Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Namna Gani Naweza Kujifunza Kukaza Akili Juu ya Jambo Fulani?

Namna Gani Naweza Kujifunza Kukaza Akili Juu ya Jambo Fulani?

 Juu ya nini siwezake kukaza akili juu ya jambo fulani?

 “Siwezake tena kusoma vitabu sawa zamani. Sipendake tena hata kusoma mafungu ao paragrafe za murefu.”—Elaine.

 “Nikiona kama video iko inaenda polepole, ninaifanyaka iende mbio-mbio.”—Miranda.

 “Wakati niko nakaza akili juu ya jambo fulani ya maana na palepale telefone yangu inalia, mawazo yangu yote inakuwa tu: Kuangalia kama nani njo ameniandikia’”—Jane.

 Vyombo ya kielektroniki vinaweza kufanya mutu ashindwe kukaza akili juu ya jambo fulani? Wamoja wanasema, ndiyo. Nicholas Carr, muandikaji na mushauri wa mambo ya namna ya kusimamia kompanyi, anaandika hivi: “Kadiri tunazoea sana kutumia Enternete, ni vile tunafanya akili yetu izoee kuenda huku na huku. Enternete inatusaidia kupata habari mbio sana, lakini haitusaidie tukaze akili juu ya zile habari.” *

 Vyombo vya kielektroniki vinaweza kufanya tushindwe kukaza akili juu ya jambo fulani. Tuone hali tatu.

  •   Wakati uko unazungumuza na mutu. Kijana fulani mwanamuke, mwenye anaitwa Maria, alisema hivi: “Hata wakati watu wako wanazungumuza uso kwa uso, utaona wengine wako wanaandika ujumbe, kucheza michezo ao kuzungumuza na wengine kupitia telefone yao. Hawakaze akili kabisa juu ya mambo yenye wako wanazungumuzia.”

  •   Wakati uko mu masomo. Kitabu Digital Kids kinasema: “Wanafunzi wengi wanasema kama wanatumikishaka vyombo vyao vya kielektroniki wakati wako mu masomo. Wanasomaka ao kuangalia habari fulani, ao kufanya mambo ingine yenye haihusu hata masomo.”

  •   Wakati uko unajifunza. Chris, wa miaka 22, anasema: “Kama telefone yangu inalia, siwezake kujizuia juu nisiiangalie. Kama uko mwanafunzi, saa moja ya kufanya devware za masomo inaweza kugeuka saa tatu ao zaidi kama haupendi kutosha macho ku telefone ao ku chombo ingine ya kielektroniki.

 Yenye usisahau ni hii: Ukiacha vyombo vya kielektroniki vikengeushe akili yako na kukuongoza, utashindwa kukaza akili juu ya mambo ya maana.

Akili yenye haiko fasi moja iko sawa vile farasi ya pori, kuliko weye njo uiongoze, ayo njo inakuongoza

 Nini njo itakusaidia uweze kukaza akili juu ya jambo fulani

  •   Wakati uko unazungumuza na mutu. Biblia inasema: “Mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.” (Wafilipi 2:4) Onyesha kama unaheshimia mwenye uko unazungumuza naye kwa kumusikiliza sana. Umuangalie wakati iko anazungumuza. Usiache vyombo vyako vya kielektroniki vikengeushe akili yako.

     “Wakati uko unazunguzumuza na mutu, usiangalie-angalie telefone yako. Onyesha kama unaheshimia mwenye uko unazungumuza naye kwa kumusikiliza sana.”—Thomas.

     SHAURI: Wakati uko unazungumuza na mutu, tia telefone yako kwenye hautaiona. Habari fulani zinaonyesha kama kuona tu telefone yako, kunaweza kufanya usikaze akili juu ya mambo yenye muko munazungumuzia, juu ikilia tu, itafanya musimamishe kwanza mazungumuzo.

  •   Wakati uko mu masomo. Biblia inasema: “Mukuwe waangalifu juu ya namna munasikiliza.” (Luka 8:18) Ile kanuni inaweza kukusaidia sana. Kama ku masomo yenu wanaruhusu kutumia Enternete mu masomo, usiangalie-angalie ujumbe, michezo ya video ao kuzungumuza na wengine ku Enternete wakati inaomba kukaza akili juu ya mambo yenye mwalimu iko anasema.

     “Ujikaze kuwa muangalifu sana mu masomo. Andika mambo ya lazima. Ikiwezekana, ikala fasi ya mbele mu masomo juu akili yako isiende huku na huku.”—Karen.

     SHAURI: Kuliko kuandika mambo ya lazima ku ordinatere, andika ku karatasi. Habari fulani zinaonyesha kama, ukifanya vile, akili yako haitakengeushwa sana na utachunga kabisa mambo yenye uko unajifunza.

  •   Wakati uko unajifunza. Biblia inasema: “Pata hekima, pata uelewaji.” (Mezali 4:5) Ile kanuni inaonyesha kama inaomba ukuwe unafikiri sana, hapana tu kusoma habari juu-juu.

     “Wakati niko najifunza, natiaka tablete yangu mu hali yenye haitanivuruga. Ile wakati siangaliake hata ujumbe. Kama mu akili yangu munakuya jambo fulani yenye sipaswe kusahau, naiandikaka.”—Chris.

     SHAURI: Ukuwe hakika kama fasi kwenye uko unajifunzia kunakusaidia ukaze akili juu ya mambo yenye uko unajifunza. Inaomba kukuwe safi na kwenye kupangiwa muzuri.

^ Maelezo ya kitabu The Shallows​—What the Internet Is Doing to Our Brains.