Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 5

Namna ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Jamaa

Namna ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Jamaa

‘Mujivike fazili . . . unyenyekevu, upole, na ustahimilivu.’​—Wakolosai 3:12

Ndoa inaanzisha familia mupya. Hata ikiwa utaendelea kuwapenda na kuwaheshimia wazazi wako, sasa mutu wa maana sana kwako katika dunia hii ni bibi ao bwana yako. Inaweza kuwa vigumu kwa watu fulani katika jamaa yako kuelewa jambo hilo. Lakini kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia kuwa na usawaziko ili kuishi kwa amani na watu wa jamaa yako unapojikaza kufanya familia yako mupya iwe muzuri.

1 UWE NA MAONI MAZURI JUU YA WATU WA JAMAA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Muheshimie baba yako na mama yako.’ (Waefeso 6:2) Hata uwe na miaka ngapi, ni lazima uendelee kuheshimia wazazi wako. Usisahau kama bibi ao bwana yako pia anapaswa kuhangaikia wazazi wake kwa kadiri fulani. “Upendo hauna wivu,” kwa hiyo, usione vibaya wakati bibi ao bwana yako anatendea wazazi wake mambo fulani.​—1 Wakorintho 13:4; Wagalatia 5:26.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Epuka masemi kama vile “Watu wa jamaa yako hawaniheshimie” ao “Mama yako hanipendi”

  • Jikaze kuona mambo kama vile bibi ao bwana yako anayaona

2 USIKUBALI KILA JAMBO BILA SABABU

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Mwanaume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na muke wake nao watakuwa mwili mumoja.’ (Mwanzo 2:24) Wakati munaoana, wazazi wenu wanaweza kufikiri kama wangali na daraka kuwaelekea, na wanaweza kutafuta kujiingiza katika mambo ya ndoa yenu hata kama si lazima.

Ni lazima ninyi wawili muamue kuhusu mipaka ambayo hawapaswe kuvuka na kisha muwajulishe mipaka hiyo kwa busara. Munaweza kuwaambia waziwazi na moja kwa moja, lakini kwa upole. (Met 15:1) Sifa kama vile unyenyekevu, upole, na uvumilivu zitawasaidia kuwa na uhusiano muzuri pamoja na watu wa jamaa zenu na kuendelea ‘kuvumiliana katika upendo.’​—Waefeso 4:2.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Ikiwa unasumbuliwa na namna watu wa jamaa wanajiingiza katika mambo ya ndoa yenu, zungumuzia jambo hilo na bibi ao bwana yako wakati hali iko muzuri

  • Mukubaliane juu ya namna mutashugulikia mambo hayo