Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 1

Mumutegemee Mungu ili Ndoa Yenu Iwe na Furaha

Mumutegemee Mungu ili Ndoa Yenu Iwe na Furaha

‘Yeye aliyewaumba hao kutoka mwanzo aliwafanya mwanaume na mwanamuke.’​—Mathayo 19:4

Yehova Mungu alianzisha ndoa ya kwanza. Bibia inatuambia kwamba alimufanya mwanamuke wa kwanza na kisha ‘alimuletea mwanaume.’ Adamu alifurahi sana na akasema: ‘Mwishowe huyu ni mufupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu.’ (Mwanzo 2:22, 23) Leo pia, Yehova anataka familia iwe na furaha.

Wakati unafunga ndoa, unaweza kufikiri kwamba mambo yote yatakuwa sawa. Lakini, ukweli ni kwamba, hata bwana na bibi wenye kupendana kabisa watapambana na matatizo fulani katika ndoa yao. (1 Wakorintho 7:28) Katika broshua hii, utajifunza kanuni za Biblia. Ikiwa unatumikisha kanuni hizo, unaweza kupata furaha katika ndoa na familia yako.​—Zaburi 19:8-11.

1 KUBALI DARAKA AMBALO YEHOVA AMEKUPATIA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: Mwanaume ni kichwa cha familia.​—Waefeso 5:23.

Ikiwa uko baba ya familia, Yehova anataka umutendee bibi yako kwa upendo. (1 Petro 3:7) Alimufanya mwanamuke ili awe musaidizi wako, na anataka umuheshimie na kumupenda. (Mwanzo 2:18) Ni lazima umupende bibi yako sana hivi kwamba uwe tayari kutia faida zake mbele ya zako.​—Waefeso 5:25-29.

Ikiwa uko bibi, Yehova anataka umuheshimie bwana yako sana na kumusaidia atimize daraka lake. (1 Wakorintho 11:3; Waefeso 5:33) Ukubali maamuzi yake na kumuunga mukono kabisa. (Wakolosai 3:18) Kwa kufanya hivyo, utamufurahisha bwana yako, na Yehova pia.​—1 Petro 3:1-6.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Umuulize mwenzako mambo ambayo unaweza kufanya ili uwe bibi ao bwana muzuri zaidi. Umusikilize, na ufanye yote unayoweza ili kutengeneza hali yako

  • Umuvumilie mwenzako. Itaomba wakati ili kila mumoja wenu ajue namna anaweza kumufurahisha mwenzake

2 HANGAIKIA KABISA HALI YA MOYONI YA MWENZAKO

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: Ni lazima ufikirie faida za bibi ao bwana yako. (Wafilipi 2:3, 4) Umuone bibi yako ao bwana yako kuwa mutu wa maana sana, na ukumbuke kwamba Yehova anataka watumishi wake wawe ‘wapole kwa wote.’ (2 Timotheo 2:24) ‘Mutu anayesema bila kufikiri ni kama upanga unaochoma, lakini ulimi wa mwenye hekima unaponya.’ Kwa hiyo, wakati unasema na bibi yako ao bwana yako, chagua maneno yako kwa uangalifu. (Methali 12:18) Roho ya Yehova itakusaidia useme naye kwa upole na upendo.​—Wagalatia 5:22, 23; Wakolosai 4:6.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Umuombe Mungu akusaidie utulie na uwe tayari kusikiliza mawazo ya bibi ao bwana yako mbele ya kuzungumuzia mambo ya maana sana

  • Fikiria sana mambo ambayo utasema na namna utayasema

3 MUFANYE MAAMUZI PAMOJA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: Wakati munaoana, munakuwa ‘mwili mumoja.’ (Mathayo 19:5) Hata hivyo, mungali watu wawili na munaweza kuwa na mawazo tofauti. Kwa hiyo, ni lazima mujifunze kuwa na umoja katika mawazo. (Wafilipi 2:2) Umoja ni wa lazima wakati munachukua maamuzi. Biblia inasema hivi: ‘Kwa shauri mipango yenyewe inafanywa imara.’ (Methali 20:18) Mukubali kuongozwa na kanuni za Biblia wakati munafanya maamuzi ya maana pamoja.​—Methali 8:32, 33.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Umuelezee mwenzako habari, na pia umuambie mawazo yako na namna unajisikia

  • Mbele ya kufanya maamuzi fulani mazito, umuambie mwenzako

Biblia inaonyesha kwamba jina la Mungu ni Yehova.