Isaya 48:1-22

  • Watu wa Israeli wakemewa na kusafishwa (1-11)

  • Yehova atachukua hatua dhidi ya Babiloni (12-16a)

  • Mafundisho ya Mungu ni yenye faida (16b-19)

  • “Tokeni Babiloni!” (20-22)

48  Sikieni hili, enyi watu wa nyumba ya Yakobo,Ninyi mnaojiita kwa jina la Israeli+Na ambao mmetoka katika maji ya Yuda,*Ninyi mnaoapa kwa jina la Yehova+Na mnaomwitia Mungu wa Israeli,Ingawa si katika kweli na uadilifu.+   Kwa maana wanajiita kwa jina la jiji takatifu+Na kutafuta msaada wa Mungu wa Israeli,+Ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.   “Mambo ya kwanza* niliwaambia zamani za kale. Yalitoka kinywani mwangu,Nami niliyatangaza.+ Kwa ghafla nilichukua hatua, nayo yakatokea.+   Kwa sababu nilijua jinsi ulivyo mkaidi—Kwamba shingo yako ni kano ya chuma na paji la uso wako ni shaba+   Nilikuambia zamani za kale. Kabla halijatukia, nilikufanya ulisikie,Hivi kwamba hungeweza kusema, ‘Sanamu yangu ilifanya hivi;Sanamu yangu ya kuchongwa na sanamu yangu ya chuma* ziliamuru jambo hili.’   Umesikia na kuona mambo haya yote. Je, hutayatangaza?+ Kuanzia sasa na kuendelea ninakutangazia mambo mapya,+Siri zilizofichwa ambazo hujazijua.   Ni sasa yanapoumbwa, si zamani za kale,Mambo ambayo kabla ya leo hukuwahi kuyasikia,Hivi kwamba huwezi kusema, ‘Tazama! Tayari ninayajua.’   Hapana, hujasikia,+ hujajua,Na zamani masikio yako hayakuwa yamefunguliwa. Kwa maana ninajua kwamba wewe ni mwenye hila sana,+Nawe umeitwa mkosaji tangu ulipozaliwa.+   Lakini kwa sababu ya jina langu nitaizuia hasira yangu;+Kwa ajili ya sifa yangu mwenyewe nitajizuia,Nami sitakuangamiza.+ 10  Tazama! Nimekusafisha, lakini si kama fedha.+ Nimekujaribu* katika tanuru la kuyeyushia la mateso.+ 11  Nitatenda kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe nitatenda,+Ninawezaje kukubali nitiwe unajisi?+ Simpi yeyote utukufu wangu.* 12  Nisikilize mimi, Ee Yakobo, na Israeli, ambaye nimemwita. Mimi ni yuleyule.+ Mimi ndiye wa kwanza; mimi pia ndiye wa mwisho.+ 13  Mkono wangu mwenyewe uliuweka msingi wa dunia,+Na mkono wangu wa kuume ulizitandaza mbingu.+ Ninapoziita, zinasimama pamoja. 14  Kusanyikeni pamoja, ninyi nyote, msikilize. Ni nani kati yao ameyatangaza mambo haya? Yehova amempenda.+ Atatekeleza mapenzi yake dhidi ya Babiloni,+Na mkono wake utawashambulia Wakaldayo.+ 15  Mimi mwenyewe nimesema, nami nimemwita.+ Nimemleta, na njia yake itafanikiwa.+ 16  Nikaribieni, msikie jambo hili. Tangu mwanzoni kabisa sijasema kwa siri.+ Tangu lilipotokea nilikuwapo.” Na sasa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amenituma, na* roho yake. 17  Yehova, Mkombozi wako, Mtakatifu wa Israeli,+ anasema hivi: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako,Ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe,*+Ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea.+ 18  Laiti ungesikiliza amri zangu!+ Ndipo amani yako ingekuwa kama mto+Na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.+ 19  Uzao wako ungekuwa mwingi* kama mchangaNa wazao wako kama chembe zake.+ Jina lao halingefutiliwa mbali kamwe wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.” 20  Tokeni Babiloni!+ Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Litangazeni kwa vigelegele vya shangwe! Litangazeni!+ Lijulisheni mpaka kwenye miisho ya dunia.+ Semeni: “Yehova amemkomboa mtumishi wake Yakobo.+ 21  Hawakupata kiu alipowaongoza katika maeneo yaliyoharibiwa.+ Alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao;Aliupasua mwamba maji yakabubujika.”+ 22  “Hakuna amani kwa waovu,”+ asema Yehova.

Maelezo ya Chini

Au labda, “mnaotoka Yuda.”
Au “awali.”
Au “sanamu yangu ya kuyeyushwa.”
Au “Nimekuchunguza.” Au labda, “Nimekuchagua.”
Au “Sishiriki utukufu wangu na yeyote.”
Au “pamoja na.”
Au “kwa faida yako.”
Tnn., “Mbegu yako ingekuwa nyingi.”