Zaburi 127:1-5

  • Bila Mungu, kila kitu ni bure

    • “Yehova asipoijenga nyumba” (1)

    • Watoto ni thawabu kutoka kwa Mungu (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani. 127  Yehova asipoijenga nyumba,Wale wanaoijenga wanafanya kazi ngumu ya bure.+ Yehova asipolilinda jiji,+Mlinzi anakesha bure.   Mnajisumbua bure kuamka mapema,Na kuchelewa kulala,Mkitaabika kupata chakula,Kwa maana yeye huwaandalia anaowapenda na kuwapa usingizi.+   Tazama! Watoto* ni urithi kutoka kwa Yehova;+Uzao wa tumbo ni thawabu.+   Kama mishale mkononi mwa mwanamume hodari,Ndivyo walivyo watoto ambao mtu anawazaa akiwa kijana.+   Mwenye furaha ni mwanamume anayelijaza podo lake watoto.+ Hawataaibishwa,Kwa maana watazungumza na maadui katika lango la jiji.

Maelezo ya Chini

Au “Wana.”