Mhubiri 1:1-18

  • Kila kitu ni ubatili (1-11)

    • Dunia inadumu milele (4)

    • Mizunguko ya asili huendelea (5-7)

    • Hakuna jambo jipya chini ya jua (9)

  • Hekima ya wanadamu ni duni (12-18)

    • Kukimbiza upepo (14)

1  Maneno ya mkutanishaji,*+ mwana wa Daudi, mfalme wa Yerusalemu.+   “Ubatili mkubwa kupita wote!” asema mkutanishaji,“Ubatili mkubwa kupita wote! Kila kitu ni ubatili!”+   Mtu hupata faida gani kutokana na kazi yake yote ngumuAnayofanya kwa jasho chini ya jua?+   Kizazi huenda, na kizazi huja,Lakini dunia inadumu* milele.+   Jua huchomoza,* na jua hutua;Kisha hurudi haraka* mahali linapochomozea tena.+   Upepo huelekea kusini na kuzungukazunguka hadi kaskazini;Huendelea kuzungukazunguka; upepo huendelea na mizunguko yake.   Vijito vyote* hutiririka kuingia baharini, lakini bado bahari haijai.+ Mahali vijito vinakotoka, huko ndiko vinakorudi ili vitiririke tena.+   Mambo yote yanachosha sana;Hakuna yeyote anayeweza hata kueleza jambo hilo. Jicho halitosheki kuona;Wala sikio halishibi kusikia.   Jambo ambalo limekuwako, ndilo litakalokuwako,Na jambo ambalo limefanywa, litafanywa tena;Hakuna jambo jipya chini ya jua.+ 10  Je, kuna jambo lolote ambalo mtu anaweza kusema, “Tazama jambo hili—ni jipya”? Tayari lilikuwako tangu zamani za kale;Lilikuwako kabla ya wakati wetu. 11  Hakuna yeyote anayewakumbuka watu wa zamani;Wala hakuna yeyote atakayewakumbuka watakaokuja baadaye;Wala hawatakumbukwa na wale watakaokuja hata baadaye.+ 12  Mimi, mkutanishaji, nimekuwa mfalme wa Israeli huko Yerusalemu.+ 13  Niliazimia moyoni mwangu kujifunza na kuchunguza kwa hekima+ kila jambo ambalo limefanywa chini ya mbingu+—kazi ya kusikitisha ambayo Mungu amewapa wanadamu inayofanya waendelee kushughulika. 14  Niliona kazi zote zilizofanywa chini ya jua,Na, tazama! kila jambo lilikuwa ubatili, kukimbiza upepo.+ 15  Kilichopinda hakiwezi kunyooshwa,Na kisichokuwapo huenda kisiweze kuhesabiwa. 16  Kisha nikasema moyoni mwangu: “Tazama! Nimepata hekima nyingi, kuliko mtu yeyote aliyenitangulia Yerusalemu,+ na moyo wangu ulipata hekima nyingi sana na ujuzi.”+ 17  Nilijitahidi sana ili moyo wangu ujue hekima na kujua wazimu* na kujua ujinga,+ na hilo pia ni kukimbiza upepo. 18  Kwa maana hekima nyingi humfanya mtu azidi kukata tamaa,Hivi kwamba yeyote anayeongeza ujuzi anaongeza maumivu.+

Maelezo ya Chini

Au “yule anayewakusanya watu; mhubiri.”
Tnn., “inasimama.”
Au “huangaza.”
Au “hurudi likihemahema.”
Au “Vijito vyote vya majira ya baridi kali; Vijito vyote vya majira.”
Au “upumbavu wa kupindukia.”