Barua ya Yuda 1:1-25

  • Salamu (1, 2)

  • Hukumu ya walimu wa uwongo ni hakika (3-16)

    • Mikaeli abishana na Ibilisi (9)

    • Unabii wa Enoko (14, 15)

  • Endeleeni kujitunza katika upendo wa Mungu (17-23)

  • Kumpa Mungu utukufu (24, 25)

 Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo, pia ndugu ya Yakobo,+ kwa walioitwa+ ambao wanapendwa na Mungu Baba na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo:+  Na mzidi kuwa na rehema, amani, na upendo.  Wapendwa, ingawa nilikusudia kuwaandikia kuhusu wokovu tulio nao kwa pamoja,+ niliona ni lazima niwaandikie ili kuwahimiza mfanye pigano kali kwa ajili ya imani+ ambayo watakatifu walipewa mara moja kwa wakati wote.  Kwa maana watu fulani wameingia kisiri kati yenu ambao Maandiko yalisema tangu zamani kwamba wanastahili hukumu; watu hao hawamwogopi Mungu, wanazitumia fadhili zisizostahiliwa za Mungu wetu kuwa kisingizio cha mwenendo mpotovu*+ wakimkana mmiliki* wetu pekee na Bwana wetu, Yesu Kristo.+  Ingawa mnajua vizuri mambo yote haya, nataka kuwakumbusha kwamba ijapokuwa Yehova* aliwaokoa watu kutoka nchi ya Misri,+ baadaye aliwaangamiza wale waliokosa imani.+  Pia malaika ambao hawakubaki mahali pao pa kwanza bali waliacha makao yao yanayowafaa,+ amewafunga minyororo milele katika giza zito kwa ajili ya hukumu ya ile siku kuu.+  Vivyo hivyo, watu wa Sodoma na Gomora na majiji ya karibu walifanya uasherati* wa kupindukia na kufuatilia tamaa za mwili zilizo kinyume cha maumbile;+ wamewekwa mbele yetu kama onyo kwa sababu walihukumiwa adhabu ya moto wa milele.+  Licha ya hayo, watu hawa pia wanajishughulisha na ndoto, wanauchafua mwili, wanadharau mamlaka, na kuwatukana watukufu.+  Lakini Mikaeli,+ yule malaika mkuu+ alipopingana na Ibilisi na kubishana naye kuhusu mwili wa Musa,+ hakuthubutu kumhukumu kwa kumtukana,+ bali alimwambia: “Yehova* na akukemee.”+ 10  Lakini watu hawa wanayatukana mambo yote ambayo kwa kweli hawayafahamu.+ Na kuhusu mambo yote wanayoyafahamu kiasili kama wanyama wasio na akili,+ wanaendelea kujipotosha wenyewe. 11  Ole wao, kwa sababu wamefuata mwenendo wa Kaini,+ wamejiingiza katika kosa la Balaamu+ ili kupata faida, nao wameangamia katika maneno ya uasi+ ya Kora!+ 12  Hao ndio miamba iliyo chini ya maji katika karamu zenu za kuonyesha upendo+ wanapokula nanyi, wachungaji wanaojilisha bila woga;+ mawingu yasiyo na maji yanayopeperushwa na upepo;+ miti isiyozaa matunda katika majira yake, ambayo imekufa mara mbili* na kung’olewa; 13  mawimbi ya bahari iliyochafuka yenye mapovu ya aibu yao;+ nyota zisizofuata njia hususa, ambazo zitatupwa katika giza zito la milele.+ 14  Enoko,+ wa kizazi cha saba kutoka kwa Adamu, alitabiri pia kuwahusu aliposema: “Tazama! Yehova* alikuja pamoja na maelfu* ya watakatifu wake+ 15  ili kuwahukumu wote,+ na kuwaonyesha wale wasiomwogopa Mungu kwamba wana hatia kwa matendo yao yote ya kutomwogopa Mungu waliyotenda bila kumwogopa Mungu, na kwa maneno yote yenye kushtua ambayo watenda dhambi wasiomwogopa Mungu walisema kumhusu.”+ 16  Watu hawa ni wanung’unikaji,+ walalamikaji kuhusu fungu lao maishani, wakifuata tamaa zao wenyewe+ na kujigamba huku wakiwasifusifu wengine* ili wapate faida.+ 17  Lakini ninyi wapendwa, kumbukeni maneno yaliyosemwa zamani* na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, 18  jinsi walivyokuwa wakiwaambia: “Wakati wa mwisho kutakuwa na wadhihaki, watakaofuata tamaa zao zisizompendeza Mungu.”+ 19  Hao ndio wanaosababisha migawanyiko,+ watu wanaotenda kama wanyama,* wasio na hali ya kiroho.* 20  Lakini ninyi wapendwa, jijengeni juu ya imani yenu takatifu zaidi, na kusali mkiwa na roho takatifu,+ 21  ili mwendelee kujitunza katika upendo wa Mungu,+ mkingojea Bwana wetu Yesu Kristo awaonyeshe rehema ili hatimaye mpate uzima wa milele.+ 22  Pia, endeleeni kuwaonyesha rehema+ wale walio na shaka;+ 23  waokoeni+ kwa kuwanyakua kutoka katika moto. Lakini endeleeni kuwaonyesha wengine rehema, mkifanya hivyo kwa woga, huku mkichukia hata vazi ambalo limetiwa doa kupitia mwili.+ 24  Kwake yeye anayeweza kuwalinda ili msijikwae na kuwasaidia msimame bila dosari+ mbele za utukufu wake* mkiwa na shangwe kubwa, 25  kwa Mungu pekee aliye Mwokozi wetu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu, kuwe na utukufu, ukuu, nguvu, na mamlaka kwa umilele wote uliopita na sasa na mpaka umilele wote. Amina.

Maelezo ya Chini

Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.
Au “mkuu.”
Angalia Kamusi.
Au “imekufa kabisa.”
Au “makumi ya maelfu.”
Au “kuwastaajabia watu.”
Au “yaliyotabiriwa.”
Au “watu wa kimwili.”
Tnn., “roho.”
Au “katika kuwapo kwake kwenye utukufu.”