Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Bwana—Mufanye Nyumba Zenu Kuwa Mahali Salama

Bwana—Mufanye Nyumba Zenu Kuwa Mahali Salama

BWANA anapaswa kumutolea bibi yake usalama wa namna gani? Watu wengi wamefundishwa tangu utoto kuamini kuwa kusudi la kwanza la bwana ni kusaidia familia yake ikuwe na feza nyingi. Lakini, bibi wengi walio na vitu vingi vya kimwili wanajisikia kuwa hawana usalama katika moyo, na hata wanajisikia kuwa na woga. Kwa mufano, mwanamuke Muhispania anayeitwa Rosa, anasema hivi juu ya bwana yake: “Kwa watu wa inje alikuwa mwanaume muzuri, lakini nyumbani alikuwa bwana mugumu.” Joy, wa inchi ya Nigeria, anasema, “Wakati sikukubaliana na bwana yangu, alikuwa ananiambia, ‘Unapaswa kufanya kila kitu ninasema kwa sababu niko bwana yako.’”

Namna gani mwanaume anaweza kutimiza daraka lake la bwana kwa njia ya upendo? Inaomba nini kwa bwana ili kufanya nyumba yake kuwa mahali salama, ‘mahali pa kupumuzika’ kwa ajili ya bibi yake?—Ruthu 1:9.

MAMBO BIBLIA INASEMA JUU YA MAMLAKA YA BWANA

Hata ikiwa Mungu anaona bwana na bibi kuwa sawa, Biblia inasema kama kila mumoja iko na daraka lake katika familia. Andiko la Waroma 7:2 linasema kuwa mwanamuke mwenye kuolewa iko chini ya “sheria ya mume [bwana] wake.” Kama vile mashirika mengi yanavyochagua kichwa wa kuongoza kazi zao, Mungu amemuweka bwana kuwa kichwa cha bibi yake. (1 Wakorintho 11:3) Bwana wanapaswa kuchukua uongozi katika nyumba zao.

Ninyi bwana, namna gani munaweza kutumia mamlaka yenu muliyopewa na Mungu? Biblia inasema hivi: ‘Muendelee kuwapenda wake [bibi] zenu kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko.’ (Waefeso 5:25) Kwa kweli, hata ikiwa Yesu Kristo hakuoa, mufano wake unaweza kuwasaidia mukuwe bwana wazuri. Tuone namna gani.

MAISHA YA YESU NI MUFANO MUZURI SANA KWA BWANA

Yesu alitafuta kuburudisha wengine na kuwaregezea muzigo. Yesu aliwaahidi wale walioteswa sana na kulemewa na magumu yao: ‘Muje kwangu, . . . nami nitawaburudisha ninyi.’ (Mathayo 11:28, 29) Mara nyingi, Yesu aliwapunguzia mateso yao ya kimwili na aliwatolea musaada wa kiroho. Haishangaze kuwa watu wengi walimukaribia Yesu, wakiwa na uhakika kama atawaregezea muzigo wao!

Namna bwana wanaweza kumuiga Yesu. Tafuta namna ya kuregezea bibi yako muzigo. Bibi fulani wanajisikia kama Rosa, aliyetoa malalamiko haya: “Bwana yangu alikuwa ananiona tu sawa mutu wake wa kazi.” Tofauti na hilo, mwanaume anayeitwa Kweku, aliye na ndoa ya muzuri, anasema hivi: “Mara nyingi ninamuuliza bibi yangu namna ninaweza kumusaidia. Kwa sababu ninamupenda, mara nyingi ninajitolea kumusaidia kufanya kazi za nyumbani.”

Yesu alikuwa mwenye huruma na mwenye kufikiria watu wengine. Kwa miaka 12, mwanamuke mumoja alikuwa amesumbuliwa na ugonjwa mubaya sana. Wakati alisikia juu ya uwezo wa Yesu wa kufanya miujiza, ‘alikuwa anasema: Nikiyagusa tu mavazi yake ya inje nitapona.’ Alisema kweli. Mwanamuke huyo alimukaribia Yesu na kugusa sehemu ya chini iliyokunjwa ya nguo yake, na kisha akaponywa mara moja. Hata ikiwa watazamaji fulani waliwaza kuwa mwanamuke huyo alitenda kwa kimbelembele, Yesu alitambua kama alikuwa katika hali ngumu kabisa. * Alimuambia kwa huruma hivi: ‘Binti yangu, . . . ukuwe na afya njema kutokana na ugonjwa wako wenye kuhuzunisha.’ Aliepuka kumupatisha mwanamuke huyo haya ao kumukaripia na alitambua kuwa alikuwa mugonjwa kabisa. Kwa kufanya hivyo, alionyesha kuwa alikuwa mwanaume mwenye huruma.—Marko 5:25-34.

Namna bwana wanaweza kumuiga Yesu. Wakati bibi yako hajisikie muzuri, umuonyeshe kuwa unamufikiria zaidi na ukuwe muvumilivu. Jaribu kujitia pa nafasi yake na kuelewa mambo anatenda. Kwa mufano, Ricardo anaeleza, “Wakati ninaona kuwa bibi yangu anaweza kukasirika haraka, ninajikaza sana kuepuka kusema mambo yanayoweza kumufanya ajisikie mubaya sana.”

Yesu alikuwa anazungumuza na wanafunzi wake. Yesu alizungumuza sana na wanafunzi wake. Alisema hivi: “Mambo yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu nimewajulisha ninyi.” (Yohana 15:15) Ni kweli kwamba wakati fulani Yesu alipenda kuwa mwenyewe ili kufikiria mambo fulani na kusali. Lakini mara nyingi alizungumuza na wafuasi wake juu ya namna alikuwa anajisikia katika moyo. Usiku uliotangulia kifo chake kama vile mutenda-mabaya, aliwaambia waziwazi kuwa ‘nafsi yake ilikuwa na huzuni sana.’ (Mathayo 26:38) Hata wakati matendo yao yalimuvunja moyo, Yesu hakuacha kuzungumuza na marafiki wake hata siku moja.—Mathayo 26:40, 41.

Kufikiri juu ya mufano wa Yesu kunaweza kusaidia mwanaume akuwe bwana na baba muzuri

Namna bwana wanaweza kumuiga Yesu. Ambia bibi yako mawazo yako na namna unajisikia katika moyo. Mwanamuke anaweza kulalamika kuwa bwana yake hana magumu ya kuzungumuza mbele ya watu wengine lakini anakaa kimya nyumbani. Tofauti na hilo, ona namna Ana anajisikia wakati bwana yake anamufungulia moyo wake. Anasema hivi: “Ninajisikia kuwa ananipenda kwelikweli, na ninajisikia kuwa karibu naye.”

Epuka kumunyamazia bibi yako ukiwaza kuwa ndiyo malipizi unamupatia. Mwanamuke mumoja anasema hivi: “Wakati bwana yangu alinikasirikia, alikataa kuzungumuza na mimi kwa siku fulani. Alinifanya nijisikie kuwa mwenye kosa na mwenye kuzarauliwa.” Lakini, Edwin yeye anajikaza kuiga mufano wa Yesu. Anasema hivi: “Wakati ninakasirika, sijibie mara moja, lakini ninatafuta wakati unaofaa ili kuzungumuzia tatizo na kutafuta namna ya kulimaliza.”

Joy, aliyetajwa kwenye mwanzo wa habari hii, ameona kuwa bwana yake amebadilika tangu alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Joy anasema, “Amebadilika na anajikaza sana kuwa bwana mwenye upendo zaidi kwa kumuiga Yesu.” Mamilioni ya bibi na bwana zao wanafaidika na mafundisho hayohayo ya Biblia. Wewe pia ungependa kufaidika na mafundisho ya Biblia? Unaweza kumuomba Shahidi mumoja wa Yehova akufundishe Biblia bila kulipa.

^ fu. 10 Kulingana na Sheria ya Musa, hali ya mwanamuke huyo ilimufanya kuwa asiyekuwa safi, na kwa hiyo kila mutu mwanamuke huyo aligusa angeonwa kuwa asiyekuwa safi.—Mambo ya Walawi 15:19, 25.