  naye akamwambia: ‘Ondoka katika nchi yako na kutoka kwa watu wako wa ukoo uje katika nchi nitakayokuonyesha.’+  Ndipo akaondoka katika nchi ya Wakaldayo, akaanza kuishi Harani. Na kutoka hapo, baada ya baba yake kufa,+ Mungu akamwagiza ahamie nchi hii ambayo mnaishi sasa.+  Lakini hakumpa urithi wowote ndani yake, hapana, hata sehemu ya kutosha kukanyaga kwa mguu; bali aliahidi atampa aimiliki yeye na baada yake uzao wake,*+ ingawa bado hakuwa na mtoto.  Isitoshe, Mungu alimwambia kwamba wazao* wake wangekuwa wageni katika nchi ambayo si yao na kwamba watu wa nchi hiyo wangewafanya kuwa watumwa na kuwatesa* kwa miaka 400.+  ‘Nami nitalihukumu taifa hilo ambalo watalitumikia,’+ Mungu akasema, ‘na baada ya mambo hayo watatoka na kunitolea utumishi mtakatifu mahali hapa.’+  “Pia, alimpa agano la tohara,+ naye Abrahamu akawa baba ya Isaka+ na kumtahiri siku ya nane,+ na Isaka akawa baba ya* Yakobo, naye Yakobo akawa baba ya wale vichwa 12 vya familia.*  Na wale vichwa vya familia wakamwonea wivu Yosefu+ na kumuuza Misri.+ Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,+ 10  akamkomboa kutoka katika dhiki zake zote, akampa kibali na hekima mbele ya Farao mfalme wa Misri. Naye Farao akamteua aongoze Misri na nyumba yake yote.+ 11  Lakini kukawa na njaa kali katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ndiyo, dhiki kuu, na mababu zetu hawakuweza kupata chakula chochote.+ 12  Lakini Yakobo akasikia kwamba kulikuwa na chakula* huko Misri, naye akawatuma mababu zetu mara ya kwanza.+ 13  Walipoenda mara ya pili, Yosefu akajitambulisha kwa ndugu zake, naye Farao akaifahamu familia ya Yosefu.+ 14  Basi Yosefu akawatuma watu wamlete Yakobo baba yake na watu wake wote wa ukoo kutoka huko,+ jumla ya watu* 75.+ 15  Ndipo Yakobo akashuka kwenda Misri,+ naye akafa akiwa huko,+ na pia mababu zetu.+ 16  Wakabebwa mpaka Shekemu na kulazwa katika kaburi ambalo Abrahamu alikuwa amenunua kwa kiasi fulani cha fedha kutoka kwa wana wa Hamori huko Shekemu.+ 17  “Wakati ulipokuwa ukikaribia wa kutimizwa kwa ahadi ambayo Mungu alikuwa amempa Abrahamu, watu wakazidi kuongezeka huko Misri, 18  mpaka alipotokea mfalme mwingine huko Misri ambaye hakumjua Yosefu.+ 19  Mfalme huyo akaitendea jamii yetu kwa hila na kuwalazimisha kimakosa akina baba wawaache watoto wao wachanga ili wafe.+ 20  Wakati huo Musa akazaliwa, naye alikuwa mwenye sura nzuri machoni pa Mungu. Akanyonyeshwa* kwa miezi mitatu nyumbani mwa baba yake.+ 21  Lakini alipoachwa,*+ binti ya Farao akamchukua na kumlea kama mwana wake mwenyewe.+ 22  Basi Musa akafundishwa hekima yote ya Wamisri. Kwa kweli, alikuwa mwenye nguvu katika maneno na matendo yake.+ 23  “Sasa alipokuwa na umri wa miaka 40, wazo likaingia moyoni mwake* awatembelee * ndugu zake, wana wa Israeli.+ 24  Alipoona mmoja wao akitendewa isivyo haki, akamtetea na kulipiza kisasi kwa kumuua Mmisri. 25  Alidhani ndugu zake wangeelewa kwamba Mungu alikuwa akiwaokoa kupitia mkono wake, lakini hawakuelewa. 26  Siku iliyofuata aliwakuta wakipigana, akajaribu kuwapatanisha kwa amani, akisema: ‘Wanaume, ninyi ni ndugu. Kwa nini mnatendeana vibaya?’ 27  Lakini yule aliyekuwa akimtendea jirani yake vibaya akamsukuma Musa na kumwambia: ‘Ni nani aliyekuweka uwe mtawala na mwamuzi wetu? 28  Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?’ 29  Aliposikia maneno hayo, Musa akakimbia na kwenda kuishi akiwa mgeni katika nchi ya Midiani, na huko akawa baba ya wana wawili.+ 30  “Baada ya miaka 40, malaika akamtokea kwenye nyika ya Mlima Sinai katika mwali wa moto wa kichaka cha miiba kilichokuwa kikiwaka.+ 31  Musa alipoona jambo hilo, akashangaa sana. Lakini alipokaribia ili kuchunguza, akasikia sauti ya Yehova* ikisema: 32  ‘Mimi ni Mungu wa mababu zako, Mungu wa Abrahamu na wa Isaka na wa Yakobo.’+ Musa akaanza kutetemeka na hakuthubutu kuchunguza zaidi. 33  Yehova* akamwambia, ‘Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni ardhi takatifu. 34  Hakika nimeona jinsi watu wangu walio Misri wanavyokandamizwa, nimesikia kilio chao cha huzuni,+ nami nimeshuka ili kuwaokoa. Basi njoo, nitakutuma huko Misri.’ 35  Huyo Musa ambaye walimkana wakisema: ‘Ni nani aliyekuweka uwe mtawala na mwamuzi?’+ ndiye ambaye Mungu alimtuma+ akiwa mtawala na mkombozi kupitia malaika aliyemtokea katika kichaka cha miiba. 36  Yeye ndiye aliyewaongoza watoke huko,+ akifanya mambo ya ajabu* na ishara huko Misri+ na kwenye Bahari Nyekundu+ na nyikani kwa miaka 40.+ 37  “Huyo ndiye Musa aliyewaambia hivi wana wa Israeli: ‘Mungu atawainulia nabii kama mimi kutoka kati ya ndugu zenu.’+ 38  Huyo ndiye aliyekuwa kati ya kutaniko huko nyikani pamoja na malaika+ aliyezungumza naye+ kwenye Mlima Sinai na mababu zetu, naye akapokea maneno matakatifu yaliyo hai ili atupatie.+ 39  Mababu zetu walikataa kumtii, badala yake wakampuuza+ na katika mioyo yao wakarudi Misri,+ 40  wakimwambia Haruni: ‘Tutengenezee miungu itakayotuongoza. Kwa sababu hatujui lililompata huyu Musa aliyetuongoza kutoka nchi ya Misri.’+ 41  Ndipo wakatengeneza ndama siku hizo na kuiletea sanamu hiyo dhabihu nao wakaanza kufurahia kazi za mikono yao.+ 42  Basi Mungu akageuka na kuwaacha, akawakabidhi watoe utumishi mtakatifu kwa jeshi la mbinguni,+ kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Manabii: ‘Enyi nyumba ya Israeli, je, mimi ndiye mliyetolea matoleo na dhabihu nyikani kwa miaka 40? 43  Bali mlilichukua hema la Moloki+ na nyota ya mungu Refani, sanamu mlizotengeneza ili kuziabudu. Kwa hiyo nitawahamishia ng’ambo ya Babiloni.’+ 44  “Mababu zetu walikuwa na hema la ushahidi nyikani, lililotengenezwa kwa kufuata maagizo ambayo Mungu alimpa Musa kulingana na mfano aliokuwa amemwonyesha.+ 45  Nao mababu zetu wakalimiliki na kulileta pamoja na Yoshua kwenye nchi iliyomilikiwa na mataifa,+ ambayo Mungu aliyafukuza kutoka mbele ya mababu zetu.+ Nalo likakaa huko mpaka siku za Daudi. 46  Alipata kibali machoni pa Mungu naye akaomba pendeleo la kujenga makao kwa ajili ya Mungu wa Yakobo.+ 47  Lakini Sulemani ndiye aliyemjengea nyumba.+ 48  Hata hivyo, Aliye Juu Zaidi haishi katika nyumba zilizojengwa kwa mikono,+ kama vile nabii anavyosema: 49  ‘Mbingu ni kiti changu cha ufalme,+ nayo dunia ni kiti cha miguu yangu.+ Mtanijengea nyumba ya aina gani? Asema Yehova.* Au pako wapi mahali pangu pa kupumzikia? 50  Mkono wangu uliumba vitu hivi vyote, sivyo?’+ 51  “Ninyi watu wagumu na wasiotahiriwa katika mioyo na masikio, sikuzote mnaipinga roho takatifu; kama mababu zenu walivyofanya, ndivyo mnavyofanya pia.+ 52  Ni yupi kati ya manabii ambaye mababu zenu hawakumtesa?+ Ndiyo, waliwaua wale waliotangaza mapema kuhusu kuja kwa yule mwadilifu,+ ambaye ninyi mmemsaliti na kumuua,+ 53  ninyi mliopokea Sheria kupitia malaika+ lakini hamkuishika.” 54  Basi, waliposikia mambo hayo wakawaka hasira* moyoni na kuanza kumsagia meno yao. 55  Lakini Stefano akiwa amejaa roho takatifu, akatazama mbinguni, akaona utukufu wa Mungu na wa Yesu akiwa amesimama kwenye mkono wa kuume wa Mungu,+ 56  naye akasema: “Tazama! Ninaziona mbingu zimefunguka na Mwana wa binadamu+ akiwa amesimama kwenye mkono wa kuume wa Mungu.”+ 57  Ndipo wakapaza sauti ya juu na kuziba masikio kwa mikono yao, wote wakamrukia kwa pamoja. 58  Baada ya kumtupa nje ya jiji, wakaanza kumpiga mawe.+ Wale mashahidi+ wakaweka mavazi yao ya nje miguuni pa kijana aliyeitwa Sauli.+ 59  Walipokuwa wakimpiga mawe Stefano, akaomba hivi: “Bwana Yesu, pokea roho yangu.” 60  Kisha akapiga magoti, akasema kwa sauti kubwa: “Yehova,* usiwahesabie dhambi hii.”+ Na baada ya kusema hayo, akalala usingizi katika kifo.

Maelezo ya Chini

Tnn., “mbegu yake.”
Tnn., “mbegu.”
Au “kuwatendea vibaya.”
Au “wazee wetu wa ukoo.”
Au labda, “akafanya vivyo hivyo na.”
Au “nafaka.”
Au “nafsi.”
Au “Akalelewa.”
Au “alipotupwa.”
Au “akaamua.”
Au “awakague.”
Au “miujiza.”
Au “wakachomwa.”