Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Nifanye Nini Kama Inaonekana Kuwa Wengine Hawanipendi?

Nifanye Nini Kama Inaonekana Kuwa Wengine Hawanipendi?

 “Unapaswa kufanya yote yenye unaweza juu wengine wakupende, kama haufanye vile, hautakuwa na rafiki, hautakuwa na maisha ya muzuri sasa na wakati wenye kuja. Utafikia kusahauliwa na utabakia peke yako.”​—Carl.

 Je, ametia chumvi? Pengine. Lakini, watu fulani wako tayari kufanya kila jambo ili wasijikute mu hali yenye Carl alizungumuzia. Halafu wewe? Habari hii itakuonyesha njia ya muzuri zaidi ya kujifanyia marafiki.

 Juu ya nini vijana wanatafuta wengine wawapende?

  •   Juu hawapendi kukataliwa na vijana wengine. “Ku site ya Enternete ya kupashana habari, niliona picha za kikundi fulani chenye kilifanya matembezi na kufanya mambo fulani bila mimi. Ile ilinifanya nijiulize kama niko na shida fulani, na ilinifanya nikose amani kwa sababu niliwaza kama hawanipendi.”​—Natalie.

     MAMBO YA KUFIKIRIA: Umekwisha kukataliwa na kikundi fulani? Ulifanya jambo fulani juu waanze kukupenda?

  •   Juu hawapendi kuwa tofauti. “Wazazi wangu hawaniruhusu nikuwe na telefone. Wakati vijana wenzangu wananiomba namba yangu na ninawaambia kama sina telefone, wanasema: ‘Nini? Uko na miaka ngapi?’ Wakati ninawaambia kama niko na miaka 13, wananiangalia na macho ya huruma.”​—Mary.

     MAMBO YA KUFIKIRIA: Ni jambo gani lenye wazazi wako wanakukataza lenye linafanya ujisikie kuwa tofauti na wengine? Unaona namna gani jambo hilo?

  •   Juu hawapendi wengine wawaonee. “Ku masomo, vijana hawapendi mutu mwenye anatenda tofauti, mwenye anaongea tofauti, ao hata kuabudu kwa njia tofauti. Kama unatenda tofauti na vijana wengine, ni mwepesi wakuonee.”​—Olivia.

     MAMBO YA KUFIKIRIA: Umekwisha kutendewa mubaya juu ya kutenda tofauti na wengine? Ulifanya nini?

  •   Juu hawapendi kupoteza marafiki. “Nilijaribu kufanya mambo yote yenye watu wa kikundi chenye nilikuwa ndani walifanya. Nilikuwa ninaongea tofauti na vile ninaongeaka. Nilichekea jambo lenye halikukuwa la kuchekesha. Na hata nilikuwa ninajiunga na vijana wengine ili kumuchekelea mutu fulani, hata kama nilijua muzuri kwamba kufanya vile kungemuumiza.”​—Rachel.

     MAMBO YA KUFIKIRIA: Ni jambo la maana kabisa upendwe na vijana wenzako? Umekwisha kubadilisha namna unakuwaka juu wengine wakupende?

 Mambo yenye unapaswa kujua

  •   Kuiga wengine ili tu wakupende kunaweza kukuletea matokeo ya mubaya. Juu ya nini? Juu, mara mingi watu wanaweza kuona kama uko unajifanya vile haukuwake. Briana, wa miaka 20, anasema hivi: “Wanafunzi wenzangu hawakunipenda wakati nilijaribu kujifanya vile sikuwake. Nilitambua kama ni muzuri sana kuwa vile unakuwaka, juu watu wanaweza kuona kama uko unajifanya vile haukuwake.”

     NJIA YA MUZURI ZAIDI: Fikiria tena ni mambo gani unaona kuwa ya maana zaidi. Biblia inasema hivi: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.” (Wafilipi 1:10) Kwa hiyo ujiulize, ‘Ni nini njo ya maana zaidi​—kutafuta kupendwa na watu wenye wako na kanuni tofauti na zangu, ao kubakia namna niko?’

     “Kutafuta kuwa kama watu wengine haina maana. Hakutafanya watu wakupende zaidi, na hakutakufanya ukuwe mutu muzuri zaidi.”​—James.

  •   Kutafuta wengine wakupende kutakuchochea uanze kufanya mambo yenye haufanyake. Kunaweza kukufanya utafute tu kufurahisha watu na ufanye tu mambo yenye wengine wanapenda ufanye. Kijana mwenye kuitwa Jeremy anasema hivi: “Nilikuwa ninafanya yote yenye nilipaswa kufanya juu tu watu wa kikundi fulani wanipende, na ile iliharibisha sifa yangu. Ilifanya waniongoze kama vile walipenda. Nilifikia kuwa kitu chao cha kuchezea.”

     NJIA YA MUZURI ZAIDI: Ujue kanuni zenye zinaongoza maisha yako na uzitii, kuliko kuwa sawa vile kinyonga mwenye anabadilisha rangi juu afanane na vitu vyenye kumuzunguka. Biblia haikosee wakati inasema hivi: “Haupaswe kufuata watu wengi ili kutenda maovu.”​—Kutoka 23:2.

     “Nilijaribu kupenda kila kitu chenye walipenda​—muziki, michezo, manguo, programu za televizyo ao radio, namna yao ya kujipamba. . . Nilijaribu kuwaiga. Ninawaza kama walitambua kwamba nilikuwa ninajifanya vile sikuwake. Ninawaza kama kila mutu alijua vile, na mimi pia. Nilifikia kujiona kuwa mutu wa bure na nilijisikia kuwa peke yangu, na sikujua tena kama nilikuwa nani kabisa. Nilipoteza utu wangu. Ile ilinifundisha kama kila mutu mwenye unakutana naye hawezi kukupenda ao kukufurahia. Haimaanishe kama unapaswa kuacha kujifanyia marafiki, lakini ukuwe tu muvumilivu na usisahau kama inaomba wakati juu ufikie kuwa mutu mukomavu.”​—Melinda.

  •   Kutafuta wengine wakupende kunaweza kuharibisha mwenendo wako. Kijana mumoja mwenye kuitwa Chris alitambua kama ile ni kweli kupitia mambo yenye ilimupata binamu yake. Chris anasema hivi: “Alianza kufanya mambo yenye kwa kawaida hafanyake, kwa mufano kutumia dawa za kulewesha, juu tu wengine wamupende. Alifikia kabisa kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha, na alikuwa karibu kuharibisha maisha yake.”

     NJIA YA MUZURI ZAIDI: Uepuke watu wenye wanaonyesha kupitia maneno na matendo yao kama hawafuate kanuni za muzuri. Biblia inasema hivi: “Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.”​—Mezali 13:20.

     “Wakati fulani, ni muzuri kujikaza ili wengine wakupende. Lakini haupaswe hata kidogo kutenda mambo yenye unajua kama haiko muzuri juu tu wakupende. Marafiki wazuri watakupenda juu ya namna uko kabisa.”​—Melanie.

     Shauri: Wakati unakutana na watu wenye haujue ao wakati unajaribu kuanzisha urafiki, usiangalie tu watu wenye wanapenda mambo yenye unapendaka. Tafuta wale wenye wanafuata kanuni kama zako kuhusu mambo ya kiroho, mwenendo, na tabia za muzuri.

    Haiko kila nguo njo inaweza kukufanya upendeze. Vilevile, haiko kila mutu njo atakusaidia ukuwe na tabia za muzuri