Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 4

Yesu Kristo Ni Nani?

Yesu Kristo Ni Nani?

1. Yesu alitoka wapi?

Yesu alikuwa na sifa gani zenye zilifanya watu wasiogope kumukaribia?​—MATAYO 11:29; MARKO 10:13-16.

Yesu hakukuwa kama wanadamu wengine wote, juu mbele azaliwe hapa ku dunia alikuwa anaishi mbinguni; kule alikuwa malaika. (Yohana 8:23) Yeye njo Mungu aliumba wa kwanza, na alimusaidia Mungu kuumba vitu vingine vyote. Yeye tu njo Yehova aliumba moja kwa moja, njo maana anaitwa Mwana “muzaliwa-pekee” wa Mungu. (Yohana 1:14) Tena Yesu anaitwa “Neno,” juu yeye njo alikuwa musemaji wa Mungu.​—Soma Mezali 8:22, 23, 30; Wakolosai 1:15, 16.

2. Juu ya nini Yesu alikuja ku dunia?

Mungu alituma Mwana wake ku dunia kwa kutosha uzima wake mbinguni na kuuhamishia mu tumbo la uzazi la bikira Muyahudi mwenye aliitwa Maria. Kwa hiyo, baba ya Yesu hakukuwa mwanadamu. (Luka 1:30-35) Yesu alikuja ku dunia ili (1) kutufundisha kweli juu ya Mungu, (2) kutuonyesha namna tunaweza kufanya mapenzi ya Mungu hata wakati tuko na magumu, na (3) kutoa uzima wake mukamilifu kuwa “bei ya ukombozi.”​—Soma Matayo 20:28.

3. Juu ya nini tuko na lazima ya bei ya ukombozi?

Bei ya ukombozi ni bei yenye inalipwa ili kukomboa mutu mwenye kuwa mu hatari ya kifo. (Kutoka 21:29, 30) Wakati Mungu aliumba watu, hakupenda siku fulani wazeeke na kufa. Ni nini inaonyesha vile? Mungu aliambia Adamu, mutu wa kwanza, kama akifanya “zambi” atakufa. Kwa hiyo, kama Adamu hangefanya zambi, hangekufa hata siku moja. (Mwanzo 2:16, 17; 5:5) Biblia inasema kama kifo ‘kiliingia’ mu dunia kupitia Adamu. Basi, watoto wote wa Adamu waliriti kutoka kwake zambi na azabu ao malipizi ya zambi, ni kusema, kifo. Tuko na lazima ya bei ya ukombozi ili tukombolewe kutoka katika azabu ya kifo yenye tuliriti kutoka kwa Adamu.​—Soma Waroma 5:12; 6:23.

Ni nani angelipa bei ya ukombozi ili kutukomboa kutoka katika kifo? Wakati mutu anakufa, analipia deni la zambi zake mwenyewe. Hakuna mutu yeyote mwenye haiko mukamilifu mwenye anaweza kulipia deni la zambi za watu wengine.​—Soma Zaburi 49:7-9.

4. Juu ya nini Yesu alikufa?

Yesu hakukuwa na zambi kama sisi, alikuwa mukamilifu. Kwa hiyo, hakupaswa kufa kwa ajili ya zambi zake, juu hakufanya hata zambi moja. Lakini, alikufa juu ya zambi za wengine. Mungu alionyesha kama anapenda watu sana, wakati alimutuma Mwana wake ili akufe kwa ajili yetu. Yesu naye alionyesha kama anatupenda kwa sababu alimutii ao kumusikia Baba yake na akatoa uzima wake juu ya zambi zetu.​—Soma Yohana 3:16; Waroma 5:18, 19.

Angalia video Sababu Gani Yesu Alikufa?

5. Yesu iko anafanya nini leo?

Wakati Yesu alikuwa ku dunia, aliponyesha wagonjwa, alifufua watu wenye walikuwa wamekufa, na alisaidia watu wenye walikuwa wanateseka. Kwa kufanya vile, alionyesha mambo yenye atafanya wakati wenye kuja kwa ajili ya watu wote wenye kumutii Mungu. (Matayo 15:30, 31; Yohana 5:28) Kisha Yesu kufa, Mungu alimufufua akiwa kiumbe wa roho. (1 Petro 3:18) Yesu alingojea kwenye mukono wa kuume wa Mungu mpaka wakati Mungu alimupatia mamlaka ya kuwa Mufalme juu ya dunia yote. (Waebrania 10:12, 13) Sasa Yesu ni Mufalme mwenye kutawala mbinguni, na wanafunzi wake wanatangaza habari hiyo njema mu dunia yote.​—Soma Danieli 7:13, 14; Matayo 24:14.

Kwa sababu Yesu ni Mufalme, hivi karibuni, atatumia mamlaka yake ili kumaliza mateso yote na kuharibu wale wote wenye kuleta mateso. Wale wote wenye wanamuamini Yesu na kumutii watapata uzima wa milele mu Paradiso ku dunia.​—Soma Zaburi 37:9-11.