Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Nafsi

Nafsi

Dini zinatoa mawazo mbalimbali yenye kupingana juu ya nafsi na kile kinapata nafsi wakati tunakufa. Lakini, Biblia inatoa maelezo ya waziwazi.

Nafsi haikufake?

MAMBO WATU WANASEMA

Watu wengi wanaamini kama nafsi haikufake. Watu fulani wanaamini kama nafsi inaendelea kuzaliwa, kwa kutokea tena na tena katika mwili mupya kisha kufa kwa mwili wa kwanza. Wengine wanaamini kama mwishowe nafsi inaenda katika makao fulani, kama vile mbinguni ao katika moto wa mateso.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia haiseme kama nafsi haikufake. Kwa kweli, inaonyesha mara nyingi kama nafsi inakufaka. Nabii Ezekieli, mwenye Mungu alitumia kuandika sehemu fulani ya Biblia, alisema kama nafsi inaweza kufa. Wakati mwengine, Biblia inatumia maneno ‘nafsi iliyokufa’ ili kumaanisha maiti. (Mambo ya Walawi 21:11) Ni wazi kama Biblia haifundishe kuwa nafsi haikufake.

‘Nafsi inayotenda zambi—hiyo yenyewe itakufa.’Ezekieli 18:20.

Nafsi iko tofauti na mwili?

MAMBO WATU WANASEMA

Nafsi inafanya mwili utumike wakati mutu iko muzima, lakini inaenda wakati anakufa.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia inazungumuzia mama mwenye kuzaa “nafsi,” ni kusema, watu wazima, wenye kupumua. (Mwanzo 46:18) Kwa kweli, neno la Kiebrania lenye kutumiwa katika Biblia kwa ajili ya “nafsi” linaweza kutafsiriwa “enye kupumua.” Wakati fulani neno hilo linatumiwa hata ili kumaanisha wanyama. Tena, Biblia inaonyesha kama nafsi iko na lazima ya chakula. (Kumbukumbu la Torati 12:20) Kama nafsi ingekuwa kitu chenye kuwa tofauti na mwili, ingekuwa na lazima ya kupumua ao kula? Katika Biblia, mara nyingi neno nafsi linamaanisha mutu muzima mwenye kuishi, ni kusema, mwili, namna mutu anajisikia, na sifa zake.

‘Akamuzalia . . . nafsi 16.’Mwanzo 46:18.

Nafsi inapatwa na nini wakati mutu anakufa?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Kwa kweli, “hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi.” (Mhubiri 9:10) Maandiko yanatuambia kama wakati mutu fulani anakufa, ‘anarudia kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake yanapotea.’ (Zaburi 146:4) Nafsi yenye kufa iko katika hali ya kutotenda, na ndiyo sababu, mara nyingi kwa njia ya mufano, Maandiko yanasema kama mutu mwenye kufa “analala usingizi.”—Mathayo 9:24.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Wakati unafiwa na watu wenye unapenda, unataka kupata majibu ya maulizo kama vile: Wako wapi? Wako katika hali gani? Wako wanateseka? Kwa sababu Biblia inatuhakikishia kama watu waliokufa hawajue jambo lolote, tunaweza kutulizwa kwa kujua kama watu wenye tunapenda ambao wamekufa hawateseke. Tena, tunaweza kutulizwa kwa kujua kama, Yehova anaahidi kwamba wakati unaokuja, atafufua nafsi zilizokufa zenye hazijue jambo lolote.—Isaya 26:19.

Wafu, hawajue lolote kamwe.’Mhubiri 9:5.