Ona video zinazopatikana

Je, Biblia Inaweza Kusaidia Familia Yangu Iwe na Furaha?

Je, Biblia Inaweza Kusaidia Familia Yangu Iwe na Furaha?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Mashauri fulani yanayofuata yamesaidia wanaume na wanawake wengi wawe na furaha katika familia zao:

  1.   Andikisha ndoa yako kwenye serikali. Kujua kwamba ndoa ni mupango unaodumu maisha yote kunasaidia kabisa kuwa na ndoa yenye furaha.​—Mathayo 19:4-6.

  2.   Onyesha upendo na heshima. Hilo linamaanisha kumutendea bibi ao bwana yako namna unavyopenda utendewe.​—Mathayo 7:12; Waefeso 5:25, 33.

  3.   Epuka maneno makali. Zungumuza kwa upole hata ikiwa bibi ao bwana yako anafanya ao kutenda jambo lenye kuumiza. (Waefeso 4:31, 32) Kama Biblia inavyosema kwenye Methali 15:1: ‘Jibu, linapokuwa la upole, linageuza gazabu, lakini neno linaloumiza linafanya hasira ipande.’

  4.   Uwe mwaminifu kwa bibi ao bwana yako. Bibi ao bwana yako tu ndiye unayepaswa kuonyesha mapenzi na kufanya naye kitendo cha ndoa. (Mathayo 5:28) Biblia inasema hivi: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi.”​—Waebrania 13:4.

  5.   Fundisha watoto wako kwa upendo. Usiwe mupole kupita kiasi ao mwenye kuachilia mambo na usiwe mukali.​—Methali 29:15; Wakolosai 3:21.