Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Nilishavunja Sheria ya Familia—Nifanye Nini Sasa?

Nilishavunja Sheria ya Familia—Nifanye Nini Sasa?

 Karibu mu kila familia muko sheria. Kwa mufano, kuko sheria yenye inakuonyesha saa yenye unapaswa kurudia ku nyumba, namna unapaswa kutumia vyombo vya kielektroniki, na namna ya kutendea wengine.

 Utafanya nini kama unavunja sheria moja ya familia yenu? Hauwezi kubadilisha jambo yenye ilishatokea. Lakini kuko kitu unaweza kufanya juu mambo isiharibike zaidi. Hii habari itakuonyesha mambo ya kufanya.

 Jambo yenye haupaswe kufanya

  •   Ikiwa wazazi wako hawajue kama ulivunja sheria fulani, pengine utapenda kuwaficha.

  •   Kama wanajua, utapenda kujitetea ao kutupia mutu mwingine ile kosa.

 Ile yote haiko muzuri. Juu ya nini? Kuficha mambo yenye ulifanya ao kujitetea-tetea, ni kutenda sawa mutoto. Na inaonyesha wazazi wako kama hauyakomala.

 “Kusema uongo haisaidiake hata kidogo. Bipande bishuke, mambo yenye ulifanya itajulikana. Na malipizi yenye watakupatia itakuwa ya nguvu kupite ile yenye wangekupatia kama ungesema kweli ku mwanzo.”—Diana.

 Namna muzuri ya kufanya

  •   Itika mambo yenye ulifanya. Biblia inasema: “Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa.” (Mezali 28:13) Wazazi wako wanajua kama haukamilike, wanapenda tu ukuwe nasema kweli.

     “Wazazi wako watakuwa tayari kukusamehe kama unasema kweli. Kama unasemaka kweli watakutumainia sana.”—Olivia.

  •   Omba musamaha. Biblia inasema: “Muvae unyenyekevu.” (1 Petro 5:5) Inaomba kuwa munyenyekevu juu ufikie kusema “unisamehe” bila kujitetea-tetea.

     “Watu wenye wanaendelea kujitetea-tetea wanaweza kuharibisha zamiri yao. Na wakati zamiri inaharibika, haitakusumbua tena hata wakati unafanya jambo ingine ya mubaya.”—Heather.

  •    Itika mashauri ao malipizi yenye watakupatia. Biblia inasema: “Musikilize nizamu (ao malipizi).” (Mezali 8:33) Acha kujitetea-tetea, na uitike mashauri ao malipizi yenye wazazi watakupatia.

     “Ukilaumu wazazi juu wanakupatia malipizi fulani, utafanya mambo ikuwe nguvu tena zaidi. Itika tu vizuizi vyenye wanakutilia, usikaze akili juu ya mambo yenye hautaweza kufanya juu ya vile vizuizi.”—Jason.

  •   Fanya nguvu juu wakutumainie tena. Biblia inasema: ‘Muondoe utu wa zamani wenye unapatana na mwenendo wenu wa zamani.” (Waefeso 4:22) Kamata maamuzi ya hekima juu wazazi wako wakutumainie tena.

     “Kama unaendelea kukamata maamuzi ya hekima na kuonyesha wazazi wako kama hautafanya tena ile makosa, watakutumainia tena.”—Karen.

 SHAURI: Fanya mambo mingi zaidi ya ile yenye walikuomba, ile itawasaidia wakutumainie tena sana. Kwa mufano, wakati uko unarudia kutoka kwenye ulienda, uwaite ku telefone na kuwaonyesha kama uko mu njia, hata kama hauyapitisha saa ya kurudia ku nyumba. Ile itawasaidia wajue kama unapenda wakutumainie tena.