Zaburi 100:1-5

  • Kumshukuru Muumba

    • “Mtumikieni Yehova kwa kushangilia” (2)

    • ‘Ni Mungu aliyetuumba’ (3)

Muziki wa shukrani. 100  Mpazieni Yehova sauti ya ushindi, dunia yote.+   Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+ Njooni mbele zake kwa kelele za shangwe.   Jueni* kwamba Yehova ni Mungu.+ Yeye ndiye aliyetuumba, na sisi ni mali yake.*+ Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+   Ingieni katika malango yake kwa shukrani,+Katika nyua zake kwa sifa.+ Mshukuruni yeye; lisifuni jina lake.+   Kwa maana Yehova ni mwema;+Upendo wake mshikamanifu unadumu milele,Na uaminifu wake katika vizazi vyote.+

Maelezo ya Chini

Au “Tambueni.”
Au labda, “hatukujiumba wenyewe.”