Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Biblia Inaweza Kunisaidia Namna Gani?​—Sehemu ya 2: Mambo ya Kufanya Juu Ufurahie Kusoma Biblia

Biblia Inaweza Kunisaidia Namna Gani?​—Sehemu ya 2: Mambo ya Kufanya Juu Ufurahie Kusoma Biblia

 Kijana mwenye kuitwa Will anasema kama “Biblia inaweza kuchokesha kama mutu hajue namna ya muzuri ya kuisoma.”

 Unapenda kujua mambo yenye itakusaidia ufurahie kusoma Biblia? Hii habari itakusaidia.

 Wazia mambo yenye uko nasoma

 Uite akili mu mambo yenye uko nasoma. Unaweza kufanya hivi:

  1.   Chagula habari yenye unapenda kujifunza. Unaweza kuchagula habari ao andiko fulani mu Vitabu vya Injili, ao unaweza kuchagula habari fulani kati ya habari za Usomaji wa Biblia Wenye Kuchezwa zenye zinapatikana ku jw.org.

  2.   Soma ile habari. Unaweza kuisoma weye peke, ao kuisoma kwa sauti na marafiki wako na watu wa familia yako. Mutu mumoja anaweza kusoma maneno ya musimuliaji na wengine wanaweza kusoma maneno ya watu wengine wenye kuwa mu ile habari.

  3.   Pima tena kufanya hivi:

    •   Chapa picha zenye zinafasiria ile habari. Ao chapa picha zenye kuonyesha namna matukio ilifuatana. Andika maelezo kidogo yenye kufasiria mambo yenye iko inapitikana mu kila picha.

    •   Wakati uko nasoma habari ya mutu fulani mwenye alikuwa muaminifu, uandike sifa na matendo yake ya muzuri na baraka zenye alipata.

    •   Kisha kusoma, ukuwe sawa vile weye njo uko unaeleza ile habari. Eleza ile habari mu njia mbalimbali, ukuwe sawa vile “uko unauliza maulizo” watu wenye kuzungumuziwa mu ile habari na watu wenye walikuwaka pale.

    •   Kama mutu mwenye kuzungumuziwa mu ile habari alikamataka uamuzi mubaya, wazia namna mambo ingekuwaka kama hangefanyaka vile. Kwa mufano, wazia namna Petro alimukanaka Yesu. (Marko 14:66-​72) Petro alipaswaka kufanya nini mu ile hali?

    •   Kama unajisikia kufanya jambo fulani ya mupya, na weye pima kuandika drama yenye inategemea habari yenye umesoma. Utie ndani somo mbalimbali zenye umejifunza mu ile habari.​—Waroma 15:4.

      Unaweza kufanya ionekane kuwa uko naona kabisa mambo yenye uko nasoma!

 Tafuta kujifunza mambo mingi zaidi!

 Kama unachunguza mambo ya kidogo-kidogo, unaweza kuvumbula mambo mingi ya maana mu habari yenye uko nasoma. Kusema kweli, wakati fulani neno moja ao mbili inaweza kutufundisha mambo mingi sana.

 Kwa mufano, linganisha Matayo 28:7 na Marko 16:7.

  •    Juu ya nini Marko aliongeza kama Yesu alisema kuwa atatokea na wanafunzi wake “na Petro”?

  •  Jambo ya kukusaidia kuelewa: Marko hakujioneaka ile mambo; inawezekana Petro njo alimuelezeaka.

  •  Mambo ya maana yenye utavumbula: Juu ya nini inawezekana kabisa Petro alijisikiaka muzuri wakati alisikia kama Yesu anapenda kumuona tena? (Marko 14:66-​72) Namna gani Yesu alionyesha kama alikuwa rafiki muzuri wa Petro? Namna gani unaweza kuiga Yesu na kujikaza kuwa rafiki muzuri kwa wengine?

 Wakati unawazia mambo yenye uko nasoma, na unachunguza mambo ya kidogo-kidogo, utafurahia sana kusoma Biblia!