Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Nyangumi Wako Hapa!

Nyangumi Wako Hapa!

Kila mwaka, kuanzia Mwezi wa 7, nyangumi wenye kufaa wa kike wa kusini (Eubalaena australis) wanafika kwenye sehemu ya kusini ya pembeni ya bahari ya jimbo la Santa Catarina, katika inchi ya Brazili. Wanatokea mbali sana kwenye mamia ya kilometre, upande wa antaktiki, ili kuja kuzaa na kunyonyesha watoto wao katika maji yasiyokuwa marefu. Kwa miezi mingi, wakaaji na watembeaji kwenye sehemu za muchanga pembeni ya bahari ao kwenye miamba wanafurahi sana wakati wanaangalia nyangumi, mama na watoto, wakipumuzika ao kucheza-cheza katika maji!

Viumbe Vikubwa Vyenye Kufanya Michezo ya Kushangaza

Nyangumi wa kike anaweza kuwa na urefu wa metre 16, karibu ukubwa wa bisi kubwa ndefu, na uzito wa kilo 80000! Mara nyingi mwili wake munene sana ni mweusi, nyakati fulani ni wenye kuwa na madoadoa meupe kwenye tumbo. Kichwa chake ni kikubwa sana, kinakamata sehemu 1 juu ya 4 ya mwili wake. Kinywa chake ni kirefu na kiko kama upinde (arc). Nyangumi huyo hana pezi la mugongo (kiungo cha kumusaidia kuogelea) kama vile aina zingine. Ili kuogelea katika maji, nyangumi huyo anatikisa juu chini mukia wake mukubwa wenye kuwa kama V, kuliko kuutikisa kushoto kuume kama vile samaki wanafanya. Ili kubadilisha njia, anatikisa viungo vyake vya kuogelea. Jambo hilo linafanana na vile ndege (avion) inaongozwa.

Jambo la kushangaza ni kwamba, hata kama nyangumi hao wako wakubwa sana, ni wepesi na wanafanya michezo ya kushangaza. Unaweza kuona nyangumi hao wanaacha mikia yao juu ya maji kwa muda murefu wakati wako wanaogelea; wanaonyesha mikia yao na kupiga maji kwa nguvu sana; na wanajitupa katika hewa na kisha kuanguka kwa kujigeuza-geuza katika maji kwa kishindo kikubwa chenye mutu anaweza kuona kwa mbali sana.

Mambo ya Pekee Juu ya Mwili Wake

Kwenye kichwa na kuzunguka kichwa, kuko sagamba nyingi za rangi ya mweupe na kimanjano (jaune), ni kusema, sehemu zenye kuwa nguvu-nguvu za ngozi yake zenye kufunikwa na viumbe vidogo-vidogo vya baharini vyenye kuitwa chawa za nyangumi. Katarina Groch, mwenye kusimamia mupango wa kuangalia mambo ya nyangumi katika inchi ya Brazili, anasema hivi: “Kila sagamba ni la pekee, kama vile alama za vidole za kila mutu ni za pekee. Jambo hilo linasaidia kutambulisha kila nyangumi mwenye kufaa. Tunakamata picha za sagamba za nyangumi wakati wanakuja kandokando ya bahari na tunazichunga nafasi fulani.”

Wanasayansi wa biolojia wanasema kama ni vigumu kujua miaka ya nyangumi wenye kufaa wakati wanakufa, kwa sababu hawana meno. Wanakadiria kuwa nyangumi anaweza kuishi miaka 65 hivi. *

Namna ya Kula Yenye Kushangaza

Nyangumi wenye kufaa wanakula viumbe vidogo-vidogo vya baharini. Kwenye kila upande wa mufupa wa juu wenye kubeba meno, kuko utaratibu wa kuchuja wenye kufanyizwa na mamia ya mifupa yenye kufunikwa na manyoya ya muzuri. Wakati wanaogelea, kinywa chao chenye kuwa wazi kinaruhusu maji yachujwe kupitia mifupa ya nyangumi. Viumbe vidogo-vidogo vya baharini vinakamatwa kupitia manyoya yenye kufunika mifupa hiyo. Kupitia njia hiyo, kila nyangumi anaweza kula kilo 2000 za viumbe vidogo-vidogo vya baharini kwa siku.

Nyangumi hao wanapitisha kipindi cha joto (Mwezi wa 1 na wa 2) wakikula katika Bahari ya Antaktiki, jambo hilo linawasaidia kutengeneza kiasi kingi cha mafuta katika mwili wao. Mafuta hayo mengi yanawasaidia kupata joto wakati wanakuwa katika maji ya baridi na yanatumika kama chakula wakati wanahama.

Jina Lao Lilitoka Wapi?

Tangu kati ya mwaka wa 1701 na 1800 na kuendelea, wavuaji wa nyangumi walivua sana nyangumi hao katika Kizio cha Kusini. Waliwaona kuwa nyangumi “wenye kufaa” wa kuwinda. Sababu gani? Kwa sababu nyangumi hao wanaogelea polepole, walikuwa wanakamatwa kwa vyepesi, hata wavuaji wenye walikuwa na mikuki tu ambao walitumia mitumbwi ya mbao isiyokuwa migumu, waliweza kuwakamata. Tena, tofauti na nyangumi wengine, nyangumi wenye kufaa wanabakia juu ya maji wakati wanauawa kwa sababu wako na mafuta mengi sana. Ndiyo maana wavuaji wa nyangumi wangeweza kuwakokota kwa vyepesi kwenye inchi kavu.

Zaidi ya hilo, mafuta ya nyangumi na mifupa yenye kuwa katika kinywa chake vilikuwa vitu vya maana sana wakati huo. Mafuta hayo yalitumiwa katika taa za barabara na pia ili kuregeza vyuma. Mifupa hiyo ilitumiwa ili kufanya vitu mbalimbali kama vile nguo za ndani za wanawake (gaine), fimbo za kuongoza farasi, na vyuma vyenye kutegemeza miavuli. Kwa kweli, mifupa hiyo ya nyangumi mumoja tu ingeweza kulipia garama za safari nzima!

Kati ya mwaka wa 1901 na 2000, nyangumi wenye kufaa walipunguka kwa sababu ya kuvuliwa sana, na kwa hiyo biashara ya nyangumi haikukuwa inaleta faida tena. Katika inchi ya Brazili, kituo cha mwisho cha kuwinda nyangumi kilifungwa katika mwaka wa 1973. Hata kama aina fulani za nyangumi zililindwa, zingine zingali katika hatari ya kupotea.

Nyangumi wenye kufaa ni mufano muzuri sana wenye kuonyesha kama uzima duniani uko wa ajabu sana na wa aina nyingi sana. Nyangumi huyo anaonyesha hekima na nguvu yenye kushangaza ya ule mwenye alimuumba, ni kusema, Muumbaji Mukubwa, Yehova Mungu.—Zaburi 148:7.

^ fu. 8 Maji mengine kwenye wanazalia yanapatikana karibu na sehemu za pembeni ya bahari za Argentina, Australia, Afrika Kusini, Uruguai, na Visiwa vya Auckland.

Wanasayansi wanaonyesha kama kuko aina mbalimbali za nyangumi wenye kufaa. Kwa mufano, zaidi ya Eubalaena australis katika Kizio cha Kusini, kuko pia Eubalaena glacialis na Eubalaena japonica katika Kizio cha Kaskazini.