Kwa Waroma 8:1-39

  • Uzima na uhuru kupitia roho (1-11)

  • Roho ya kuwa wana hutoa ushahidi (12-17)

  • Uumbaji unangojea uhuru wa wana wa Mungu (18-25)

  • ‘Roho hutuombea’ (26, 27)

  • Mungu aliwachagua awali (28-30)

  • Ushindi kupitia upendo wa Mungu (31-39)

8  Kwa hiyo, wale walio katika muungano na Kristo Yesu hawana hukumu ya hatia.  Kwa maana sheria ya roho ambayo hutokeza uzima katika muungano na Kristo Yesu imewaweka ninyi huru+ kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.  Kile ambacho Sheria ilishindwa kufanya+ kwa sababu ilikuwa dhaifu+ kupitia mwili, Mungu alifanya kwa kumtuma Mwana wake mwenyewe+ akiwa katika mfano wa mwili wenye dhambi+ na kuhusu dhambi, akiihukumu dhambi katika mwili,  ili takwa la uadilifu la Sheria litimizwe ndani yetu+ sisi tunaotembea, si kulingana na mwili, bali kulingana na roho.+  Kwa kuwa wale wanaoishi kulingana na mwili hukaza akili zao kwenye mambo ya mwili,+ lakini wale wanaoishi kulingana na roho kwenye mambo ya roho.+  Kwa maana kukaza akili kwenye mwili humaanisha kifo,+ lakini kukaza akili kwenye roho humaanisha uzima na amani;+  kwa sababu kukaza akili kwenye mwili humaanisha uadui na Mungu, kwa kuwa mwili haujitiishi kwa sheria ya Mungu,+ nao kwa kweli hauwezi kujitiisha.  Basi wale wanaopatana na mwili hawawezi kumpendeza Mungu.  Hata hivyo, ninyi hampatani na mwili, bali mnapatana na roho,+ ikiwa kweli roho ya Mungu inakaa ndani yenu. Lakini ikiwa mtu yeyote hana roho ya Kristo, mtu huyo si wake. 10  Lakini ikiwa Kristo yuko katika muungano pamoja nanyi,+ mwili umekufa kwa sababu ya dhambi, bali roho ni uzima kwa sababu ya uadilifu. 11  Basi, ikiwa roho ya yule aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu inakaa ndani yenu, yule aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu+ ataifanya pia miili yenu inayoweza kufa iwe hai+ kupitia roho yake inayokaa ndani yenu. 12  Basi, akina ndugu, sisi tuna wajibu, si kwa mwili ili tuishi kulingana na mwili;+ 13  kwa maana ikiwa mnaishi kulingana na mwili hakika ninyi mtakufa; bali mkiyaua mazoea ya mwili+ kwa roho, mtaishi.+ 14  Kwa maana wote wanaoongozwa na roho ya Mungu, kwa kweli ndio wana wa Mungu.+ 15  Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa inayosababisha woga tena, bali mlipokea roho ya kufanywa kuwa wana, roho ambayo kupitia hiyo tunapaza sauti: “Abba,* Baba!”+ 16  Roho yenyewe hutoa ushahidi pamoja na roho yetu+ kwamba sisi ni watoto wa Mungu.+ 17  Basi, ikiwa sisi ni watoto, sisi pia ni warithi—warithi wa Mungu kwelikweli, lakini warithi pamoja+ na Kristo—mradi tu tunateseka pamoja+ ili pia tutukuzwe pamoja.+ 18  Kwa maana ninaona kwamba mateso ya wakati huu si kitu yakilinganishwa na utukufu utakaofunuliwa ndani yetu.+ 19  Kwa kuwa uumbaji unangojea na kutazamia kwa hamu kufunuliwa kwa wana wa Mungu.+ 20  Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili,+ si kwa mapenzi yake wenyewe bali kupitia yule aliyeutiisha, kwa msingi wa tumaini 21  kwamba uumbaji wenyewe pia utawekwa huru+ kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu. 22  Kwa maana tunajua kwamba uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja mpaka sasa. 23  Si hilo tu, bali sisi wenyewe pia tulio na matunda ya kwanza, yaani, ile roho, ndiyo, sisi wenyewe tunaugua ndani yetu wenyewe,+ huku tukingojea kwa hamu kufanywa kuwa wana,+ kuachiliwa huru kutoka kwenye miili yetu kupitia fidia. 24  Kwa maana tuliokolewa katika tumaini hili; lakini tumaini linaloonekana si tumaini, kwa kuwa mtu anapoona kitu, je, yeye hukitumainia? 25  Lakini tukitumainia+ kile ambacho hatuoni,+ sisi huendelea kukisubiri kwa hamu na uvumilivu.+ 26  Vivyo hivyo, roho pia hutoa msaada kwa ajili ya udhaifu wetu;+ kwa maana tatizo ni kwamba hatujui kile tunachopaswa kusali kuhusu kama tunavyohitaji, lakini roho yenyewe hutuombea kwa kuugua kusikotamkwa.* 27  Lakini yule anayechunguza mioyo+ anajua maana ya roho, kwa sababu inaomba kupatana na Mungu kwa ajili ya watakatifu. 28  Tunajua kwamba Mungu huzifanya kazi zake zote zishirikiane pamoja kwa ajili ya mema ya wale wanaompenda Mungu, wale ambao wameitwa kulingana na kusudi lake;+ 29  kwa sababu wale aliowatambua kwanza, aliwachagua awali pia wafananishwe na mfano wa Mwana wake,+ ili awe mzaliwa wa kwanza+ kati ya ndugu wengi.+ 30  Isitoshe, wale aliowachagua awali+ ndio aliowaita pia;+ na wale aliowaita ndio aliowatangaza kuwa waadilifu pia.+ Mwishowe wale aliowatangaza kuwa waadilifu ndio aliowatukuza pia.+ 31  Basi, tuseme nini kuhusu mambo haya? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani atakayekuwa dhidi yetu?+ 32  Kwa kuwa hakusita kumtoa hata Mwana wake mwenyewe bali alimkabidhi kwa ajili yetu sote,+ je, hatatupatia pia pamoja naye kwa fadhili vitu vingine vyote? 33  Ni nani atakayewashtaki waliochaguliwa wa Mungu?+ Mungu Ndiye anayewatangaza kuwa waadilifu.+ 34  Ni nani atakayewahukumu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa, ndiyo, isitoshe yeye ndiye aliyefufuliwa, aliye kwenye mkono wa kuume wa Mungu+ na ambaye pia hutuombea.+ 35  Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo?+ Je, ni dhiki au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga?+ 36  Kama ilivyoandikwa: “Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.”+ 37  Badala yake, katika mambo haya yote tunatoka tukiwa tumeshinda kabisa+ kupitia yule aliyetupenda. 38  Kwa maana nimesadiki kwamba wala kifo wala uzima wala malaika wala serikali wala mambo yaliyopo sasa wala mambo yatakayokuja wala nguvu+ 39  wala kimo wala kina wala uumbaji mwingine wowote havitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Maelezo ya Chini

Neno la Kiebrania au Kiaramu linalomaanisha “Ee Baba!”
Au “kusikosemwa.”