Matendo ya Mitume 15:1-41

  • Bishano kuhusu tohara huko Antiokia (1, 2)

  • Suala lapelekwa Yerusalemu (3-5)

  • Wazee na mitume wafanya mkutano (6-21)

  • Barua kutoka baraza linaloongoza (22-29)

    • Kujiepusha na damu (28, 29)

  • Makutaniko yatiwa moyo kupitia barua (30-35)

  • Paulo na Barnaba waachana (36-41)

15  Sasa watu fulani wakashuka kutoka Yudea na kuanza kuwafundisha akina ndugu: “Msipotahiriwa kulingana na desturi ya Musa,+ hamwezi kuokolewa.”  Baada ya Paulo na Barnaba kutoelewana na kubishana sana na watu hao, wakapanga Paulo na Barnaba na wengine wapande kwenda kwa mitume na wazee huko Yerusalemu+ kuuliza kuhusu jambo* hilo.  Basi, baada ya kusindikizwa umbali fulani na kutaniko, watu hao wakaenda wakapitia Foinike na Samaria, wakisimulia kirefu kuhusu kugeuka kwa watu wa mataifa, nao wakafanya akina ndugu washangilie sana.  Walipofika Yerusalemu, walikaribishwa kwa fadhili na kutaniko na mitume na wazee, nao wakawasimulia mambo mengi ambayo Mungu alifanya kupitia kwao.  Lakini baadhi ya wale wa madhehebu ya Mafarisayo ambao sasa walikuwa waamini wakasimama kutoka kwenye viti vyao na kusema: “Ni lazima watahiriwe na kuwaamuru washike Sheria ya Musa.”+  Basi, mitume na wazee wakakusanyika pamoja ili kulichunguza jambo hilo.  Baada ya kujadiliana sana,* Petro akasimama na kuwaambia: “Wanaume, akina ndugu, mnajua vema kwamba tangu siku za zamani Mungu alinichagua kati yenu ili kupitia kinywa changu watu wa mataifa wasikie neno la habari njema na kuamini.+  Pia, Mungu anayeujua moyo,+ alitoa ushahidi kwa kuwapa roho takatifu,+ kama vile alivyotupatia sisi.  Naye hakutofautisha hata kidogo kati yetu na wao,+ bali aliisafisha mioyo yao kwa imani.+ 10  Basi kwa nini sasa mnamjaribu Mungu kwa kuweka kwenye shingo za wanafunzi nira+ ambayo mababu zetu na sisi wenyewe tulishindwa kuibeba?+ 11  Badala yake, sisi tunaamini kwamba tunaokolewa kupitia fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu+ katika njia ileile wanayookolewa.”+ 12  Ndipo kikundi chote kikanyamaza na kuanza kuwasikiliza Barnaba na Paulo wakisimulia ishara nyingi na mambo ya ajabu* ambayo Mungu alifanya kupitia kwao miongoni mwa mataifa. 13  Walipomaliza kuzungumza, Yakobo akasema: “Wanaume, akina ndugu, nisikilizeni. 14  Simioni+ amesimulia kikamili jinsi Mungu kwa mara ya kwanza alivyoelekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.+ 15  Na maneno ya Manabii yanaunga mkono jambo hilo, kama ilivyoandikwa: 16  ‘Baada ya mambo hayo nitarudi na kuliinua tena hema la* Daudi ambalo limeanguka chini; nitayajenga upya magofu yake na kulirudisha tena, 17  ili watu wanaobaki wamtafute Yehova* kwa bidii, pamoja na watu wa mataifa yote, watu wanaoitwa kwa jina langu, asema Yehova,* anayefanya mambo haya,+ 18  yanayojulikana tangu zamani.’+ 19  Kwa hiyo uamuzi wangu* ni kutowataabisha watu wa mataifa wanaomgeukia Mungu,+ 20  bali kuwaandikia wajiepushe na vitu vilivyochafuliwa na sanamu,+ na uasherati,*+ na vitu vilivyonyongwa,* na damu.+ 21  Kwa maana tangu nyakati za kale kuna watu ambao wamekuwa wakihubiri kumhusu Musa katika kila jiji, kwa sababu yeye husomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila sabato.”+ 22  Ndipo mitume na wazee, pamoja na kutaniko lote wakaamua kuwatuma wanaume waliochaguliwa kutoka miongoni mwao waende Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba; waliwatuma Yuda aliyeitwa Barsaba, na Sila,+ wanaume waliokuwa wakiongoza kati ya akina ndugu. 23  Wakaandika maneno haya na kuyatuma kupitia kwao: “Mitume na wazee, ndugu zenu, kwa ndugu walio huko Antiokia,+ Siria, na Kilikia ambao ni wa kutoka kwa mataifa: Salamu! 24  Kwa kuwa tumesikia kwamba watu fulani walitoka miongoni mwenu na kuwataabisha kwa mambo waliyosema,+ wakijaribu kuwavuruga,* ingawa hatukuwapa maagizo yoyote, 25  tumefikia kauli moja kwamba tuwachague wanaume ili tuwatume kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo, 26  wanaume ambao wametoa uhai wao* kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.+ 27  Kwa hiyo, tunawatuma Yuda na Sila, ili wao pia waeleze mambo hayohayo kwa maneno.+ 28  Kwa maana roho takatifu+ na sisi wenyewe tumeona ni vizuri tusiwaongezee ninyi mzigo zaidi ila mambo haya ya lazima: 29  kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu,+ na damu,+ na vitu vilivyonyongwa,*+ na uasherati.*+ Mkijiepusha kwa uangalifu na mambo haya, mtafanikiwa. Afya njema kwenu!”* 30  Basi, watu hao walipoondoka wakashuka kwenda Antiokia, nao wakakusanya kundi lote pamoja na kuwapa barua hiyo. 31  Baada ya kuisoma, wakashangilia kwa sababu ya kutiwa moyo. 32  Nao Yuda na Sila, kwa sababu walikuwa manabii pia, wakawatia moyo akina ndugu kwa hotuba nyingi na kuwaimarisha.+ 33  Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, ndugu hao wakawaacha warudi kwa amani kwa wale waliokuwa wamewatuma. 34 * —— 35  Lakini Paulo na Barnaba wakakaa Antiokia, wakifundisha na kutangaza habari njema ya neno la Yehova,* wakiwa pamoja na wengine wengi. 36  Baada ya siku kadhaa, Paulo akamwambia Barnaba: “Turudi* tukawatembelee akina ndugu katika kila jiji ambalo tulitangaza neno la Yehova* tuone jinsi wanavyoendelea.”+ 37  Barnaba alikuwa ameazimia kwenda na Yohana, aliyeitwa Marko.+ 38  Lakini Paulo hakutaka waende pamoja naye, kwa sababu alikuwa amewaacha huko Pamfilia na hakuenda pamoja nao kwenye kazi.+ 39  Ndipo wakagombana kwa ukali hivi kwamba wakaachana; naye Barnaba+ akamchukua Marko na kusafiri pamoja naye baharini kwenda Kipro. 40  Paulo akamchagua Sila na kuondoka baada ya akina ndugu kumkabidhi kwenye fadhili zisizostahiliwa za Yehova.*+ 41  Akapitia Siria na Kilikia, akiyaimarisha makutaniko.

Maelezo ya Chini

Au “bishano.”
Au “kubishana sana.”
Au “miujiza.”
Au “ kibanda cha; nyumba ya.”
Au “maoni yangu.”
Au “wanyama waliouawa bila kutolewa damu.”
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “kuzivuruga nafsi zenu.”
Au “nafsi zao.”
Au “Kwaherini.”
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “wanyama waliouawa bila kutolewa damu.”
Au labda, “Kwa vyovyote vile turudi.”