Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA MAKUMI MBILI NA MOJA

Alishinda Woga na Mashaka

Alishinda Woga na Mashaka

1-3. Petro alijionea nini siku iliyopita na pia usiku muzima?

PETRO anajikaza kupiga kasia na anaangalia-angalia ikiwa kuna alama yoyote inayoonyesha kwamba usiku unataka kucha. Mishipa yake ya mugongo na ya mabega inauma kwa sababu ya kupiga kasia kwa saa nyingi. Upepo umeichafua Bahari ya Galilaya na unamupiga usoni. Mawimbi yanaipiga-piga mashua yao ya kuvua samaki na maji hayo baridi yanamumwangikia na kumuloanisha. Lakini bado anaendelea kupiga kasia.

2 Petro na wenzake walimuacha Yesu inchi kavu. Siku iliyopita, waliona namna Yesu alivyolisha maelfu ya watu waliokuwa na njaa kwa mikate michache na samaki wachache tu. Kwa hiyo, watu walitaka kumufanya Yesu awe mufalme, lakini Yesu alikataa kujiingiza katika mambo ya politike. Hataki pia kuwaona wafuasi wake wanajiingiza katika mambo ya politike. Ili kuepuka watu hao, Yesu anawaagiza wanafunzi wake wachukue mashua na waende upande mwengine wa bahari; wakati huo yeye anaenda mulimani peke yake ili kusali.—Mk. 6:35-45; soma Yohana 6:14-17.

3 Wanafunzi walipoondoka mwezi ulikuwa bado ni wenye kuonekana vizuri angani, lakini sasa mwezi unaelekea polepole kutua upande wa mangaribi. Hata hivyo, wamekwisha kufanya tu kilometre chache. Hawazungumuze tena kwa sababu ya muchoko na makelele ya upepo mukali unaovuma pamoja na mawimbi. Lakini inaonekana Petro ni mwenye kufikiria mambo fulani.

Petro amepitisha zaidi ya miaka miwili pamoja na Yesu na amejifunza mambo mengi, lakini bado ana mengine mengi ya kujifunza

4. Sababu gani Petro ni mufano muzuri wa kuiga?

4 Ni mambo gani hayo ambayo Petro anafikiria? Amepitisha zaidi ya miaka miwili pamoja na Yesu wa Nazareti. Amejifunza mambo mengi, lakini bado ana mengine mengi ya kujifunza. Iko tayari kujifunza mengi zaidi, kwa mufano namna ya kushinda uzaifu wake, kama vile mashaka na woga. Mambo yote ambayo Petro alikutana nayo yanamufanya awe mufano muzuri wa kuiga. Acheni tuone mambo yaliyomupata.

‘Tumemupata Masiya’!

5, 6. Petro alikuwa na maisha ya namna gani?

5 Petro hawezi hata kidogo kusahau ile siku ambayo alikutana na Yesu wa Nazareti. Siku hiyo, ndugu yake Andrea alimupasha habari hii yenye kushangaza: ‘Tumemupata Masiya.’ Petro aliposikia maneno hayo, maisha yake yalianza kubadilika kabisa.​—Yoh. 1:41.

6 Petro alikuwa akiishi huko Kapernaumu, muji ulio kandokando ya ziwa lenye maji baridi linaloitwa Bahari ya Galilaya. Yeye na Andrea walitumika pamoja na Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, katika kazi ya kuvua samaki. Petro hakuishi yeye mwenyewe, alikuwa na bibi yake, mama yake mukwe, na ndugu yake Andrea. Ili kushugulikia familia kama hiyo inaomba nguvu na ufundi ikiwa ni kwa kuvua tu samaki. Wazia wanaume hao wakitupa nyavu zao usiku kucha na kuzikokota katika mashua zao mbili ili kuvua samaki yoyote ile inayoweza kupatikana katika ziwa. Wazia pia namna wanavyotumika muchana muzima ili kuchagua na kuuzisha samaki wao, kutengeneza nyavu zao na kuzisafisha.

7. Petro alisikia habari gani juu ya Yesu, na sababu gani ilikuwa habari yenye kufurahisha sana?

7 Biblia inatueleza kwamba Andrea alikuwa mwanafunzi wa Yohana Mubatizaji. Bila shaka, Petro alimusikiliza kaka yake kwa uangalifu kabisa wakati alimuzungumuzia ujumbe ambao Yohana alikuwa anatangaza. Siku moja, Andrea alimuona Yohana akimuelekezea Yesu mukono na kusema: “Ona, Mwana​-Kondoo wa Mungu!” Na mara moja Andrea akawa mufuasi wa Yesu na kwa hamu sana anamuambia Petro habari hii yenye kufurahisha: Masiya amefika! (Yoh. 1:35-40) Miaka 4 000 hivi mbele ya hapo, kisha uasi kutokea huko Edeni, Yehova Mungu aliahidi kwamba mutu wa pekee atakuja kuwapatia wanadamu tumaini la kweli. (Mwa. 3:15) Andrea alikuwa amekutana na mutu huyo ambaye alipaswa kukomboa wanadamu, Masiya mwenyewe! Petro alienda haraka kukutana na Yesu.

8. Jina ambalo Yesu alimupatia Petro lina maana gani, na sababu gani watu fulani wanaona kama Petro hastahili jina hilo?

8 Mupaka hapo, Petro alikuwa anajulikana kwa jina Simoni, ao Simeoni. Lakini Yesu alimutazama na akamuambia: “‘Wewe ni Simoni mwana wa Yohana; utaitwa Kefa’ (ambalo linatafsiriwa Petro).” (Yoh. 1:42) “Kefa” ni neno la kawaida linalomaanisha “jiwe,” ao “mwamba.” Ni wazi kwamba maneno ya Yesu yalikuwa ya unabii. Aliona mbele ya wakati kwamba Petro atakuwa kama mwamba, mutu imara mwenye kutegemeka kati ya wafuasi wa Kristo. Lakini je, Petro mwenyewe alijiona kuwa mutu mwenye imani kama mwamba? Inaonekana jibu ni hapana! Hata watu fulani wanaosoma Injili leo hawamuone Petro hivyo. Wengine wamesema kwamba tabia ya Petro kama inavyoonyeshwa na Biblia, inaonekana kuwa ya mutu asiye na musimamo na mwenye kuyumbayumba.

9. Yehova na Mwana wake wanatafuta nini ndani yetu, na wewe unawaza ni sababu gani tunapaswa kukubali maoni yao?

9 Petro alikuwa na uzaifu wake na Yesu aliujua. Lakini sikuzote Yehova anatafuta sifa nzuri zilizo katika mutu, Yesu pia anamuiga Baba yake. Yesu aliona kuwa Petro ana sifa fulani nzuri, kwa hiyo alitaka kabisa kumusaidia ili akomalishe sifa hizo. Leo pia, Yehova na Mwana wake wanatafuta sifa nzuri ndani yetu. Wakati fulani tunaweza kuwaza kwamba hawawezi kupata sifa nzuri ndani yetu. Lakini kama Petro, lazima tukubali kwanza maoni yao na kujiacha kufundishwa na kufinyangwa nao.—Soma 1 Yohana 3:19, 20.

“Acha Kuogopa”

10. Inaonekana Petro alijionea nini, hata hivyo alirudilia kufanya nini?

10 Inaonekana Petro alimusindikiza Yesu katika safari yake ya kuhubiri iliyofuata. Kwa hiyo, alimuona Yesu akifanya muujiza wake wa kwanza, kubadili maji yawe divai katika karamu ya ndoa huko Kana. Na jambo la maana zaidi ni kwamba alimusikia Yesu akizungumuzia Ufalme wa Mungu, ujumbe wenye kupendeza na unaotolea watu tumaini. Hata hivyo, alimuacha Yesu na kurudilia kazi yake ya kuvua samaki. Miezi fulani baadaye, Petro anakutana tena na Yesu, na wakati huu Yesu anamuambia Petro amufuate ili afanye kazi ya kuhubiri wakati wote pamoja naye.

11, 12. (a) Kazi ngumu ambayo Petro alifanya usiku muzima ilikuwa na matokeo gani? (b) Anapomusikiliza Yesu, labda Petro anajiuliza nini?

11 Usiku muzima Petro na wenzake walikuwa wamefanya kazi ya bure. Walishusha nyavu zao tena na tena, lakini hawakupata kitu. Bila shaka, Petro alitumia uzoefu na ufundi wake wote ili kupata samaki. Alijaribu nafasi mbalimbali katika bahari hiyo ili apate mahali samaki hao walikuwa wanakula. Kwa kweli, kuna wakati muvuvi wa samaki angetaka awe na uwezo wa kutazama ndani ya maji na kuona mahali samaki wapo ao kuwa na uwezo wa kuwafanya waingie katika nyavu zake, Petro pia angeweza kuwa na tamaa hiyo. Lakini, kuwaza hivyo kungemufanya avunjike moyo hata zaidi. Petro havue samaki ili kujifurahisha; hiyo ndio kazi yake inayotegemeza familia yake. Mwishowe, walirudi inchi kavu bila kunasa hata samaki moja. Lakini hata hivyo anapaswa kusafisha nyavu. Kwa hiyo, Yesu anapomukaribia, anamukuta mwenye kazi sana ya kusafisha nyavu.

Petro hachoke kumusikiliza Yesu anapozungumuzia kichwa kikubwa cha mahubiri yake, ni kusema, Ufalme wa Mungu

12 Watu ni wenye kumusonga Yesu sana, wana hamu sana ya kusikiliza kila neno analosema. Kwa kuwa watu ni wengi sana, Yesu anaingia katika mashua ya Petro na anamuomba aipeleke mbali kidogo na inchi kavu. Kwa sababu wakiwa juu ya maji, watu wanaweza kwa mbali kusikia waziwazi sauti ya Yesu, basi anaanza kuwafundisha watu hao wengi. Petro anasikiliza kwa uangalifu sana kama vile watu walio inchi kavu wanavyofanya. Hachoke kumusikiliza Yesu anapozungumuzia kichwa kikubwa cha mahubiri yake, ni kusema, Ufalme wa Mungu. Labda Petro anaona namna ni pendeleo kabisa kumusaidia Kristo kueneza ujumbe huo katika inchi yote, ujumbe wenye kutolea wanadamu tumaini! Lakini inawezekana Petro anajiuliza hivi, ‘je, itawezekana? Halafu familia yangu?’ Labda Petro anafikiria tena usiku uliotangulia, usiku ambao alifanya kazi ya bure; anafikiri kwamba itakuwa vigumu sana kumufuata Yesu katika kazi ya kuhubiri, na wakati uleule kuendelea na kazi yake ya kuvua samaki.—Lu. 5:1-3.

13, 14. Yesu anafanya muujiza gani kwa ajili ya Petro, na Petro anafanya nini anapoona muujiza huo?

13 Yesu anapomaliza kuwahubiria watu, anamuambia Petro hivi: ‘Vuta mupaka mahali penye kilindi, nanyi mushushe nyavu zenu, muvue.’ Petro ni mwenye kuwa na mashaka sana. Anamuambia Yesu hivi: “Mwalimu, tulitaabika usiku wote na hatukupata chochote, lakini nitazishusha nyavu kwa amri yako.” Petro amemaliza tu kusafisha nyavu na kwa hiyo hataki kuzishusha tena ndani ya maji, zaidi sana kwa kuwa wakati huu si wakati ambao mutu anaweza kuwakuta samaki wanakula! Hata hivyo, anakubali, na labda anawaita wenzake walio katika mashua ya pili wawafuate.—Lu. 5:4, 5.

14 Petro anapoanza kukokota zile nyavu, anashangaa kusikia kwamba zinakuwa nzito. Akiwa tu katika hali ya mashaka, anazikokota kwa nguvu, na mara moja anaona samaki wengi sana wakirukaruka ndani ya wavu! Kwa furaha sana, anawaita wanaume walio katika mashua ya pili waje kuwasaidia. Wanapofika inaonekana wazi kwamba mashua moja haingetosha kuchukua samaki hao wote. Wanaijaza mashua ile nyingine ya pili, na bado samaki ni wengi sana hivi kwamba mashua zote mbili zinaanza kuzama kwa sababu ya uzito wa samaki. Petro anashangaa sana. Amemuona Kristo akifanya miujiza kwa ajili ya watu wengine, lakini sasa anafanya muujiza ambao kwa mara ya kwanza utamufaidi Petro na watu wa familia yake! Yesu ana uwezo wa kufanya hata samaki waingie ndani ya nyavu! Petro anaanza kuogopa sana. Anapiga magoti na kusema: ‘Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mutu mwenye zambi, Bwana.’ Anajiona kuwa hastahili hata kidogo kushirikiana na Mutu ambaye Mungu amepatia nguvu za ajabu kama hizo.—Soma Luka 5:6-9.

‘Mimi ni mutu mwenye zambi, Bwana’

15. Yesu alimufundisha Petro namna gani kwamba hakuwa na sababu ya kuwa na mashaka, wala woga?

15 Yesu anamuambia hivi kwa upole: “Acha kuogopa. Tangu sasa na kuendelea utakuwa ukiwavua watu wakiwa hai.” (Lu. 5:10, 11) Huo haukuwa wakati wa kuwa na mashaka ao woga. Petro hakuwa na sababu yoyote ya kuwa na mashaka kuhusu mambo ya kawaida kama vile kuvua samaki, kutimizia watu wa familia yake mahitaji yao ao kuogopa kwa sababu ya makosa yake na kupungukiwa na uwezo fulani. Yesu alikuwa na kazi kubwa sana ya kufanya, huduma ambayo ingebadilisha maisha ya wanadamu wakati ujao. Alikuwa anamutumikia Mungu ambaye ‘anasamehe kwa njia kubwa.’ (Isa. 55:7) Yehova alikuwa na uwezo wa kumusaidia Petro ili aweze kutimizia watu wa familia yake mahitaji yao na kumusaidia aendelee na kazi ya kuhubiri.—Mt. 6:33.

16. Petro, Yakobo na Yohana wanatenda namna gani wanapoalikwa na Yesu, na sababu gani uamuzi waliofanya ulikuwa ndilo jambo la lazima sana?

16 Petro, Yakobo na Yohana wanatenda haraka. ‘Wanazirudisha mashua kwenye inchi kavu, wanaacha kila kitu, wanamufuata.’ (Lu. 5:11) Petro anamuamini Yesu na Yule aliyemutuma Yesu. Uamuzi ambao alifanya, ilikuwa ndio jambo la lazima sana. Leo, Wakristo wanaoondoa mashaka na kushinda woga ili kumutumikia Mungu wanaonyesha kwamba wana imani pia. Yehova hakose kuwatunza wale wanaomutegemea hivyo.—Zab. 22:4, 5.

‘Kwa Nini Umekuwa na Mashaka?’

17. Petro anakumbuka mambo gani ambayo amejionea katika miaka miwili ambayo amepitisha na Yesu?

17 Miaka miwili imepita tangu wakati Petro alikutana na Yesu. Sasa tunarudi mwanzoni mwa habari hii, ni usiku, wako juu ya Bahari ya Galilaya, upepo mukali unavuma, na Petro ni mwenye kupiga kasia. Bila shaka, inaonekana kwamba anafikiria mambo mengi ambayo amejionea. Yesu amemuponyesha mama mukwe wa Petro. Amehubiria watu kwenye Mulima. Kupitia mafundisho na kazi zake za ajabu, amehakikisha mara nyingi kwamba yeye ni Masiya, yule Muchaguliwa wa Yehova. Miezi iliyopita, bila shaka Petro amejifunza kwa kiasi fulani namna ya kuondoa mashaka na kushinda woga wake. Pia Yesu amemuchagua Petro kuwa mumoja wa wale mitume 12! Hata hivyo, karibuni Petro atatambua kwamba bado angali na woga na mashaka moyoni mwake.

18, 19. (a) Eleza ni nini Petro anaona juu ya Bahari ya Galilaya. (b) Yesu anafanya nini Petro anapomuomba atembee pia juu ya maji?

18 Sasa katika kipindi cha kesha la ine la usiku, ao wakati fulani kati ya saa 9 ya usiku na asubuhi, kwa gafula Petro anaacha kupiga kasia na anakaa vizuri. Kule mbele, juu ya mawimbi, anaona kitu fulani kinatembea! Je, ni mwangaza wa mwezi unaochezacheza juu ya mawimbi? Hapana, kitu hicho ni kirefu na kinanyooka. Kumbe ni mutu! Ndiyo, ni mutu, na anatembea juu ya bahari! Kadiri mutu huyo anavyokaribia, inaonekana kwamba anakuja upande wao. Wanafunzi wanaogopa, wanawaza ni muzuka ao pepo wa aina fulani. Mutu huyo anawaambia: ‘Mujipe moyo, ni mimi; musiogope.’ Kumbe ni Yesu!—Mt. 14:25-28.

19 Petro anasema hivi: “Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.” Mwanzoni Petro anaonyesha ujasiri mwingi. Akiwa mwenye kuchangamuka kwa sababu ya muujiza huo wa pekee, Petro anachukua uamuzi utakaotia imani yake nguvu. Kwa upole, Yesu anamuambia Petro amufuate mahali alipo. Petro anashuka kutoka katika mashua na kukanyaga juu ya maji. Wazia namna Petro anavyojisikia miguu yake inapokanyaga kitu fulani kigumu kumbe anasimama juu ya maji. Bila shaka, anashangaa anapotembea na kuenda mahali Yesu iko. Lakini, mara moja anaingiliwa na mawazo mengine.—Soma Mathayo 14:29.

‘Alipotazama ile zoruba ya upepo, akaogopa’

20. (a) Petro anakengeushwa fikira namna gani, na hilo lina matokeo gani? (b) Yesu anamufundisha Petro somo gani?

20 Petro anapaswa kumukazia Yesu uangalifu kwa sababu ni yeye anayetumia nguvu za Yehova ili kumuzuia Petro asizame. Na Yesu anafanya hivyo kwa sababu ya imani ya Petro. Lakini Petro anakengeushwa fikira. Tunasoma hivi: ‘Alipoitazama ile zoruba ya upepo, akaogopa.’ Petro anapoona mawimbi yakiipiga mashua na kuwarushia-rushia maji, anaogopa sana. Labda anawazia namna anavyoweza kuzama katika maji hayo. Kadiri woga unavyomushika sana, imani yake inapunguka. Yeye anayeitwa sasa Mwamba, ambaye angepaswa kuwa imara, anaanza kuzama kama jiwe kwa sababu ya imani yake yenye kuyumbayumba. Hata ikiwa Petro anajua kuogelea vizuri, wakati huu anachanganyikiwa kabisa na kushindwa kuogelea. Analalamika: “Bwana, niokoe!” Yesu anamushika mukono na kumukokota. Kisha, wakiwa bado juu ya maji, Yesu anamufundisha somo hili la maana: “Wewe mwenye imani kidogo, kwa nini umekuwa na shaka?”​—Mt. 14:30, 31.

21. Sababu gani ni hatari kuwa na mashaka, na tunaweza kupiganisha mashaka namna gani?

21 Maneno ‘kuwa na mashaka’ yanaeleza vizuri hali ya Petro! Mashaka yanaweza kuwa na nguvu za kumuangamiza kabisa mutu. Tukiachia mashaka nafasi, hilo linaweza kuharibisha imani yetu na kuturegeza kabisa kiroho. Tunapaswa kupiganisha mashaka kwa bidii! Namna gani? Kwa kukazia fikira mambo yanayofaa. Tukikazia akili mambo yanayotuogopesha, yanayotuvunja moyo, na yanayotukengeusha ili tusifikirie Yehova na Mwana wake, tutakuwa na mashaka sana. Lakini, tukikazia akili Yehova na Mwana wake, na tukikazia akili juu ya mambo ambayo wamefanya, yale wanayofanya leo, na yale watakayofanya wakati ujao kwa ajili ya watu wanaowapenda, tutashinda mashaka yoyote yanayoweza kuharibisha imani yetu.

22. Sababu gani inaomba tuige imani ya Petro?

22 Petro anamufuata Yesu na wanapanda katika mashua, wakati huo Petro anaona kwamba zoruba inatulia. Bahari ya Galilaya inakuwa kimya kabisa. Petro na wanafunzi wenzake wanasema hivi kwa mushangao, “Wewe kwa kweli ni Mwana wa Mungu.” (Mt. 14:33) Wakati jua linaanza kutokea juu ya bahari hiyo, bila shaka, moyo wa Petro unajaa shukrani. Amejifunza kwamba hapaswe kuruhusu woga wake umufanye awe na mashaka juu ya Yehova na Yesu. Ni kweli kwamba bado kuna mabadiliko mengi ambayo anapaswa kufanya ili awe Mukristo imara kama mwamba ambao Yesu alitabiri. Lakini anaazimia kuendelea kujikaza, na pia kukomaa. Je, wewe pia unaazimia kufanya hivyo? Ukifanya hivyo, utaonyesha kwamba unaiga imani ya Petro..