Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 3

Namna ya Kumaliza Matatizo

Namna ya Kumaliza Matatizo

‘Muwe na upendo mukubwa ninyi kwa ninyi, kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.’​—1 Petro 4:8

Wakati munaanza kuishi pamoja, matatizo mbalimbali yatatokea. Matatizo hayo yanaweza kutokea kwa sababu kila mutu ana namna yake ya kufikiri, namna yake ya kujisikia, na namna yake ya kushugulika na mambo katika maisha. Pia, matatizo yanaweza kutokea kwa sababu zingine na kwa sababu ya mambo yasiyotazamiwa.

Mutu anaweza kutafuta kukimbia matatizo, lakini Biblia inatushauria tupambane na matatizo. (Mathayo 5:23, 24) Utamaliza matatizo yako kwa njia inayofaa ikiwa unatumikisha kanuni za Biblia.

1 MUZUNGUMUZIE TATIZO

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: “Kuna . . . wakati wa kusema.” (Mhubiri 3:1, 7) Mupitishe wakati pamoja ili kuzungumuzia tatizo fulani. Acha bibi ao bwana yako ajue namna unajisikia na mawazo yako kuhusu tatizo hilo. “Sema kweli” na bibi ao bwana yako sikuzote. (Waefeso 4:25) Hata wakati unakasirika sana, ujikaze usipigane. Jibu la upole linaweza kufanya mazungumuzo yasitokeze ugomvi.​—Metali 15:4; 26:20.

Hata kama haukubaliane na bibi ao bwana yako, endelea kumuheshimia na kumupenda. (Wakolosai 4:6) Mujikaze kumaliza tatizo haraka kadiri inawezekana, na musianze kunyamazana.​—Waefeso 4:26.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Mupange wakati unaofaa ili kuzungumuzia tatizo lenu

  • Ikiwa ni wakati wa mwenzako kuzungumuza, usimukatize. Wakati wako wa kuzungumuza utafika

2 UMUSIKILIZE MWENZAKO NA UMUELEWE

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Muwe na upendo mwororo kwa mutu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima muwe wa kwanza.’ (Waroma 12:10) Ni jambo la lazima sana kumusikiliza mwenzako. Jaribu kuelewa mawazo ya bibi ao bwana yako ukiwa mwenye “hisia-mwenzi . . . na unyenyekevu.” (1 Petro 3:8; Yakobo 1:19) Usijifanye tu kama unasikiliza. Ikiwezekana, acha mambo yote ambayo unafanya, na hivyo umusikilize bibi ao bwana yako kwa uangalifu zaidi, ao umuombe ikiwa munaweza kuzungumuzia jambo hilo kisha. Ikiwa unamuona bibi ao bwana yako kuwa rafiki yako, wala si adui yako, hautakuwa ‘haraka kuuzika.’​—Mhubiri 7:9.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Endelea kumusikiliza bibi ao bwana yako kwa uangalifu, hata kama mambo anayosema hayakufurahishe

  • Sikiliza na utafute kujua kile kinachomuchochea aseme maneno fulani. Ona ishara zake za mwili na sauti yake

3 MUTENDE KULINGANA NA MAAMUZI YENU

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Kwa kila kazi ngumu kunatokea faida, lakini neno la midomo tu linaelekea kuleta uhitaji.’ (Methali 14:23) Kukubaliana katika jambo fulani hakutoshe. Ni vizuri kutenda kulingana na maamuzi yenu. Hilo linaweza kuomba kujikaza sana, lakini faida ni nyingi. (Methali 10:4) Ikiwa munafanya kazi kwa umoja ‘mutapata zawadi nzuri’ kwa ajili ya kazi yenu ngumu.​—Mhubiri 4:9.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Muamue mambo ambayo kila mumoja atafanya ili kumaliza tatizo lenu

  • Mara kwa mara, muangalie kama mambo yanaendelea namna gani