Barua ya Pili ya Petro 1:1-21

  • Salamu (1)

  • Fanyeni mwito wenu uwe hakika (2-15)

    • Sifa zinazoongezwa kwenye imani (5-9)

  • Neno la kinabii lafanywa hakika zaidi (16-21)

1  Simoni Petro, mtumwa na mtume wa Yesu Kristo, kwa wale ambao wamepata imani, yenye thamani kama yetu* kupitia uadilifu wa Mungu wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo:  Na mwongezewe fadhili zisizostahiliwa na amani kwa ujuzi sahihi+ kumhusu Mungu na kumhusu Yesu Bwana wetu,  kwa maana nguvu zake za kimungu zimetupatia* mambo yote yanayoleta uzima na ujitoaji-kimungu* kupitia ujuzi sahihi kumhusu Yule ambaye alituita+ kwa utukufu wake na wema wa adili.  Kupitia mambo haya ametupatia* ahadi zenye thamani na zilizo bora,+ ili kupitia hizo muwe washiriki katika asili ya kimungu,+ mkiwa mmeponyoka kutoka katika uharibifu wa ulimwengu unaosababishwa na tamaa mbaya.*  Kwa sababu hii, jitahidini kabisa+ kuongeza kwenye imani yenu wema wa adili,+ kwenye wema wenu wa adili ujuzi,+  kwenye ujuzi wenu kujizuia,* kwenye kujizuia*+ kwenu uvumilivu, kwenye uvumilivu wenu ujitoaji-kimungu,*+  kwenye ujitoaji-kimungu* wenu upendo wa kindugu, kwenye upendo wenu wa kindugu upendo.+  Kwa maana mambo hayo yakiwa ndani yenu na kufurika, yatawazuia msiwe wasiotenda ama wasiozaa matunda*+ kuhusiana na ujuzi sahihi kumhusu Bwana wetu Yesu Kristo.  Kwa maana yeyote asiye na mambo hayo ni kipofu, na amefunga macho yake yasione nuru,*+ naye amesahau kutakaswa kwake kutoka kwenye dhambi zake+ za zamani za kale. 10  Kwa hiyo, akina ndugu, jitahidini hata zaidi ili kufanya mwito+ na kuchaguliwa kwenu kuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe, kwa maana mkiendelea kufanya mambo hayo, hamtashindwa kamwe.+ 11  Kwa kweli, hivyo ndivyo mtakavyowezeshwa* kwa wingi kuingia katika Ufalme wa milele+ wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.+ 12  Kwa sababu hiyo sikuzote ninakusudia kuwakumbusha mambo haya, ingawa mnayajua na mko imara katika kweli iliyo ndani yenu. 13  Lakini ninaona inafaa, maadamu niko katika maskani hii,*+ kuwachochea kwa kuwakumbusha,+ 14  kama ninavyojua kwamba maskani yangu itaondolewa hivi karibuni, kama vile pia Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha.+ 15  Sikuzote nitafanya yote ninayoweza ili nitakapoondoka, ninyi wenyewe muweze kuyakumbuka* mambo hayo. 16  Hapana, hatukuwajulisha kuhusu nguvu na kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo kwa kufuata hadithi za uwongo zilizotungwa kwa werevu, badala yake, tulijionea kwa macho fahari yake.+ 17  Kwa maana alipokea kutoka kwa Mungu Baba heshima na utukufu alipoambiwa maneno kama haya* kwa utukufu wenye fahari: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ambaye mimi mwenyewe nimemkubali.”+ 18  Ndiyo, maneno hayo tuliyasikia yakitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika ule mlima mtakatifu. 19  Basi tuna neno la kinabii likiwa limefanywa hakika zaidi, nanyi mnafanya vema kulikazia uangalifu kama vile taa+ inayoangaza mahali penye giza (mpaka siku ipambazuke na nyota ya mchana+ ichomoze) mioyoni mwenu. 20  Kwa kuwa kwanza mnajua kwamba hakuna unabii wa Andiko unaotokana na fasiri yoyote ya kibinafsi. 21  Kwa maana unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu,+ bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa* na roho takatifu.+

Maelezo ya Chini

Au “imani waliyo nayo katika pendeleo lililo sawa na letu.”
Au “zimetupatia bila malipo.”
Angalia Kamusi.
Au “ametupatia bila malipo.”
Au “uchu.”
Au “kujidhibiti; kujiweza.”
Au “kujidhibiti; kujiweza.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “wasiopata matokeo mazuri.”
Au labda, “kipofu, asiyeona mbali.”
Au “mtakavyoongezewa.”
Au “hema hili,” yaani, mwili wake wa duniani.
Au “kuyataja.”
Tnn., “sauti kama hii.”
Tnn., “walivyochukuliwa.”