Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Nifanye Nini Wakati Ninafanya Makosa?

Nifanye Nini Wakati Ninafanya Makosa?

 Weye ungefanya nini?

 Soma mambo yenye ilimupata Carine, na uwazie kama inakupata. Weye, ungefanya nini?

 Carine: “Mu kuenda ku masomo, nilikuwa nikitembeza motokari mbio sana. Polisi alinisimamisha na kunilipisha feza. Nilisirika sana! Wakati nilielezea Mama, aliniomba nimuambie Papa. Sikutaka Papa ajue.”

 

  1.  Uamuzi wa A: Kunyamaza na kutumainia kama baba yako hatajua.

  2.  Uamuzi wa B: Kumuelezea baba yako mambo yote yenye ilifanyika.

 Pengine ungependa kuchagua Uamuzi wa A. Unaweza hata kufikiri hivi: Maman, atawaza kama nimekwisha kumuambia papa mambo yote. Lakini kuko sababu zenye kufaa zenye zinakulazimisha kusema wazi makosa yenye ulifanya, hata kama ni makosa ya kuvunja sheria za barabarani ao jambo lingine.

 Sababu tatu za kukubali makosa yako

  1.  1. Kwa sababu kufanya hivyo ni jambo lenye kufaa. Biblia inasema Wakristo wanapaswa: “Kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”​—Waebrania 13:⁠18.

     “Ninajikaza sana kusema kweli kila mara, kukubali makosa yangu, na kukubali matokeo ya makosa hayo.”​—Alexis.

  2.  2. Kwa sababu kwa kawaida watu wanasamehe wale wenye kukubali makosa yao. Biblia inasema hivi: “Anayefunika makosa yake hatafanikiwa, lakini yeye anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.”​—Methali 28:13.

     “Inaomba unyenyekevu ili kukubali makosa yetu, na tukikubali makosa yetu, watu watatuamini zaidi. Wataona kama tunapenda kusema kweli. Wakati tunakubali makosa yetu, hilo linafanya yasionekane tena kuwa makosa.”—Richard.

  3.  3. Jambo la maana zaidi, utamufurahisha Yehova Mungu. Biblia inasema: ‘Mutu mwenye hila ni chukizo kwa Yehova, lakini urafiki Wake uko pamoja na watu wanyoofu.’​—Methali 3:​32.

     “Kisha kufanya kosa nzito, nilitambua kama nilipaswa kusema mambo yenye nilifanya. Yehova hawezi kunibariki kama sifanye mambo kwa njia yenye anakubali.”—Rachel.

 Kisha Carine alifanya nini? Alijaribu kuficha mambo ili baba yake asijue kama walimulipisha feza. Lakini hangeweza kuficha jambo hilo milele. Carine anasema: “kisha mwaka moja hivi, papa alikuwa anaangalia karatasi za assurance akavumbula karatasi hiyo yenye kuwa na jina yangu. Ni vile walinivumbula. Maman alisirika sana kwa sababu sikufanya jambo lenye alikuwa ameniambia nifanye!”

 Somo: Carine anasema: “Mutu akificha makosa yake, anafanya hali ikuwe mubaya zaidi. Mwisho na mwisho, utalipa makosa yako!”

 Makosa yako ikufundishe

 Kila mutu anafanya makosa. (Waroma 3:23; 1 Yohana 1:8) Lakini kama tunakubali makosa kisha tu kuyafanya, hilo litaonyesha kama tuko wanyenyekevu na tunakomaa.

 Jambo la kufuata ni kuacha makosa yako ikufundishe. Jambo la huzuni ni kwamba, vijana fulani hawaache makosa yao iwafundishe! Pengine wanajisikia kama kijana moja mwanamuke mwenye kuitwa Priscille. Anasema hivi: “Nilikuwa navunjika moyo sana kwa sababu ya makosa yenye nilifanya. Kwa sababu sikujiona tena kuwa wa maana, niliona makosa yangu kuwa muzigo muzito wenye siwezi kubeba. Nilijisikia kama sina nguvu na nilijiona kuwa wa bure.”

 Na weye unajisikia hivyo wakati fulani? Kama jibu ni ndiyo, ukumbuke jambo hili: kuendelea kuwaza sana juu ya makosa ya zamani ni kama unatembeza motokari na unakazia macho kioo cha kuangalia nyuma. Kuendelea kukazia akili makosa ya zamani, kutakufanya ujisikie kama haufae kitu na unaweza hata kukosa nguvu za kupiganisha matatizo ya wakati wenye kuja.

 Ujikaze kuwa na mawazo ya muzuri juu ya makosa yako ya zamami

 “Kumbuka makosa yenye ulifanya na uiache ikufundishe ili usiirudilie tena. Lakini, usiikumbuke tena na tena mupaka uvunjike moyo.”—Elliot.

 “Nawaza kama, kufanya makosa kunanifundisha. Najikaza sana ili kila kosa lenye ninafanya linifundishe jambo fulani na nitengeneze tabia yangu ili nisirudilie tena kosa hilo wakati wenye kuja. Kwa kweli, hiyo ndiyo njia yenye kufaa kwa sababu, inanisaidia kukomaa.”—Vera.