Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUFANYA AMANI KATIKA NYUMBA YENU

Namna ya Kuendeleza Amani Katika Nyumba Yenu

Namna ya Kuendeleza Amani Katika Nyumba Yenu

UNAWAZA kama Biblia inaweza kusaidia kuendeleza amani katika familia? Tafazali, ulinganishe mambo Biblia inasema na mambo yenye watu wenye kufuata ambao waliulizwa waliona kuwa yenye kusaidia. Chunguza ni mambo gani yanaweza kukusaidia uepuke kukosa kuelewana, uendeleze amani, na kufanya urafiki kati yenu ukuwe nguvu na uendelee.

KANUNI ZA BIBLIA ZENYE KUSAIDIA KUENDELEZA AMANI

KILA MUTU AKUWE NA MAWAZO YA MUZURI JUU YA MWENZAKE.

‘Musifanye jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kujisifu, bali [lakini] kwa unyenyekevu wa akili mukiwaona wengine kuwa ni bora [muzuri] kuliko ninyi.’Wafilipi 2:3, 4.

“Tumeona kama ni muzuri kumuona bibi ao bwana yako kuwa wa maana sana kuliko wewe mwenyewe na wengine.”—C. P., mwenye ameolewa kwa miaka 19.

USIKILIZE KWA UANGALIFU NA USIKAZIE MAWAZO YAKO.

‘Uendelee kuwakumbusha . . . wasikuwe wataka-vita, wakuwe wenye usawaziko, wakionyesha upole wote kuelekea watu wote.’Tito 3:1, 2.

“Unaweza kuepuka kukosana kwingi ikiwa haumujibu bibi ao bwana yako kwa sauti ya mabishano. Ni jambo la maana kusikiliza kwa heshima mawazo ya bibi ao bwana yako bila kuyazarau hata kama hauyapendi.”—P. P., mwenye ameolewa kwa miaka 20.

UKUWE NA SIFA YA UVUMILIVU NA UPOLE.

‘Kwa subira kiongozi anashawishiwa, na ulimi wa upole unaweza kuvunja mufupa.’Methali 25:15.

“Kukosa kuelewana kutatokea, lakini matokeo yanategemea roho tunaonyesha. Ni lazima kabisa tukuwe na sifa ya uvumilivu. Wakati tuko na sifa hiyo, tunaona kama mambo yanaendeka muzuri.”—G. A., mwenye ameolewa kwa miaka 27.

SIKUZOTE, UEPUKE MATUSI AO KUPIGANA.

‘Muyaondolee mbali mambo haya yote kutoka kwenu, gazabu, hasira, ubaya, matukano [matusi], na maneno machafu kutoka kinywani mwenu.’Wakolosai 3:8.

“Ninapendezwa na sifa ya kujizuia ya bwana yangu. Kila mara yeye ni mutulivu na hanifokee hata siku moja ao kunitukana.”—B. D., mwenye ameolewa kwa miaka 20.

UKUWE TAYARI KUSAMEHE NA UMALIZE HARAKA KUKOSA KUELEWANA.

‘Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari [kupenda] ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwengine.’Wakolosai 3:13.

“Katika hali ya kukosa kuelewana haiko vyepesi sikuzote kubakia kimya, na unaweza kusema ao kufanya haraka mambo yenye yatamuumiza moyoni bibi ao bwana yako. Katika hali kama hiyo, ni muzuri kusamehe. Haiwezekane kuwa na ndoa ya muzuri bila musamaha.”—A. B., mwenye ameolewa kwa miaka 34.

USIKUWE MUCHOYO.

‘Mukuwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi. . . . Kwa maana kwa kipimo munachopimia, watawapimia ninyi pia.’Luka 6:38.

“Bwana yangu anajua vitu vyenye kunifurahisha, na mara nyingi ananiletea zawadi zenye sikuwazia. Kwa upande wangu, ninajiuliza mara nyingi, ‘Namna gani ninaweza kumufurahisha?’ Matokeo ni kwamba, tumecheka sana, na tunaendelea kufanya hivyo.”—H. K., mwenye ameolewa kwa miaka 44.

USICHOKE KUENDELEZA AMANI KATIKA NYUMBA YENU

Biblia imesaidia mamilioni ya watu katika dunia kuonyesha sifa zenye kuchangia utulivu zaidi katika familia. Watu wa familia wenye waliulizwa na Amuka! ni mifano kidogo tu kati ya hao. * Hata kama watu wengine katika familia zao wanaonekana kuwa hawapendi kufanya bidii yoyote, watu hao wameona kama ni jambo la maana tu kufanya amani, kwa sababu Biblia inatoa ahadi hii: “Wale wanaoshauri amani wanashangilia.”—Methali 12:20.

^ fu. 24 Ili kupata habari zingine juu ya namna ya kufanya maisha ya familia yakuwe yenye furaha, soma sura ya 14 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova, na kinapatikana kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com/swc. Tena, fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA.