Zaburi 86:1-17

  • Hakuna mungu aliye kama Yehova

    • Yehova yuko tayari kusamehe (5)

    • Mataifa yote yatamwabudu Yehova (9)

    • ‘Nifundishe kuhusu njia yako’ (11)

    • “Unganisha moyo wangu” (11)

Sala ya Daudi. 86  Tega sikio lako,* Ee Yehova, nawe unijibu,Kwa maana ninateseka nami ni maskini.+   Ulinde uhai wangu,* kwa maana mimi ni mshikamanifu.+ Mwokoe mtumishi wako anayekutumaini,Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+   Nionyeshe kibali, Ee Yehova,+Kwa maana ninakulilia wewe mchana kutwa.+   Mfanye mtumishi wako ashangilie,Kwa maana ninakugeukia wewe,* Ee Yehova.   Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni mwema+ na uko tayari kusamehe;+Una upendo mwingi mshikamanifu kwa wote wanaokuitia.+   Ee Yehova, sikiliza sala yangu;Na usikilize sihi zangu za kuomba msaada.+   Ninakuitia wewe katika siku ninayotaabika,+Kwa maana utanijibu.+   Hakuna yeyote aliye kama wewe kati ya miungu, Ee Yehova,+Hakuna kazi zilizo kama kazi zako.+   Mataifa yote uliyoyaumbaYatakuja na kuinama mbele zako, Ee Yehova,+Nayo yatalitukuza jina lako.+ 10  Kwa maana wewe ni mkuu, nawe unafanya mambo yanayostaajabisha;+Wewe ni Mungu, wewe peke yako.+ 11  Nifundishe, Ee Yehova, kuhusu njia yako.+ Nitatembea katika kweli yako.+ Unganisha moyo wangu* ili niliogope jina lako.+ 12  Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+Nami nitalitukuza jina lako milele, 13  Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkuu kwangu,Nawe umeuokoa uhai wangu* kutoka katika vina vya Kaburi.*+ 14  Ee Mungu, watu wenye kimbelembele wanainuka dhidi yangu;+Kundi la wanaume wakatili wanataka kuniua,*Nao hawakuheshimu kamwe.*+ 15  Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na huruma,*Si mwepesi wa hasira, nawe una upendo mwingi mshikamanifu na uaminifu.*+ 16  Nigeukie na kunionyesha kibali.+ Mpe mtumishi wako nguvu zako,+Na umwokoe mwana wa kijakazi wako. 17  Nionyeshe ishara ya* wema wako,Ili wale wanaonichukia waione na kuaibika. Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni msaidizi wangu na mfariji wangu.

Maelezo ya Chini

Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “Ilinde nafsi yangu.”
Au “ninakuinulia wewe nafsi yangu.”
Au “Nipe moyo ambao haujagawanyika.”
Au “umeiokoa nafsi yangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “hawajakuweka mbele yao.”
Au “wanaitafuta nafsi yangu.”
Au “neema.”
Au “kweli.”
Au “uthibitisho wa.”