Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Tuvunje Urafiki Wetu? (Sehemu 1)

Tuvunje Urafiki Wetu? (Sehemu 1)

 Wakati fulani ni muzuri kuvunja urafiki. Fikiria hali yenye ilimupata Jill. Anasema hivi: “Mwanzoni nilifurahi kwamba kila mara rafiki yangu mwanaume alihangaikia kujua kama nilikuwa wapi, nilikuwa nafanya nini na nani. Lakini, mwisho na mwisho sikupitisha wakati na mutu mwingine yeyote isipokuwa yeye tu. Alisikia hata wivu wakati nilipitisha wakati pamoja na watu wa familia yangu​—zaidi sana baba yangu. Wakati nilikata urafiki pamoja naye, nilijisikia kama vile wananitosha muzigo mukubwa kwenye mabega yangu!”

 Hali kama hiyo ilimupata pia Sarah. Alianza kutambua kwamba John, kijana mwanaume mwenye alipendana naye, alikuwa mwenye zarau, mwenye kuomba mambo mengi, na mwenye kukosa heshima. Sarah anasema kwamba “siku moja” rafiki yake huyo, “alikuja nyumbani akiwa mwenye kuchelewa kwa saa tatu! Wakati mama yangu alifungua mulango, alimupuuza, kisha akasema: ‘Tuende. Tunachelewa.’ Hapana ‘Ninachelewa,’ lakini ‘Tunachelewa.’ Alipaswa kuomba musamaha ao kueleza sababu gani alichelewa. Zaidi ya yote, alipaswa kumuonyesha mama yangu heshima!”

 Ni kweli kwamba, haiko lazima kuvunja urafiki kwa sababu ya tabia fulani ao tendo moja tu lenye kuvunja moyo. (Zaburi 130:3) Lakini wakati Sarah alitambua kwamba ni vile John anakuwaka, aliamua kuvunja urafiki.

 Sasa, ikiwa kama vile Jill na Sarah, unatambua kama mupenzi wako hatakuwa bibi ao bwana muzuri, utafanya nini? Kama ni vile, usipuuze hisia zako! Hata kama haiko mwepesi kukubali, inaweza kuwa muzuri kuvunja urafiki. Methali 22:3 inasema hivi: ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba na kujificha.’

 Ni kweli kwamba, haiwezi kuwa mwepesi kuvunja urafiki. Lakini, ndoa ni kifungo cha kudumu. Ni muzuri zaidi kuteseka kidogo sasa, kuliko kuteseka maisha yote kwa sababu ya kuchagua bibi ao bwana mwenye hakustahili!