Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI FULANI ZA ULIMWENGU

Habari Fulani Juu ya Ulaya

Habari Fulani Juu ya Ulaya

Katika Ulaya, zamani watu walikuwa wanapenda dini sana, lakini leo haiko tena vile. Hata hivyo, habari za hivi karibuni za Ulaya zinapatana na Biblia kwa njia zenye zinaweza kukushangaza.

Faida za Sauti ya Mama

Wachunguzi katika muji wa Milan, inchi ya Italia, walisema kama, watoto wenye kuzaliwa mbele ya kueneza miezi walipata faida nyingi za afya kwa kuwasikilizisha sauti ya mama yao katika hospitali, kupitia chombo chenye kuwekwa kwenye mukono wa mutoto. Ufundi huo unapima kuiga namna mutoto alikuwa anasikia sauti ya mama yake wakati alikuwa katika tumbo la uzazi. Uchunguzi huo unamalizia kwa kusema kama “kusikia sauti ya mama mbele ya wakati kuko na faida kwa watoto wenye kuzaliwa mbele ya kueneza miezi.”

MAMBO BIBLIA INASEMA: ‘Nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu kama mutoto aliyeachishwa kunyonya juu ya mama yake.’—Zaburi 131:2.

Ni Kuchochea Roho ya Kujipenda?

Kulingana na uchunguzi wenye ulifanywa juu ya watoto 565 katika inchi ya Uholanzi (Hollande), watoto wenye kuambiwa na wazazi wao kuwa “wa maana kuliko watoto wengine” na kuwa wanastahili “kutendewa kwa njia ya pekee,” walionekana kuwa wenye kujipenda sana na wenye kujiona wa maana na wenye haki zote kuliko marafiki wao. Mutu mumoja kati ya wale wenye walianzisha uchunguzi huo anasema kama, “watoto wanaamini wakati wazazi wao wanawaambia kama wako wa pekee sana kupita wengine.”

MAMBO BIBLIA INASEMA: ‘Namuambia kila mutu hapo kati yenu asijifikirie mwenyewe zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri; bali [lakini] kufikiri ili akuwe na akili timamu [ya muzuri].’—Waroma 12:3.

Watu Wenye Miaka 100 ao Zaidi Walionyesha Mawazo ya Muzuri

Wachunguzi kwenye masomo ya Juu ya Heidelberg, katika inchi ya Ujerumani, walionyesha kuwa watu wenye miaka 100 ao zaidi wako na tamaa kubwa ya kuishi, hata kama wako na magonjwa na uzaifu wa kimwili. Kati ya watu 4 wenye miaka 100 ao zaidi wenye waliulizwa, watu 3 walionyesha kuwa walipenda sana kuishi na walijikaza kufurahia maisha. Walitimiza mipango yao, walikuwa na mawazo ya muzuri na tumaini, waliona kama maisha yako na kusudi, na walifuata kanuni zao za dini na za mwenendo.

FIKIRIA JAMBO HILI: Kulingana na andiko la Mhubiri 3:11, tamaa yenye tulizaliwa nayo ya kuendelea kuishi inaonyesha nini?