Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Ni Muzuri Kufanya Mambo Mingi kwa Wakati Moja?

Ni Muzuri Kufanya Mambo Mingi kwa Wakati Moja?

 Unajuaka sana kufanya mambo mingi kwa wakati moja?

 Unajuaka sana kufanya mambo mingi kwa wakati moja? Watu wengi wanawazaka kama wale wenye wanazoea mambo ya teknolojia tangu utoto wanajua sana kufanya mambo mingi kwa wakati moja kuliko wale wenye wanajifunzia mambo ya teknolojia mu bukubwa. Ni kweli kabisa?

 NDIYO ao HAPANA?

  •   Kufanya mambo mingi kwa wakati moja inasaidia ufanye mambo mingi mu wakati kidogo.

  •   Kama unajifunza kufanya mambo mingi kwa wakati moja, utazoea kufanya vile.

  •   Vijana njo wanawezaka sana kufanya mambo mingi kwa wakati moja, hapana watu wenye walishakomala.

 Kama jibu yako ni “ndiyo” ku ile mawazo yote, ni kusema, kuko mambo yenye haujue.”

 Mambo yenye inafaa kujua

 Unawaza unaweza kufanya mambo mbili kwa wakati moja? Unaweza kufanya mambo mbili kwa wakati moja kama ile jambo ingine haiombe kuikazia akili sana. Kwa mufano, unaweza kusafisha chumba yako muzuri na uko unasikiliza muziki.

 Lakini kama uko unafanya kazi mbili kwa wakati moja, na kama zile kazi zote mbili zinaomba uangalifu sana, inawezekana hautazifanya zote mbili muzuri. Pengine njo maana kijana moja mwanamuke, mwenye kuitwa Katherine, anafasiria ile jambo hivi: “Kufanya mambo mingi kwa wakati moja, ni kufanya mambo ovyo-ovyo kwa wakati moja.”

 “Nilikuwa nazungumuza na mutu fulani, kisha iliomba nijibie ujumbe fulani ku telefone. Nilipima kufanya mambo mbili kwa wakati moja. Mambo ilikuwa namna gani? Sikuelewa mambo yote yenye tulikuwa nazungumuza na sikuweza kuandika muzuri ile ujumbe.”—Caleb

 Sherry Turkle, mwenye kujua sana mambo ya Teknolojia, aliandika hivi: “Wakati tunawaza kama tunaweza kufanya mambo mingi muzuri kwa wakati moja, . . . uwezo wetu wa kukaza akili juu ya jambo fulani unapunguka kila mara wakati tunaongeza jambo ingine ku mambo yenye tulikuwa tunafanya. Ubongo wetu unachamuka na tunafikia kuwaza kama tuko tunafanya mambo muzuri sana, kumbe tuko tunaifanya mubaya.” *

 “Wakati fulani, nawazaka kama niko nafanya muzuri kwa kuandikia mutu fulani ujumbe na niko ninazungumuza na mutu mwingine. Lakini, kisha navurugika, na kufikia kutambua kama maneno yenye nilipaswa kutia mu ujumbe njo naanza kuambia mwenye tuko nazungumuza naye, na ile yenye nilikuwa nazungumuza naye njo niko naandika!”—Tamara.

 Watu wenye wanapendaka kufanya mambo mingi kwa wakati moja, wanajivurugaka tu bure. Kwa mufano, hawamalizake mbio kufanya devware zao ao kazi zingine. Wakati ingine wanarudiliaka-rudiliaka kazi yenye waliwaza kama walishamaliza. Ile yote inafanyaka wakose wakati ya kufanya mambo ingine!

 Kulingana na Thomas Kersting, (munganga wa mambo ya akili na mushauri wa mambo ya masomo), kama tunalinganisha ubongo wa mutu na kabati mwenye dosye zinapaswa kupangwa muzuri, ubongo wa mutu mwenye anapenda sana kufanya mambo mingi kwa wakati moja uko sawa kabati mwenye dosye zimepangwa ovyoovyo.

 “Vile utakuwa uko unafanya mambo mingi kwa wakati moja, na njo vile utakuwa unasahau mambo ingine ya lazima. Ku mwisho, utavumbua kama umejiongezea tena kazi ya mingi na umepoteza wakati.”—Teresa.

Kupima kufanya mambo mingi kwa wakati moja ni sawa vile kupima kutembeza motokari mu barabara mbili kwa wakati moja

 Namna muzuri ya kufanya

  •   Ujizoeze kukaza akili juu ya kazi moja kwanza. Haitakuwa mwepesi, zaidi sana kama ulizoeaka kufanya mambo mingi kwa wakati moja, sawa vile kujifunza mambo ya masomo na uko unaandikia wenzako ujumbe ku telefone. Lakini Biblia inatuambia ‘tuhakikishe mambo ya maana zaidi.’ (Wafilipi 1:10) Kuko mambo ya maana kuliko ingine. Kwa hiyo, amua ni kazi gani njo utaanza nayo, kisha ukaze akili yako juu ya ile kazi mupaka iishe.

     “Akili yenye ilishazoea kufanya mambo mingi kwa wakati moja iko sawa vile mutoto mwenye hasikiake, inaomba kumukataza mambo fulani hata kama alishapenda kuifanya.”—Maria

  •   Epuka mambo yenye inaweza kufanya akili yako iende huku na huku. Unakuwaka na tabia ya kuangalia-angalia telefone yako wakati uko unajifunza? Kama ni vile, uitie mu chumba ingine. Funga televizyo. Sahau kwanza mambo ya kuzungumuza na wenzako ku Enternete! The Biblia inasema: “Mutumie muzuri zaidi wakati wenu.”—Wakolosai 4:5.

     “Nimeelewa kama ninajisikiaka muzuri wakati nakazaka akili juu ya kazi moja kwanza. Kisha naivuta ku liste ya mambo ya kufanya, na naanza kazi ingine. Ile inanifurahishaka sana.”—Onya.

  •   Kaza akili juu ya mambo yenye muko nazungumuza na mutu. Kuangalia-angalia telefone yako wakati uko unazungumuza na mutu ni kukosa adabu, na ile haisaidiake mazungumuzo iendelee muzuri. Biblia inasema tutendee wengine vile tunapenda watutendee.—Matayo 7:12.

     “Wakati fulani, saa nakuwaka niko nazungumuza na dada yangu, anakuwaka iko anaandikia mutu mwingine ujumbe ao kufanya jambo ingine ku telefone yake. Ile inanikasirishaka sana! Lakini kusema kweli, kuko wakati na miye nafanyaka vile!”—David.

^ Inatoka mu kitabu Reclaiming Conversation.