Zaburi 115:1-18

  • Mungu peke yake ndiye anayepaswa kutukuzwa

    • Sanamu zisizo na uhai (4-8)

    • Wanadamu wamepewa dunia (16)

    • “Watu waliokufa hawamsifu Yah” (17)

115  Usitutukuze sisi, Ee Yehova, usitutukuze sisi,*Bali litukuze jina lako+Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.+   Kwa nini mataifa yaseme: “Yuko wapi Mungu wao?”+   Mungu wetu yuko mbinguni;Hufanya lolote apendalo.   Sanamu zao ni fedha na dhahabu,Kazi ya mikono ya mwanadamu.+   Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+Zina macho, lakini haziwezi kuona;   Zina masikio, lakini haziwezi kusikia;Zina pua, lakini haziwezi kunusa;   Zina mikono, lakini haziwezi kugusa;Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+Hazitoi sauti yoyote kwa koo zake.+   Watu wanaozitengeneza watakuwa kama sanamu hizo,+Na pia wote wanaozitumaini.+   Ee Israeli, mtumainini Yehova+—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.+ 10  Ee nyumba ya Haruni,+ mtumainini Yehova;—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu. 11  Ninyi mnaomwogopa Yehova, mtumainini Yehova+—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.+ 12  Yehova anatukumbuka na atatubariki;Ataibariki nyumba ya Israeli;+Ataibariki nyumba ya Haruni. 13  Atawabariki wale wanaomwogopa Yehova,Wadogo kwa wakubwa. 14  Yehova atawapa ongezeko,Ninyi na watoto* wenu.+ 15  Yehova na awabariki,+Muumba wa mbingu na dunia.+ 16  Mbingu ni za Yehova,+Lakini dunia amewapa wanadamu.+ 17  Watu waliokufa hawamsifu Yah;+Wala yeyote anayeshuka kwenye ukimya wa kifo.*+ 18  Lakini sisi tutamsifu YahKuanzia sasa mpaka milele. Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au “Hatustahili chochote, Ee Yehova, hatustahili chochote.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “kwenye kimya.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.