Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Nakuwaka Mutu wa Haya—Nifanye Nini?

Nakuwaka Mutu wa Haya—Nifanye Nini?

 Habari ya mubaya ni hii: Haya inaweza kufanya usifurahie urafiki na wengine na mambo yenye kutia moyo.

 Habari ya muzuri ni hii: Haya haiko mubaya kila wakati. Inaweza kukusaidia uwaze mbele ya kusema. Na mutu wa haya anajua sana kuangalia mambo na kusikiliza wengine.

 Habari ya muzuri sana ni hii: Haiko kusema kama uko mutu wa haya leo, njo vile tu utabakiaka. Unaweza kuacha kuwa mutu wa haya. Hii habari itakuonyesha mambo ya kufanya.

 Jua kwanza nini njo inafanyaka uogope

 Haya inaweza kufanya uogope kuzungumuza na watu uso kwa uso. Ile inaweza kufanya uone kama hauwezi kufanya urafiki na wengine, uone sawa vile uko peke yako mu chumba yenye muko giza. Ile inaweza kukuogopesha. Lakini ukijua muzuri jambo yenye inafanyaka uogope, utavumbua kama hauna sababu ya kuogopa. Ona hii mifano tatu.

  •   Woga wa #1: “Nakosaka bya kusema.”

     Ujue hivi: Watu wanakumbukaka sana namna uliwafanya wajisikie muzuri kuliko maneno yenye ulisema. Unaweza kupiganisha ile woga kwa kujifunza kusikiliza wengine, kwa kufurahia kabisa mambo yenye wanasema.

     Fikiria hii jambo: Unapendaka rafiki wa namna gani? Wa kusema-sema kila wakati ao mwenye anajua kusikiliza wakati wengine wako wanasema?

  •   Woga wa #2: “Watu watawaza kama nawasumbua.”

     Ujue hivi: Ukuwe mutu wa kusikia haya ao hapana, watu hawatakosa kuwa na mawazo fulani juu yako. Unaweza kupiganisha ile woga na kusaidia watu wakuwe na mawazo ya muzuri juu yako kama unajieleza juu wajionee wao wenyewe kama uko mutu wa namna gani.

     Fikiria hii jambo: Ukiwaza kama kila mutu iko na mawazo ya mubaya juu yako, hauone kama pengine weye njo uko na mawazo ya mubaya juu yao, kwa kuwawazia vile hawako?

  •   Woga wa #3: “Nitasikia haya kama nasema jambo ya mubaya.”

     Ujue hivi: Ile inafikiaka kila mutu. Unaweza kupiganisha ile woga kwa kuona ile makosa kuwa nafasi ya kuonyesha wengine kama hauko mukamilifu.

     Fikiria hii jambo: Haufurahiake kuwa na watu wenye wanajua kama hawakamilike?

 Ulijua? Watu fulani wanawaza kama hawako watu wa haya juu wanatumiaka wengine ujumbe ao SMS mingi. Lakini urafiki wa kweli unafanyika ni wakati muko munazungumuza uso kwa uso. Sherry Turkle, mwenye alijifunza sana mambo ya psychologie na technologie aliandika hivi: “Ni wakati munaonana uso kwa uso na kusikia sauti za wengine njo mutakuwa marafiki wa sana.” *

Ukisha kupiganisha haya yako, utaona kama kuzungumuza na watu uso kwa uso haitakugopesha tena vile ulikuwa unawaza

 Namna ya kupiganisha haya

  •   Usijilinganishe na wengine. Haiko lazima ukuwe mutu wa kusema-sema sana. Lakini, kusudi yako ikuwe kupiganisha haya yako juu usikose kufurahia urafiki wa muzuri na mambo ya wengine yenye kutia moyo.

     “Haiko lazima mazungumuzo ikuwe ya murefu na ionekane kama weye njo uko unaiongoza. Usalimie mutu mwenye haujue na ujikaze mujuane ao unaweza kumuuliza maulizo kidogo.”—Alicia.

     Kanuni ya Biblia: “Kila mutu achunguze matendo yake mwenyewe, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi juu yake yeye mwenyewe, na hapana kwa kujilinganisha na mutu mwingine.”—Wagalatia 6:4.

  •   Ukuwe unaangalia mambo yenye iko inapitikana pembeni yako. Angalia watu wenye wanajuaka sana kufanya urafiki na uone vile wanazungumuzaka na wengine. Nini njo walifanya muzuri? Nini njo hawakufanya muzuri? Ni njia gani yenye wanatumiaka ili kuanzisha mazungumuzo, na weye unaweza kuwaiga namna gani?

     “Angalia watu wenye wanajuaka sana kufanya urafiki na ufuate mufano wao. Ona vile wako wanatenda, mambo yenye wanaambia mutu mwenye wanaona kwa mara ya kwanza.”—Aaron.

     Kanuni ya Biblia: “Kama vile chuma kinanoa chuma, ni vile pia mutu ananoa rafiki yake.”—Mezali 27:17.

  •   Uliza maulizo. Kwa kawaida, watu wanapendaka kusema byenye banawaza juu ya mambo fulani. Kwa hiyo, kuwauliza maulizo ni njia ya muzuri ya kuanzisha mazungumuzo nao. Inasaidiaka pia watu wasikaze akili sana juu yako.

     “Ukijitayarisha mbele ya wakati, ile inaweza kukusaidia upunguze wasiwasi. Unaweza hata kufikiri mbele ya wakati juu ya habari fulani ao maulizo fulani yenye utatumia wakati mutakutana na marafiki fasi fulani ao wakati utakutana na watu wenye haujue.”—Alana.

     Kanuni ya Biblia: “Mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.”—Wafilipi 2:4.

^ Maelezo inatoka mu kitabu Reclaiming Conversation.