Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Ni Nini Inaweza Kunisaidia Nifurahie Kufanya Mazoezi?

Ni Nini Inaweza Kunisaidia Nifurahie Kufanya Mazoezi?

 Juu ya nini ninapaswa kufanya mazoezi?

 Katika inchi fulani, vijana wanatumia wakati kidogo ili kufanya mazoezi, na hilo linatia afya yao katika hatari. Biblia iko na haki wakati inasema kama “mazoezi ya mwili ni yenye faida.” (1?Timoteo 4:8) Fikiria mambo yenye kufuata:

  •   Mazoezi inaweza kukufanya ujisikie muzuri zaidi. Mazoezi ya mwili inafanya ubongo wako utokeze homoni zenye kuitwa endorphines zenye kufanya mutu ajisikie muzuri na kuwa mwenye furaha. Watu fulani wanasema kama mazoezi ni dawa ya kupiganisha hali ya kushuka moyo.

     “Kama ninakimbia asubui sana mbele ya kufanya mambo ingine yote, ninatumikaka muzuri na ninakuwaka na furaha siku nzima. Kukimbia kunafanya nijisikie muzuri.”—Regina.

  •   Mazoezi inaweza kufanya ukuwe na umbo ya muzuri. Kufanya mazoezi kwa kiasi kutafanya ukuwe na nguvu zaidi, ukuwe na afya ya muzuri zaidi, na mwenye kujitumainia zaidi.

     “Ninajisikia muzuri kama ninajiinua mara kumi kwenye chuma —mwaka wenye ulipita, singeweza kufanya vile hata mara moja! Na jambo la muzuri zaidi, ninajua kama niko ninahangaikia mwili wangu.”—Olivia.

  •   Kufanya mazoezi kunaweza kurefusha maisha yako. Kufanya mazoezi kunasaidia upumue muzuri na kunasaidia moyo wako utumike muzuri. Mazoezi yenye kufanya mutu apumue sana inaweza kuzuia ugonjwa wenye kufanya mishipa ya moyo ijifunge, wenye kuua sana wanaume na wanamuke.

     “Kama tuko tunafanya mazoezi kwa ukawaida, tunamuonyesha Muumbaji wetu kama tunaona mwili wenye alitupatia kuwa wa maana sana.”—Jessica.

 Kwa kifupi: Mazoezi itakuletea faida mingi juu ya afya wakati wenye kuja, na inaweza kukuletea faida hata leo. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Tonya anasema hivi: “Hakuna siku utasema hivi: ‘Ingekuwa muzuri kama singeenda kufanya ile matembezi ao kukimbia.’ Wakati ninajikaza sana ili kufanya mazoezi hata kama kuko mambo yenye ingenizuia, sihuzunike hata kidogo.”

Kama motokari haitunzwe itafikia kuacha kufanya kazi; jambo hilo linaweza kufikia mwili wako kama unazarau kufanya mazoezi

 Ni nini inanizuia kufanya mazoezi?

 Kuko mambo mbalimbali yenye inaweza kuzuia mutu kufanya mazoezi:

  •   Kukosa hamu. “Wakati mutu angali kijana, anawazaka kama hakuna kitu kinaweza kumufikia. Ni nguvu kuwazia kama wakati fulani utakuwa na matatizo ya afya. Unaweza kuwaza kama ni watu wenye kuzeeka tu njo wenye kuwa na matatizo ya afya.”—Sophia.

  •   Kukosa wakati. “Juu niko na mambo mingi ya kufanya, ninapaswa kupanga wakati wa kula muzuri na kulala, lakini sikuzote, imekuwa nguvu sana kwangu kupata wakati wa kufanya mazoezi.”—Clarissa.

  •   Sijajiandikisha mahali fulani pa kufanyia mazoezi. “Inaomba feza mingi ili uendelee kuwa na afya ya muzuri, kwa hiyo, unapaswa kulipa feza ili kujiandikisha mahali pa kufanyia mazoezi!”—Gina.

 Mambo ya kufikiria:

 Ni nini inakuzuia wewe kufanya mazoezi? Itaomba ujikaze sana ili kushinda kizuizi hicho, lakini utapata matokeo ya muzuri.

 Ni nini itanisaidia nikuwe nafanya mazoezi?

 Ona mashauri fulani:

  •   Hangaikia afya yako wewe mwenyewe.—Wagalatia 6:5.

  •   Epuka kujitafutia visababu. (Muhubiri 11:4) Kwa mufano, haiko lazima ujiandikishe mahali fulani pa kufanyia mazoezi ili uanze kufanya mazoezi. Tafuta tu jambo fulani lenye unafurahia na uanze kulifanya kwa ukawaida.

  •   Ili upate mawazo, uliza wengine ni mazoezi gani wanafanyaka.—Mezali 20:18.

  •   Ukuwe na programu fulani. Ujiwekee miradi fulani na ukuwe unaandika miradi yenye umetimiza ili uendelee kuwa na hamu ya kufanya mazoezi.—Mezali 21:5.

  •   Tafuta mutu mwenye utakuwa unafanya mazoezi pamoja naye. Kama unapata rafiki mwenye utakuwa unafanya mazoezi pamoja naye kwa ukawaida, anaweza kukutia moyo na kukusaidia uendelee.—Muhubiri 4:9, 10.

  •   Ujue kama kutakuwa mambo ya kukuzuia kufanya mazoezi, lakini usiache kufanya mazoezi wakati ile mambo inatokea.—Mezali 24:10.

 Ukuwe na usawaziko

 Biblia inashauria wanaume na pia wanamuke wakuwe ‘wenye kiasi katika tabia.’ (1?Timoteo 3:2, 11) Kwa hiyo, ukuwe na usawaziko kuhusu mazoezi. Mara mingi, watu wenye kufanya mazoezi kupita kiasi wanaonekana kuwa wenye majivuno. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Julia anasema hivi: “Mwanaume mwenye iko na misuli mingi lakini hana akili mingi, hawezi kunivutia.”

 Pia, ukuwe muangalifu juu ya mambo yenye kuchochea watu wafanye mazoezi kupita uwezo wao. Ile mambo inaweza inaweza kukuletea matokeo ya mubaya kimwili na kufanya usikazie akili “mambo ya maana zaidi” mu maisha.—Wafilipi 1:10.

 Tena, ile mambo ya kuchochea watu wafanye mazoezi inaweza kufanya uvunjike moyo. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Vera anasema hivi: “Vijana wengi wanamuke wanaweka picha za watu wenye wanapenda kuiga, na wanaangalia picha hizo wakati wanakosa hamu ya kufanya mazoezi. Lakini, wanafikia kuanza kujilinganisha na watu hao na kisha wanavunjika moyo. Ni muzuri zaidi mutu akuwe na muradi wa kufanya afya yake ikuwe muzuri, hapana tu umbo yake.”