Zaburi 37:1-40

  • Wanaomtumaini Yehova watafanikiwa

    • Usikasirishwe na waovu (1)

    • “Pata furaha tele katika Yehova” (4)

    • “Mkabidhi Yehova njia yako” (5)

    • “Wapole wataimiliki dunia” (11)

    • Waadilifu hawatakosa chakula (25)

    • Waadilifu wataishi milele duniani (29)

Wa Daudi. א [Aleph] 37  Usikasirike* kwa sababu ya waovuWala usiwaonee wivu watenda dhambi.+   Watanyauka haraka kama majani+Na kusinyaa kama majani yaliyochipuka ya kijani kibichi. ב [Beth]   Mtumaini Yehova na utende mema;+Kaa duniani,* na utende kwa uaminifu.+   Pata furaha tele* katika Yehova,Naye atatosheleza tamaa za moyo wako. ג [Gimel]   Mkabidhi* Yehova njia yako;+Mtegemee yeye, naye atatenda kwa niaba yako.+   Ataufanya uadilifu wako ung’ae kama mapambazuko,Na haki yako kama jua la adhuhuri. ד [Daleth]   Nyamaza mbele za Yehova+Na umngojee kwa matumaini.* Usikasirishwe na mtuAnayefanikiwa kutekeleza njama zake.+ ה [He]   Acha hasira na uache ghadhabu;+Usikasirike na kuanza kutenda uovu.*   Kwa maana waovu wataangamizwa,+Lakini wale wanaomtumaini Yehova wataimiliki dunia.+ ו [Waw] 10  Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena;+Utapaangalia mahali walipokuwa,Nao hawatakuwepo.+ 11  Lakini wapole wataimiliki dunia,+Nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani.+ ז [Zayin] 12  Mtu mwovu hupanga njama dhidi ya mwadilifu;+Humsagia meno yake. 13  Lakini Yehova atamcheka,Kwa maana Anajua kwamba siku yake itakuja.+ ח [Heth] 14  Waovu huchomoa panga zao na kuzikunja* pinde zaoIli kumwangusha chini aliyekandamizwa na pia maskini,Ili kuwachinja wale ambao njia yao imenyooka. 15  Lakini upanga wao utauchoma moyo wao wenyewe;+Pinde zao zitavunjwa. ט [Teth] 16  Kidogo alicho nacho mwadilifu ni boraKuliko wingi wa vitu walivyo navyo watu wengi waovu.+ 17  Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa,Lakini Yehova atawategemeza waadilifu. י [Yod] 18  Yehova anajua mambo wanayokabili watu wasio na lawama,*Na urithi wao utadumu milele.+ 19  Hawataaibishwa wakati wa msiba;Wakati wa njaa kali watakuwa na chakula tele. כ [Kaph] 20  Lakini waovu wataangamia;+Maadui wa Yehova watatoweka kama malisho bora kabisa;Watatoweka kama moshi. ל [Lamed] 21  Mwovu hukopa lakini halipi,Lakini mwadilifu ni mkarimu* naye hutoa.+ 22  Wale Anaowabariki wataimiliki dunia,Lakini wale Anaowalaani wataangamizwa.+ מ [Mem] 23  Yehova huongoza* hatua za mtu+Njia ya mtu huyo inapompendeza Yeye.+ 24  Hata akianguka, hataangushwa chini kabisa,+Kwa maana Yehova anaushika mkono wake na kumtegemeza.*+ נ [Nun] 25  Nilikuwa kijana lakini sasa nimezeeka,Lakini sijamwona mtu yeyote mwadilifu akiwa ameachwa,+Wala watoto wake wakitafuta mkate.*+ 26  Sikuzote anakopesha bila faida,+Na watoto wake watapata baraka. ס [Samekh] 27  Acha uovu, utende mema,+Nawe utaishi milele. 28  Kwa maana Yehova anapenda haki,Naye hatawaacha washikamanifu wake.+ ע [Ayin] Watalindwa sikuzote;+Lakini wazao wa waovu wataangamizwa.+ 29  Waadilifu wataimiliki dunia,+Nao wataishi humo milele.+ פ [Pe] 30  Kinywa cha mwadilifu hufundisha hekima,*Na ulimi wake huongea kuhusu haki.+ 31  Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake;+Hatua zake hazitayumbayumba.+ צ [Tsade] 32  Mwovu humtazama mwadilifu,Akitafuta kumuua. 33  Lakini Yehova hatamwacha mikononi mwa mtu huyo+Wala hatampata na hatia anapohukumiwa.+ ק [Qoph] 34  Mtumaini Yehova na ufuate njia yake,Naye atakukweza uimiliki dunia. Waovu watakapoangamizwa,+ utaona jambo hilo.+ ר [Resh] 35  Nimemwona mtu mkatili, mwovuAkisambaa kama mti wenye majani mengi katika udongo wake wa asili.+ 36  Lakini alikufa ghafla naye akatoweka;+Niliendelea kumtafuta, lakini sikuweza kumpata.+ ש [Shin] 37  Mwangalie mtu asiye na lawama,*Na uendelee kumwangalia mnyoofu,+Kwa maana wakati ujao wa mtu huyo utakuwa na amani.+ 38  Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa;Wakati ujao wa watu waovu utakomeshwa.+ ת [Taw] 39  Wokovu wa watu waadilifu unatoka kwa Yehova;+Yeye ndiye ngome yao wakati wa taabu.+ 40  Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+ Atawanusuru kutoka kwa waovu na kuwaokoa,Kwa sababu wanamkimbilia yeye.+

Maelezo ya Chini

Au “Usiwake hasira.”
Au “nchini.”
Au “Pata shangwe nyingi sana.”
Tnn., “Mvingirishie.”
Au “subira.”
Au labda, “Usikasirike, kwa maana hasira itakuongoza tu kwenye madhara.”
Au “kuzitia nyuzi.”
Tnn., “siku za wasio na lawama.”
Au “hufadhili.”
Au “huimarisha.”
Au “anamtegemeza kwa mkono Wake.”
Au “chakula.”
Au “huzungumza hekima kwa sauti ya chini.”
Au “mtu anayeshika utimilifu.”