Zaburi 146:1-10

  • Mtumaini Mungu, si wanadamu

    • Mawazo ya mwanadamu hupotea anapokufa (4)

    • Mungu huwainua juu walioinama chini (8)

146  Msifuni Yah!*+ Nafsi yangu yote na imsifu Yehova.+   Nitamsifu Yehova maisha yangu yote. Nitamwimbia sifa* Mungu wangu maadamu ninaishi.   Msiwatumaini wakuu*Wala mwanadamu, ambaye hawezi kuleta wokovu.+   Roho* yake hutoka, naye hurudi ardhini;+Siku hiyohiyo mawazo yake hupotea.+   Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaidizi wake,+Ambaye anamtumaini Yehova Mungu wake,+   Muumba wa mbingu na dunia,Wa bahari, na vyote vilivyomo,+Yeye ambaye ni mwaminifu daima,+   Yeye anayetekeleza haki kwa ajili ya waliopunjwa,Yeye anayewapa chakula* wenye njaa.+ Yehova anawaachilia huru wafungwa.*+   Yehova anafungua macho ya vipofu;+Yehova anawainua juu wale walioinama chini;+Yehova anawapenda waadilifu.   Yehova anawalinda wakaaji wageni;Humtegemeza yatima na mjane,+Lakini huivuruga mipango ya waovu.*+ 10  Yehova atakuwa Mfalme milele,+Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi baada ya kizazi. Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Nitampigia muziki.”
Au “viongozi.”
Au “Pumzi.”
Tnn., “mkate.”
Tnn., “waliofungwa.”
Au “huipotosha njia ya waovu.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.