Zaburi 145:1-21

  • Kumsifu Mungu, Mfalme mkuu

    • ‘Nitatangaza ukuu wa Mungu’ (6)

    • “Yehova ni mwema kwa wote” (9)

    • “Washikamanifu wako watakusifu” (10)

    • Ufalme wa Mungu ni wa milele (13)

    • Mkono wa Mungu huwatosheleza wote (16)

Sifa ya Daudi. א [Aleph] 145  Nitakukweza, Ee Mungu wangu Mfalme,+Nitalisifu jina lako milele na milele.+ ב [Beth]   Nitakusifu mchana kutwa;+Nitalisifu jina lako milele na milele.+ ג [Gimel]   Yehova ni mkuu na anastahili kabisa kusifiwa;+Ukuu wake hauchunguziki.*+ ד [Daleth]   Kizazi baada ya kizazi kitasifu kazi zako;Watasimulia matendo yako yenye nguvu.+ ה [He]   Watasema kuhusu fahari tukufu ya ukuu wako+Nami nitatafakari kazi zako zinazostaajabisha. ו [Waw]   Watasema kuhusu matendo yako yanayoogopesha,*Nami nitautangaza ukuu wako. ז [Zayin]   Watabubujikwa na maneno wanapokumbuka wema wako mwingi,+Nao watapaza sauti kwa shangwe kwa sababu ya uadilifu wako.+ ח [Heth]   Yehova ni mwenye huruma* na rehema,+Si mwepesi wa hasira, naye ana upendo mwingi mshikamanifu.+ ט [Teth]   Yehova ni mwema kwa wote,+Na rehema zake zinaonekana katika kazi zake zote. י [Yod] 10  Kazi zako zote zitakutukuza, Ee Yehova,+Na washikamanifu wako watakusifu.+ כ [Kaph] 11  Watatangaza utukufu wa ufalme wako+Na kusema kuhusu nguvu zako,+ ל [Lamed] 12  Ili kuwajulisha wanadamu matendo yako yenye nguvu+Na fahari yenye utukufu ya ufalme wako.+ מ [Mem] 13  Ufalme wako ni ufalme wa milele,Na mamlaka yako hudumu katika vizazi vyote.+ ס [Samekh] 14  Yehova huwategemeza wote wanaoanguka+Na kuwainua juu wote walioinama chini.+ ע [Ayin] 15  Macho yote yanakutazama yakiwa na tumaini;Unawapa chakula chao katika majira yake.+ פ [Pe] 16  Unaufumbua mkono wakoNa kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.+ צ [Tsade] 17  Yehova ni mwadilifu katika njia zake zote+Na mshikamanifu katika kila jambo analotenda.+ ק [Qoph] 18  Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia,+Wote wanaomwitia yeye katika ukweli.*+ ר [Resh] 19  Hutosheleza tamaa ya wale wanaomwogopa;+Husikia kilio chao cha kuomba msaada, naye huwaokoa.+ ש [Shin] 20  Yehova huwalinda wale wote wanaompenda,+Lakini atawaangamiza waovu wote.+ ת [Taw] 21  Kinywa changu kitatangaza sifa za Yehova;+Kila kitu kilicho hai na kilisifu* jina lake takatifu milele na milele.+

Maelezo ya Chini

Au “hauwezi kueleweka.”
Au “nguvu zako.”
Au “neema.”
Au “kwa unyoofu.”
Tnn., “Miili yote na isifu.”