Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUFANYA AMANI KATIKA NYUMBA YENU

Namna ya Kumaliza Kukosana Katika Nyumba

Namna ya Kumaliza Kukosana Katika Nyumba

UTAFANYA nini ikiwa inaonekana kuwa munakosana kila mara katika nyumba yenu? Pengine mumeanza kukosana sana na kila mara. Labda haujue hata namna kukosa kuelewana kulianza. Lakini munapendana, na hamutaki kuumizana moyoni.

Ni jambo la maana kukumbuka kama kukosa kuelewana katika mawazo hakumaanishe kabisa kuwa maisha ya nyumba yenu yanaendelea kuharibika. Haiko kukosa kuelewana ndiko kutaharibisha nyumba yenu, lakini ni namna munatenda wakati hamuelewane ndiyo itaamua ikiwa nyumba yenu itakuwa mahali pa utulivu ao hapana. Chunguza mambo fulani yenye yanaweza kukusaidia umalize kukosana.

1. UACHE KULIPIZA KISASI.

Ili kukuwe mabishano, inaomba kukuwe watu wawili, lakini wakati mutu mumoja anaanza kusikiliza kuliko kusema, mabishano makali yanaweza kuanza kutulia. Kwa hiyo, upinge kishawishi cha kulipiza kisasi wakati unakasirishwa. Ulinde heshima yako kwa kujizuia wewe mwenyewe. Ukumbuke kama, amani katika nyumba yako ni ya lazima sana kuliko kuwina katika mabishano.

‘Pasipo na kuni moto unazimika, na pasipo na muchongezi ugomvi unatulia.’Methali 26:20.

2. UITIKE NAMNA WATU WA FAMILIA YAKO WANAJISIKIA MOYONI.

Kusikiliza mutu mwengine kwa uangalifu na kwa huruma bila kumukatiza ao kumuhukumu kunaweza kusaidia sana ili kumaliza hasira na kurudisha amani. Kuliko kuwazia kuwa mutu mwengine iko na nia mubaya, ukubali namna anajisikia moyoni. Kama alifanya jambo fulani kwa sababu ya kutokamilika, usione kuwa alilifanya kwa makusudi. Maneno ya mubaya yanaweza kutokea kwa sababu ya kukosa kufikiri ao moyo wenye kuumia, haiko kwa sababu ya kukusudia ao kulipiza kisasi.

‘Mujivike upendo mwororo wenye huruma, fazili, unyenyekevu wa akili, upole, na ustahimilivu.’Wakolosai 3:12.

3. UJIPATIE WAKATI WA KUTULIA.

Kama unakasirika haraka, ni jambo la hekima kuomba musamaha kwa heshima na kuondoka kwa wakati fulani ili utulie. Pengine unaweza kuenda katika chumba kingine ao kuenda kujitembeza kidogo mupaka utulie. Kutenda hivyo hakumaanishe kama unaepuka kufanya mambo pamoja na wengine ao kama unakataa kuzungumuza na wengine. Lakini, pengine huo ni wakati muzuri wa kusali kwa Mungu ili akusaidie ukuwe na uvumilivu, utambuzi na uelewaji.

“Kabla mabishano hayajalipuka, jiondokee.”Methali 17:14.

4. UCHUNGUZE KWA UANGALIFU MAMBO YA KUSEMA NA NAMNA YA KUYASEMA.

Kujikaza sana ili kupata jibu lenye litaumiza mutu mwengine hakuwezi kumaliza magumu. Lakini, ujikaze kufanya jambo lenye litatuliza moyo wenye kuumia wa mutu mwenye unapenda. Na kuliko kumuambia namna anapaswa kujisikia, kwa unyenyekevu umuombe akufasirie mambo waziwazi na umushukuru kwa musaada ao mafasirio yoyote yenye anakutolea.

‘Kuna mutu anayesema bila kufikiri kama kwa upanga unaochoma, lakini ulimi wa mwenye hekima unaponya.’Methali 12:18.

5. UZUNGUMUZE KWA SAUTI YA CHINI NA YA KUTAFUTA MAPATANO.

Kukosa uvumilivu kwa mutu mumoja wa familia kunaweza kupandisha haraka hasira ya mutu mwengine. Hata kama unajisikia kuwa mwenye kukwazika sana, uepuke kutumia maneno ya kuchekelea mwengine ao matusi ao kupandisha sauti yako. Uepuke maneno ya kuumiza kama vile, “Haunihangaikiake” ao “Haunisikiake.” Kuliko kutumia maneno hayo, uambie bibi ao bwana yako kwa njia ya utulivu namna matendo yake yamekuumiza moyoni (“Ninakwazika wakati una. . .”). Kusukuma mutu, kumupiga kwa kutumia mukono ao muguu, ao njia ingine yoyote ya jeuri haikubalike hata kidogo. Ni vile pia juu ya kutumia matusi, maneno ya kushushiana heshima, ao maneno ya kuogopesha.

‘Uchungu wote wenye uovu na hasira na gazabu na kupiga kelele na matukano na viondolewe mbali kutoka kwenu pamoja na ubaya wote.’Waefeso 4:31.

6. UKUWE TAYARI KUOMBA MUSAMAHA, NA UELEZE JAMBO LENYE UTAFANYA ILI HALI IKUWE MUZURI.

Usiruhusu kujisikia mubaya moyoni kukufanye usahau kusudi lako kubwa, ni kusema, kufanya amani. Ukumbuke kama ikiwa unabishana na mutu fulani, ninyi wawili munapoteza. Ikiwa munafanya amani, ninyi wawili munapata ushindi. Kwa hiyo, uitike kuwa wewe pia ulichangia katika mabishano. Hata kama uko hakika kuwa hauna kosa, unaweza tu kuomba musamaha kwa sababu ulikasirika, ulitenda namna ulitenda, ao kwa sababu bila kupenda ulichangia kutokea kwa mabishano hayo. Kuwa na amani na wengine ni kwa maana sana kuliko kiburi na ushindi. Na kama mutu fulani anakuomba musamaha, ukuwe tayari kumusamehe.

‘Enda ujinyenyekeze na kumusihi sana mwenzako.’ Methali 6:3.

Wakati mabishano yanaisha, unaweza kufanya nini ili kukuwe amani katika nyumba? Habari yenye kufuata itazungumuzia jambo hilo.