Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ratiba za Usomaji wa Biblia

Ratiba za Usomaji wa Biblia

Biblia ina hekima bora zaidi ya kutusaidia maishani. Ukiisoma na kutafakari kwa ukawaida na kutumia mambo unayojifunza, ndipo “utakapofanikisha njia yako.” (Yoshua 1:8; Zaburi 1:1-3) Pia, utamjua Mungu na Mwana wake, Yesu, na ujuzi huo unaweza kuongoza kwenye wokovu.​—Yohana 17:3.

Unapaswa kusoma vitabu vya Biblia kwa mpangilio gani? Unaweza kutumia njia kadhaa. Ratiba hii ya kusoma Biblia itakusaidia kusoma vitabu vya Biblia kwa mfuatano au kwa kutegemea habari. Kwa mfano, unaweza kusoma sehemu ulizoteua ili kupata mambo ya kihistoria ya jinsi Mungu alivyoshughulika na Israeli la kale. Unaweza kusoma sehemu nyingine ili kujifunza jinsi kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza lilivyoanza na kukua. Ukisoma sura zilizoonyeshwa kila siku, utakuwa umesoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.

Iwe unatafuta ratiba ya kusoma Biblia kila siku, ratiba ya kusoma Biblia kwa mwaka mmoja, au ratiba ya kusoma Biblia kwa ajili ya wanaoanza kusoma Biblia, ratiba hii itakusaidia. Pakua ratiba hii ya kusoma Biblia inayoweza kuchapishwa, na uanze leo.