Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuwa Musikilizaji Muzuri

Namna ya Kuwa Musikilizaji Muzuri

TATIZO

Bibi ao bwana yako anasema hivi: “Haunisikilize!” Lakini unasema, ‘nilikuwa ninakusikiliza.’ Hata hivyo, ni wazi kwamba mambo ulisikia ni tofauti na yale alisema. Na kwa hiyo, munaanza kubishana tena.

Unaweza kuepuka mabishano hayo. Kwanza, ni lazima uelewe sababu gani unakosa kusikiliza mambo ya maana katika maneno bibi ao bwana yako alisema, hata ikiwa unawaza ulikuwa unamusikiliza.

SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?

Unakengeushwa fikira, unachoka, ao mambo hayo yote mawili. Watoto wanafanya fujo, televisheni inawaka, na unafikiria tatizo fulani ambalo ulipata kwenye kazi. Sasa bibi ao bwana yako anaanza kuzungumuza na wewe, labda juu ya kupokea wageni magaribi. Unatikisa kichwa kwa kukubali “ndiyo,” lakini ulisikia kweli mambo alisema? Inaonekana haukusikia.

Unawazia​-wazia maneno ambayo bibi ao bwana yako hakusema. Hilo limeitwa “kusoma akili ya mutu” vibaya. Unawazia kwamba kuna habari inayofichwa katika maneno ya bibi ao bwana yako, wakati kwa kweli unawazia​-wazia sana maneno ambayo bibi ao bwana yako hakusema. Kwa mufano, wazia bibi ao bwana yako anasema hivi: “Juma hili umetumika saa nyingi kisha kazi.” Kwa kuwa unawaza anakuambia ulifanya vibaya, unasema hivi: “Haiko kosa langu! Ninapaswa kutumika kisha kazi kwa sababu unatumia feza nyingi.” Bibi ao bwana yako anasema hivi: “Sikusema kwamba ulifanya vibaya!” Kwa kuwa alikuwa tu na nia ya kukuambia muende mahali fulani kujifurahisha mwishoni mwa juma.

Unatafuta kutatua matatizo haraka-haraka. Marcie  * anasema hivi: “Wakati fulani ninapenda tu kueleza namna ninavyojisikia, lakini Mike anapenda kuniambia namna ya kumaliza tatizo hilo. Sipendi kutatua tatizo. Ninapenda tu aelewe namna ninavyojisikia.” Tatizo ni nini? Akili ya Mike inatafuta kutatua tatizo haraka. Na kwa hiyo, atakosa kuelewa mawazo fulani ao mawazo yote katika maneno ambayo Marcie anasema.

Hata iwe tatizo linatokezwa na nini, namna gani unaweza kuwa musikilizaji muzuri?

JAMBO UNALOWEZA KUFANYA

Sikiliza kwa uangalifu kabisa. Bibi ao bwana yako ana jambo fulani la maana la kusema, lakini je, uko tayari kusikiliza? Pengine hauko tayari. Labda akili yako inawaza mambo mengine kwa wakati huo. Ikiwa ni hivyo, usijifanye kuwa unasikiliza. Ikiwezekana, acha kwanza mambo unayofanya na umusikilize bibi ao bwana yako kwa uangalifu, ao unaweza kumuomba angoje kwanza mupaka uwe tayari kumusikiliza.​—Kanuni ya Biblia: Yakobo 1:19.

Mukubaliane kuwa hamutasema ninyi wawili kwa wakati uleule. Ikiwa ni wakati wako wa kusikiliza, ujikaze kabisa ili usimukatize bibi ao bwana yako ao kumupinga. Wewe pia utapata wakati wa kusema. Lakini, sikiliza kwanza.​—Kanuni ya Biblia: Methali 18:13.

Uliza maulizo. Kufanya hivyo kutakusaidia uelewe vizuri mambo bibi ao bwana yako anasema. Marcie, aliyezungumuziwa kwenye ukurasa uliotangulia, anasema hivi: “Ninafurahi wakati Mike ananiuliza maulizo. Kufanya hivyo kunanionyesha kuwa anapendezwa na mambo ninayosema.”

Usisikilize maneno tu, lakini sikiliza habari yote. Tambua yale yanayoelezwa kupitia ishara za mwili, ishara za macho, na sauti. Maneno “hilo ni sawa” yanaweza kumaanisha “hilo si sawa,” ikitegemea namna yanavyosemwa. Maneno “haujitolee ili kunisaidia” yanaweza kumaanisha “sijisikie kuwa mutu wa maana kwako.” Jaribu kuelewa habari ambayo anataka kusema kabisa, hata ikiwa hakuisema waziwazi. Usipofanya hivyo, munaweza kujikuta mukiwa wenye kubishana juu ya maneno ambayo bibi ao bwana yako alisema kuliko kukazia akili yale aliyokuwa akimaanisha.

Endelea kusikiliza. Endelea kusikiliza na usiondoke, hata ikiwa haupendezwi na mambo unayosikiliza. Kwa mufano, unaweza kufanya nini ikiwa bibi ao bwana yako anakuchambua? Gregory, ambaye amefunga ndoa kwa miaka zaidi ya 60, anashauri hivi: “Endelea kusikiliza. Pendezwa kabisa na mambo ambayo bibi ao bwana yako anasema. Kufanya hivyo kunaomba ukomavu, lakini kutakuletea faida kabisa.”​—Kanuni ya Biblia: Methali 18:15.

Pendezwa kabisa na bibi ao bwana yako. Kusikiliza kwa uangalifu, si ufundi tu lakini ni tendo linaloonyesha upendo. Wakati unapendezwa kabisa na mambo bibi ao bwana yako anasema, utamusikiliza kwa vyepesi na bila kukazwa. Ukifanya hivyo utakuwa ukifuata shauri la Biblia ambalo linasema hivi: “Pasiwe na mtu anayetafuta faida yake mwenyewe tu bali faida ya mwenzake.”​—Wafilipi 2:4, Biblia Habari Njema.

^ Majina yamebadilishwa katika habari hii.