Zaburi 1:1-6

  • Njia mbili zatofautishwa

    • Kusoma sheria ya Mungu huleta furaha (2)

    • Waadilifu ni kama mti unaozaa matunda kwa wingi (3)

    • Waovu ni kama makapi yanayopeperushwa mbali (4)

1  Mwenye furaha ni mtu ambaye hatembei katika mashauri ya waovuNa hasimami katika njia ya watenda dhambi+Naye haketi katika kiti cha wenye dhihaka.+   Lakini anapendezwa na sheria ya Yehova,+Naye huisoma sheria Yake kwa sauti ya chini* mchana na usiku.+   Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji,Mti unaozaa matunda katika majira yake,Na majani yake hayanyauki. Na kila jambo analofanya litafanikiwa.+   Waovu hawako hivyo;Wao ni kama makapi yanayopeperushwa mbali na upepo.   Ndiyo sababu waovu hawataendelea kusimama katika hukumu;+Wala watenda dhambi hawataendelea kusimama katika kusanyiko la waadilifu.+   Kwa maana Yehova anaijua njia ya waadilifu,+Lakini njia ya waovu itaangamia.+

Maelezo ya Chini

Au “huitafakari sheria Yake.”