Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Ni Jambo ya Maana Kujulikana Sana ku Site za Enternete za Kupashana Habari?

Ni Jambo ya Maana Kujulikana Sana ku Site za Enternete za Kupashana Habari?

Kijana mwenye kuitwa Elaine anasema hivi: “Wakati niliona wanafunzi wenzangu wangu wako na marafiki wengi ku site za Enternete za kupashana habari, niliwaza hivi: Ah! wanajulikana sana!’ Kusema kweli, niliwasikilia wivu.”

 Ulishajisikia vile? Kama ni vile, hii habari itakusaidia uepuke mahangaiko ya kujaribu kujulikana sana ku site za Enternete za kupashana habari.

 Kuko hatari gani?

 Mu Mezali 22:1, Biblia inasema kama “inafaa kuchagua jina la muzuri kuliko kuchagua mali nyingi.” Kwa hiyo, haiko mubaya kuwa na sifa ya muzuri ao kutaka wengine watupende.

 Lakini wakati fulani, tamaa ya kupenda kukubaliwa inaweza kugeuka na kuwa tamaa ya kupenda kujulikana sana. Kuko hatari? Onya, wa miaka 16, anajibu ndiyo. Anasema hivi:

 “Nimeona vile watu wanafanya mambo ya upumbavu, sawa vile kuruka kutoka ku gorofa ao étage ya pili ya nyumba, juu tu waonekane watu wa ajabu sana.”

 Juu ya kujionyesha, watu fulani wanarekodi video na wako wanafanya mambo ya upumbavu na wanazitia ku Enternete. Kwa mufano, vijana fulani walitia ku Enternete video zenye kuwaonyesha na wako wanakula sabuni zenye sumu, jambo yenye mutu hapaswe kufanya!

 Biblia inasema hivi: “Msifanye chochote kwa moyo wa fitina au kwa majivuno ya bure.”​—Wafilipi 2:3, Biblia Habari Njema.

 Jambo ya kufikiria:

  •   Kujulikana sana ku site ya Enternete ya kupashana habari ni ya maana sana kwako?

  •   Unaweza kutia maisha yako mu hatari juu tu ya kujionyesha na juu tu marafiki wako wakukubali?

 Kuwaza kama unajulikana sana ni ndoto

 Kila mara, watu hawafanyake mambo yenye kuwa hatari ili wajulikane sana. Erica, wa miaka 22, anaonyesha njia ingine yenye watu wanatumiaka. Anasema hivi:

 “Watu wengi wanatiaka ku Enternete picha zenye kuonyesha mambo yenye wako wanafanya. Ni sawa vile wako na marafiki wengi sana wenye wanapitisha nao wakati mingi. Ile inafanya watu wawaze kama wanajulikana sana.”

 Cara, wa miaka 15, anasema kama watu fulani wanatia ku Enternete habari za uongo juu ionekane sawa vile wanajulikana sana. Anasema hivi:

 “Nimeona watu wametia picha zenye zinawaonyesha sawa vile wako ku karamu, kumbe wako ku nyumba.”

 Matthew, wa miaka 22, anasema kama naye alishakafanya vile. Anasema hivi:

 “Nilitia picha ku Enternete, kisha nikaonyesha kama nilikuwa ku Mulima Everest, hata kama siyafikaka Asia!”

 Biblia inasema hivi: “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”​—Waebrania 13:18.

 Jambo ya kufikiria:

  •   Ulishakatia habari za uongo ku Enternete juu tu ujulikane sana?

  •    Picha na maelezo yenye unatiaka ku Enternete inaonyesha kabisa vile uko na inapatana kabisa na mambo yenye unaamini?

 Kuwa na marafiki na kuwa na alama mingi zenye kuonyesha kama watu wanafurahia mambo yenye ulitia ku Enterne ni jambo ya maana kabisa?

 Watu wengi wanawaza kama ili kujulikana sana ku Enternete, inaomba kuwa marafiki wengi na alama mingi zenye kuonyesha kama watu wanafurahia mambo yenye unatia ku Enternete. Vile njo Matthew, mwenye tulishazungumuzia, alikuwa nawaza. Anasema hivi:

 “Nilikuwa nazoea kuuliza wengi, ‘Uko na marafiki ngapi ku Enternete?’ ao ‘Ni hesabu gani kubwa ya alama yenye kuonyesha kama watu wanafurahia mambo yenye unatia ku Enternete yenye ulishakapata?’ Juu ya kuwa na marafiki wengi, niliomba hata watu wenye sijui wakuwe marafiki wangu na kuwaza kama wataitika. Nilikomalisha tamaa ya kupenda kujulikana sana, na site za Enternete za kupashana habari ziliongeza ile tamaa.”

Kupenda kujulikana sana ni sawa vile chakula yenye haijenge mwili, inaweza kufanya ufurahi, lakini haikusaidie kabisa

 Maria, wa miaka 25, anasema kama watu fulani wanawazaka kama kuwa na marafiki na kuwa na alama mingi yenye kuonyesha kama watu wanafurahia mambo yenye unatia ku Enternete, ile njo inaonyesha kama uko mutu wa maana. Anasema hivi:

 “Kama kijana mwanamuke anatia picha yake ku Enternete na haipate alama za mingi zenye kuonyesha kama watu wanaipenda, ile inafanya mara moya aseme kama hana sura ya muzuri. Ile ni mawazo yenye haifae, lakini mu hali ya vile, wengi wanafikiriaka vile. Ni njia fulani ya kujitesa wao wenyewe.”

 Biblia inasema hivi: “Tusikuwe tunajisifu, tusichochee mashindano kati yetu, tusisikiliane wivu.”​—Wagalatia 5:26.

 Jambo ya kufikiria:

  •   Kama unatumiaka site za Enterne za kupashana habari, unaona kama ile inakuchocheaka kujilinganisha na wengine?

  •    Jambo yenye unahangaikia sana ni kuwa na marafiki wengi ku Enternete ao ni kuwa na marafiki wa kweli wenye wanakuhangaikia?