Zaburi 19:1-14

  • Uumbaji wa Mungu na sheria yake hutoa ushahidi

    • ‘Mbingu hutangaza utukufu wa Mungu’ (1)

    • Sheria kamilifu ya Mungu hurudisha nguvu (7)

    • “Dhambi nisizojua” (12)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 19  Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu;+Na anga lililo juu linatangaza kazi ya mikono yake.+   Siku baada ya siku zinabubujisha maneno yake,Na usiku baada ya usiku zinafunua ujuzi.   Hakuna usemi, wala hakuna maneno;Sauti zake hazisikiki.   Lakini sauti zake zimefika* katika dunia yote,Na ujumbe wake umefika mpaka kwenye miisho ya dunia inayokaliwa.+ Amepiga hema mbinguni kwa ajili ya jua;   Ni kama bwana harusi anayetoka katika chumba chake;Linashangilia kama mwanamume hodari anayekimbia kwenye njia yake.   Linachomoza kutoka mwisho mmoja wa mbingu,Nalo huzunguka mpaka mwisho mwingine;+Na hakuna chochote kinachojificha joto lake.   Sheria ya Yehova ni kamilifu,+ hurudisha nguvu.*+ Kikumbusho cha Yehova kinategemeka,+ humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.+   Maagizo kutoka kwa Yehova ni ya uadilifu, huufanya moyo ushangilie;+Amri ya Yehova ni safi, huyafanya macho yang’ae.+   Kumwogopa Yehova ni jambo safi,+ hudumu milele. Hukumu za Yehova ni za kweli; zote ni za uadilifu.+ 10  Zinatamanika kuliko dhahabu,Kuliko dhahabu nyingi bora,*+Na tamu zaidi kuliko asali,+ asali inayodondoka kutoka katika sega. 11  Mtumishi wako ameonywa kupitia hizo;+Anapozishika anapata thawabu kubwa.+ 12  Ni nani anayeweza kutambua makosa?+ Nitangaze kuwa sina hatia ya dhambi nisizojua. 13  Na unizuie mimi mtumishi wako nisitende matendo ya kimbelembele;+Usiruhusu yanitawale.+ Ndipo nitakapokuwa kamili,+Na sitakuwa na hatia ya dhambi zilizo wazi.* 14  Maneno ya kinywa changu na kutafakari kwa moyo wanguNa yakupendeze wewe,+ Ee Yehova, Mwamba wangu+ na Mkombozi wangu.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “kamba yake ya kupimia imefika.”
Au “huirudisha nafsi.”
Au “iliyosafishwa.”
Au “dhambi nyingi.”