Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Onyesha Adabu Unapopokea ao Unapotuma Ujumbe Kwenye Telefone

Onyesha Adabu Unapopokea ao Unapotuma Ujumbe Kwenye Telefone

TATIZO

Wazia unazungumuza uso kwa uso na rafiki wako, kisha unapokea ujumbe kwenye telefone. Unaweza kufanya nini?

  1. Kusoma ujumbe huo ukizungumuza na rafiki yako.

  2. Kumuambia rafiki yako “Tafazali univumilie kidogo ili nisome kwanza ujumbe.”

  3. Kuacha ujumbe huo na kuendelea na mazungumuzo.

Je, uamuzi ambao unaweza kufanya ni wa maana? Jibu ni ndiyo!

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Kutumia rafiki fulani ujumbe wakati unazungumuza na mwengine ni kama vile kucheza muchezo ambao unapenda sana bila kuheshimu sheria za muchezo huo. Unaweza kusema ‘lakini hawa si ni marafiki wangu.’ Kwa kuwa ni hivyo, basi unapaswa kuwa na adabu. Hilo halimaanishe kwamba unapaswa kujitilia sheria nyingi na kuwa na adabu sana. Lakini ukweli ni huu: Ikiwa hauonyeshe adabu kwa marafiki wako, siku moja watakukimbia.

Sababu gani? Kwa sababu watu hawapendi mutu anayewatendea bila adabu. Binti mumoja, anayeitwa Beth * alisema hivi: “Sifurahi wakati kila mara rafiki fulani anaangalia telefone yake ninapoongea naye, ni kama vile iko anangojea jambo fulani ambalo ni la maana kuliko mazungumuzo yetu!” Unawaza Beth ataendelea kuvumilia kuwa na rafiki wa namna hiyo mupaka siku gani?

Chunguza tabia ambazo unaonyesha wakati unatumia telefone, soma tena mufano wa kuwaziwa ulio chini ya kichwa “Tatizo.” Wewe unawaza mutu anapaswa kufanya nini? Pengine, unatambua kwamba Uamuzi A ni kukosa adabu. Lakini unawaza nini juu ya uamuzi B na C? Unawaza ni kukosa adabu ikiwa mutu anakatiza mazungumuzo ili tu kuangalia ujumbe kwenye telefone? Ao unawaza ni kukosa adabu ikiwa mutu anaacha kusoma ujumbe ambao amepokea ili tu aendelee na mazungumuzo?

Namna unajua, inaweza kuwa vigumu kujua ikiwa kufanya jambo fulani ni kukosa adabu ao hapana. Lakini Biblia inaweza kusaidia. Inasema hivi: ‘Kama vile munavyotaka watu wawatendee ninyi, muwatendee wao vivyo hivyo.’ (Luka 6:31) Unaweza kutumia shauri hilo kuhusu kutuma na kupokea ujumbe kwenye telefone. Namna gani?

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Tuma ujumbe kwa wakati unaofaa tu. Kijana mumoja anayeitwea Richard anasema hivi: “Wakati fulani ninapokea ujumbe usiku sana. Na hata hauhusu jambo fulani la maana, na unavuruga usingizi wangu!” Jiulize: ‘Je, ninatumia watu ujumbe wakati ambao wanaweza kuwa wakipumuzika?’ —Kanuni ya Biblia: Mhubiri 3:1.

Tumia maneno ya kuonyesha adabu. Mutu anaweza kuzungumuza kupitia maneno, kubadilika kwa sauti, ishara za uso, na ishara za mwili. Lakini, mambo yote hayo hayawezi kuonekana katika ujumbe unaotuma. Kwa hiyo, unaweza kufanya nini? Mwanamuke mumoja anayeitwa Jasmine anatoa shauri hili: “Tumia maneno ya kawaida ya kuonyesha adabu. Unaweza kuuliza, ‘Uko muzuri?’ na utumie maneno kama vile ‘tafazali’ na ‘asante.’”—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 4:6.

Tenda kwa hekima. Soma tena mufano wa kuwaziwa ulio chini ya kichwa “Tatizo.” Ikiwa uko unangojea ujumbe wa maana, inaweza kuwa vizuri umuombe mutu ambaye unazungumuza naye akuvumilie kidogo. Lakini, katika hali nyingi, unaweza kusoma ujumbe huo wakati mwingine. Amy, mwenye miaka 17, anasema hivi: “Wakati utamaliza kuongea na rafiki yako, telefone yako itakuwa ingali pale, lakini pengine rafiki yako hatakuwa hapo wakati utamaliza kusoma ao kutuma ujumbe.” Unaweza kufanya hivyo pia unapokuwa kwenye mukutano fulani. Jane, mwenye miaka 18, anasema hivi: “Usitume ujumbe kila wakati. Hilo linaweza kuwafanya watu ambao unazungumuza nao wafikiri kwamba haufurahie kuwa pamoja nao, ao ungependa uwe mahali pengine.”

Fikiri mbele ya kutuma ujumbe. Ujumbe wako unaweza kueleweka mubaya? Kutumia alama katika ujumbe kunaweza kuonyesha kabisa namna unajisikia? Amber, mwenye miaka 21, anasema hivi: “Ikiwa unapenda kufanya zihaka juu ya kitu fulani, tia alama ya mutu anayecheka katika ujumbe wako. Watu wanaumizwa moyoni, na wanaweza hata kuanza kupigana kwa sababu wanachukua kwa uzito maneno ambayo mutu anasema ili kufanya zihaka.”—Kanuni ya Biblia: Methali 12:18.

Bila shaka, ni lazima uonyeshe adabu unapopokea na unapotuma ujumbe kwenye telefone!

Fikiri kidogo: Ni upendo ndio unatuchochea kuonyesha adabu. Namna gani unaweza kuonyesha upendo? Biblia inasema hivi: ‘Upendo ni wenye [uvumilivu] na wenye fazili. Upendo hauna wivu, haujigambi, haujivune, haujiendeshe bila adabu, hautafute faida zake wenyewe, hauchokozeke.’ (1 Wakorintho 13:4, 5) Ni njia gani ya kuonyesha upendo ambayo unapaswa kufanyia maendeleo?

^ fu. 11 Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.