Zaburi 77:1-20

  • Sala ya wakati wa taabu

    • Kutafakari kazi za Mungu (11, 12)

    • ‘Ee Mungu, ni nani aliye mkuu kama wewe?’ (13)

Kwa kiongozi; mtindo wa Yeduthuni.* Muziki wa Asafu.+ 77  Kwa sauti yangu nitamlilia Mungu;Nitamlilia Mungu kwa sauti kubwa, naye atanisikia.+   Katika siku ya taabu yangu ninamtafuta Yehova.+ Usiku ninamnyooshea mikono yangu bila kuacha.* Siwezi* kufarijiwa.   Ninapomkumbuka Mungu, ninalia kwa maumivu;+Ninataabika na nguvu zangu zinaniishia.*+ (Sela)   Unazishika kope zangu ili nisifumbe macho;Nimefadhaika, nami siwezi kuongea.   Mawazo yangu yanarudi katika siku za zamani za kale,+Miaka mingi iliyopita.   Wakati wa usiku ninaukumbuka wimbo wangu;*+Ninatafakari moyoni mwangu;+Ninatafuta* kwa bidii.   Je, Yehova atatutupa mbali milele?+ Je, hatatuonyesha tena kamwe kibali chake?+   Je, upendo wake mshikamanifu utakoma milele? Je, ahadi yake itakosa kutimia katika vizazi vyote?   Je, Mungu amesahau kuonyesha kibali chake,+Au je, hasira yake imekomesha rehema yake? (Sela) 10  Je, ni lazima niendelee kusema: “Hili ndilo linalonitaabisha:*+ Aliye Juu Zaidi amebadili msimamo wake kutuelekea”?* 11  Nitazikumbuka kazi za Yah;Nitayakumbuka matendo yako yanayostaajabisha ya zamani za kale. 12  Nitautafakari utendaji wako woteNa kutafakari shughuli zako.+ 13  Ee Mungu, njia zako ni takatifu. Ee Mungu, ni mungu gani aliye mkuu kama wewe?+ 14  Wewe ndiye Mungu wa kweli, unayetenda mambo yanayostaajabisha.+ Umeyafunulia mataifa nguvu zako.+ 15  Kwa nguvu zako* umewaokoa* watu wako,+Wana wa Yakobo na wa Yosefu. (Sela) 16  Maji yalikuona, Ee Mungu,Maji yalikuona yakavurugika.+ Na vilindi vya maji vikatibuka. 17  Mawingu yakamwaga maji. Anga lenye mawingu likanguruma,Na mishale yako ikaruka huku na kule.+ 18  Sauti ya mngurumo+ wako ilikuwa kama magurudumu ya gari la vita;Mimweko ya radi iliangaza dunia inayokaliwa;*+Dunia ilitikisika na kutetemeka.+ 19  Njia yako ilipita baharini,+Kijia chako kilipita katika maji mengi;Lakini nyayo zako hazingeweza kuonekana. 20  Uliwaongoza watu wako kama kundi la kondoo,+Chini ya uangalizi* wa Musa na Haruni.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Tnn., “bila kufa ganzi.”
Au “Nafsi yangu haiwezi.”
Tnn., “roho yangu inazimia.”
Au “muziki wangu wa nyuzi.”
Tnn., “Roho yangu inatafuta.”
Tnn., “amebadili mkono wake wa kuume dhidi yetu.”
Au “linalonichoma.”
Tnn., “mkono wako.”
Tnn., “umewakomboa.”
Au “ardhi inayozaa.”
Tnn., “Kwa mkono.”